Kwenu waheshimiwa Patrobas Katambi(DC Dodoma) na Godwin Kunambi(mkurugenzi jiji Dodoma)

danymTZ

JF-Expert Member
Jan 17, 2014
375
568
Ndugu waheshimiwa Katambi na Kunambi kwa heshima kubwa naomba niwashauri jambo moja. Wengi wanaweza kuliona halina maana lakini naamini mkilitekeleza hili itakuwa ni heshima kubwa kwa mh. Rais wetu JPM.

USHAURI:Fanyeni maamuzi ya kufunga ndoa na kufanya harusi kwa wakati mmoja na sehemu moja.(yaani KWA PAMOJA).

Sababu za kuwashauri hili ni kama ifuatavyo
1: Heshima kwa mheshimiwa Rais wetu JPM. Heshima aliyowapa mh Rais ya kuwaomba hadharani muoe ni kubwa sana hivyo namna pekee ya kuonyesha heshima na utii kwa mh Rais ni kuoa tena kwa pamoja.

2: Sababu ya pili ni muhimu pia japo haina uhakika. Mkimualika mheshimiwa Rais kwenye harusi yenu naamini ataichukulia kwa uzito wake na naamini ataweza kuhudhulia harusi yenu. Itakuwa historia nzuri na kubwa sana kwenu na familia zenu kama harusi yenu itauzuliwa na Rais wa nchi. Ni mara chache sana hili hutokea.

3:Sababu ya tatu ni kuwa mtamthibitishia mh Rais kuwa mnafanya kazi ya kuleta maendeleo Dodoma kwa ushirikiano na upendo mkubwa. Ni juzi tu mh Rais katengua viongozi watatu wa jiji la Arusha kwa sababu zinazosemekana kuwa ni kutoshirikiana na kutoelewana katika utendaji kazi wao. Hivyo mtakuwa mmeonyesha mfano mzuri wa ushirikiano hata katika mambo yenu binafsi.

Mwisho kabisa naomba msisahau kunialika,itakuwa heshima kubwa sana kwangu.
Ahsanteni.
 
Kuoa ni mchakato. Waache wafaidi kwanza ujana wao. Muda ukifika wataoa tu. Kuoa kwa shinikizo tu kutoka kwa mtu fulani, ni hatari sana hasa pale mhusika atakapo chagua mtu ambaye si sahihi kwake.
 
Hivi hawa jamaa wana ata watoto wa their early twenties kweli....nin kinawapa kiburi cha namna hyo? Mie nko below 30, sijaoa ila nina mtoto wangu ana 6years, but still nina ratba ya kuoa soon ata before kufkia 30, hao jamaa wana shda gani?
 
Kuoa inahitaji kujipanga mkuu. Yawezekana bado wanajipanga
Hivi hawa jamaa wana ata watoto wa their early twenties kweli....nin kinawapa kiburi cha namna hyo? Mie nko below 30, sijaoa ila nina mtoto wangu ana 6years, but still nina ratba ya kuoa soon ata before kufkia 30, hao jamaa wana shda gani?
 
Kuoa inahitaji kujipanga mkuu. Yawezekana bado wanajipanga
Mkuu, suala la kuoa ni maamuzi tu,sio mipango ya kutisha.
Ukisema kujipanga sana kamwe huwez oa kwan hakunaga mwsho wa kujipanga mkuu, ni sawa na utafutaji wa mali....hakunaga mwho mkuu. ukiona mwsho ujue umekufa.
 
Uko sahihi,japo kuna mambo inabidi uwe na uhakika nayo kwanza. Mahiyaji muhimu kama makazi,chakula, afya na elimu kwa watoto inabidi viwe certain kwanza
Mkuu, suala la kuoa ni maamuzi tu,sio mipango ya kutisha.
Ukisema kujipanga sana kamwe huwez oa kwan hakunaga mwsho wa kujipanga mkuu, ni sawa na utafutaji wa mali....hakunaga mwho mkuu. ukiona mwsho ujue umekufa.
 
Kuoa nako ni mapenzi ya Mungu, unaweza kushauri mtu aowe baada ya kuona muda unaelekea jioni lakini muhimu ni kujua kwa nini kijana huyu haoi wakati jioni yake inakaribia. inawezekana ushauri wako ukawa hauna maana kwa kuwa inawezekana kijana mwenyewe pengine sio riziki.
 
Ushauri wa kuoa wamepewa na mh Rais. Mimi nimewaongezea tu ushauri mwingine kuwa wakiamua kuoa waoe kwa pamoja. Siyo lazima sana lakini pia siyo mbaya
Kuoa nako ni mapenzi ya Mungu, unaweza kushauri mtu aowe baada ya kuona muda unaelekea jioni lakini muhimu ni kujua kwa nini kijana huyu haoi wakati jioni yake inakaribia. inawezekana ushauri wako ukawa hauna maana kwa kuwa inawezekana kijana mwenyewe pengine sio riziki.
 
Back
Top Bottom