Kwenye janga hili la Corona, sisi wanasayansi tunaposema kuwa "Rais Magufuli amekuja na chai" huwa hatuziweki maanani

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Uthibitisho wa kupungua kwa Corona nchini ni lazima utolewe kwa kupewa scientific data kitu ambacho si Rais wala waziri wa afya wanacho. Wanatoa tu maoni yao kwa kutumia hisia jambo ambalo kwa kiongozi mwenye vyombo kufanya ni ukosefu wa maarifa.

Ukiwasikiliza mawaziri mfano Kabudi ni kama unaona kabisa hawaelewi chochote kuhusu mwenendo wa janga hili. Ni kama wako gizani wanapapasa. Aidha ukimsikiliza waziri wa afya Ummy Mwalimu halafu ukamsikiliza Rais Magufuli hasa hapa "Ukiwa vitani hakuna kubembelezana" unaona kabisa waziri Ummy alikuwa anashurutishwa kufanya mambo ambayo yapo nje ya taratibu.

Sasa basi, kwa kuwa hawana data zozote kuthibitisha kile wanachokinena, majukumu yote ya kupambana na janga hili ameachiwa Mwananchi huku huyo mwananchi akihakikisha kuwa Magufuli anapata stahiki zake za kodi kama kawaida.

Kwa Magufuli maneno "Uchumi kwanza" ni yakuchukuliwa kwa tahadhari kubwa sana na hasa akitazamwa mwenendo wake dhidi ya utu wa binadamu! Kwake yeye ni "Hakikisha unaleta mapato" haijalishi uko katika hali gani na unapambana na nini.

Niseme, kiongozi yeyote aliye na uwezo wa kiuongozi hawezi kuja hadharani kwa staili ya Magufuli. Haya ni mapungufu makubwa kwa kiongozi kuja na jambo linalohitaji ulinganifu wa kisayansi kisha ukaja staili kama ya Magufuli isiyo na takwimu yoyote ile kuthibitisha kile anachonena. Sisi wanansayansi hizo tunaita "Chai" na tunazipuuza mara moja.

Hakuna uthibitisho wowote wa kile anachoeleza Rais Magufuli kuhusiana na janga la Corona hivyo basi chukua tahadhari wewe na jamii yote unayohudumia kama unaipenda. Chukua tahadhari huku ukijua kuwa watanzania wenzetu zaidi ya hao 16 waliotangazwa wamekufa kwa Corona. Wamekufa na hakuna aliyejali baada ya hapo na ndiyo maana tunaambiwa kila kitu kiende kama kawaida.

Ukimtazama Magufuli kwa haya utamfahamu ni mtu wa aina gani.
1. Unakataa vifaa vya msaada vya kupambana na huu ugonjwa kwa kuhofia hujuma huku unaruhusu utalii.

2. Unakataa kutoa takwimu halisi hadharani huku unasema ugonjwa unapungua.

Kwa hayo mawili "Kuwa na akili za mbayuwayu"
 
Magufuli mjanja. Anajua akitoa data watu wataongea, maana kusema ukweli data ni mbaya. Inabidi sasa aseme uongo tu ili wananchi wajue kila kitu kipo sawa.

Ila Coronavirus haina simile. Itampiga Magu Magu mwenyewe hapo ndo sense itamjia.
 
Hivi wanasayansi mkoje? Mh. Rais pia ni mwanasayansi .. yeye ndiye mwenye mamlaka ya kutamka kila kitu kinacho husika na Usalama wetu. TUMPONGEZE MH. RAIS DR. MAGUFULI TWENDE KAZI
 
Hao wagonjwa wa corona wamejuaje kuwa wanaumwa corona wakati maabara inafanyiwa uchunguzi?
Iko hivi. Hospitalini hakuna watu wanaoenda wakiwa na dalili za Corona sasa unataka Serikali ipite kila nyumba inauliza "wewe unaumwa Corona", nk. Sijui kama umenipata Sky. Mloganzila wameisha pako almost empty eti!
 
Uthibitisho wa kupungua kwa Corona nchini ni lazima utolewe kwa kupewa scientific data kitu ambacho si Rais wala waziri wa afya wanacho. Wanatoa tu maoni yao kwa kutumia hisia jambo ambalo kwa kiongozi mwenye vyombo kufanya ni ukosefu wa maarifa.

Ukiwasikiliza mawaziri mfano Kabudi ni kama unaona kabisa hawaelewi chochote kuhusu mwenendo wa janga hili. Ni kama wako gizani wanapapasa. Aidha ukimsikiliza waziri wa afya Ummy Mwalimu halafu ukamsikiliza Rais Magufuli hasa hapa "Ukiwa vitani hakuna kubembelezana" unaona kabisa waziri Ummy alikuwa anashurutishwa kufanya mambo ambayo yapo nje ya taratibu.

Sasa basi, kwa kuwa hawana data zozote kuthibitisha kile wanachokinena, majukumu yote ya kupambana na janga hili ameachiwa Mwananchi huku huyo mwananchi akihakikisha kuwa Magufuli anapata stahiki zake za kodi kama kawaida.

Kwa Magufuli maneno "Uchumi kwanza" ni yakuchukuliwa kwa tahadhari kubwa sana na hasa akitazamwa mwenendo wake dhidi ya utu wa binadamu! Kwake yeye ni "Hakikisha unaleta mapato" haijalishi uko katika hali gani na unapambana na nini.

Niseme, kipngozi yeyote aliye na uwezo wa kiuongozi hawezi kuja hadharani kwa staili ya Magufuli. Haya ni mapungufu makubwa kwa kiongozi kuja na jambo linalohitaji ulinganifu wa kisayansi kisha ukaja staili kama ya Magufuli. Sisi wanansayansi hizo tunaita "Chai" na tunazipuuza mara moja.

Hakuna uthibitisho wowote wa kile anachoeleza Rais Magufuli kuhusiana na janga la Corona.
Hili si suala la kiafya tena,ni suala la kiusalama zaidi.Uanasayansi wako uweke pembeni kwa sasa.
 
Back
Top Bottom