Kwenu wadada

henry kilenga

JF-Expert Member
Mar 4, 2015
1,329
1,117
Y.O.L.O: Wanawake wengi wamekua wakiuliza wafanye nini ili wanaume zao wa-propose?

Nafikiri hili si swali sahihi.

Sababu zinazofanya niseme sio swali sahihi ni kwa sababu linawaweka wanawake katika pressure kubwa ya kufanya jambo lolote alimradi mwanaume amuoe.

Na bahati mbaya jamaa haoi. Mwanamke anaishia kuchanganyikiwa na kujiuliza "pamoja na yote niliyomfanyia ameniacha na kuoa mwingine?"

Ndio! ni kwa sababu ni vigumu sana kumlazimisha mwanaume akuoe labda kama ameamua kuoa. Na kiuhalisia kadiri unavyomlazimisha ndivyo unavyomuweka mbali kabisa na wewe.

Kwaio lipi swali sahihi sasa?

Nafikiri swali sahihi ni: Kwanini akuoe wewe? Sasa tunaweza tukalijibu hili swali. Lakini kabla ya kulijibu, ngoja niulize swali lingine:

Kama kwa mfano wewe mwanamke unae mtoto wa kiume na huyo mtoto wako amekuletea mwanamke aliye kama wewe nikimaanisha mnafanana tabia na mambo mengine na kukwambia 'mama, nataka kumuoa huyu mwanamke..' utamkubalia kwa moyo mweupe kabisa amuoe??

Jitizame tabia yako, mambo unayofanya, attitude yako juu ya wazazi na ndugu wa huyo mwanaume wako...je ni aina ya mwanamke ambae ungekubali mwanao amuoe?. Baada ya kujijibu hilo swali. Jijibu na hili:

Kwanini akuoe wewe?..na tatizo unafikiri mwanaume wako haoni attitude mbaya au nzuri uliyonayo..anaiona sana sema amebaki kimya kwa vile anajua utambishia kama utakavyoipinga hii makala yangu...hivyo amekuacha tu huku akiangalia mwanamke mwingine wa ku-propose!

Pia ni nini mtizamo wako wa kimaisha? Dada yangu kila mwanamke anao uwezo wa kuweka foundation na make ups usoni, kila mwanamke anao uwezo wa kuweka nywele, kila mwanamke anao uwezo wa kuongeza hips ma makalio yake.

Kila mwanamke endapo atafundishwa anao uwezo wa kumpagawisha mwanaume kitandani mpaka aka-vibrate kama Nokia tochi ya zamani.

Lakini unajua nini? Yote hayo yananunulika na pesa tu! Mwanaume anao uwezo wa kumlipia mwanamke na akayapata yote hayo bila ya kelele na stress za kila siku!

Hivyo basi, kwanini akuoe wewe?

Anatafuta mwanamke mwenye attitude na mtizamo bora. Tabia na siha njema hazifundishwi wala kununuliwa...mwanaume bora anatafuta mwanamke mwenye attitude nzuri..hayo mengine yananunulika na kufundishika.

Jambo bora kabisa kwako ni kuwa mwanamke wa msimamo mwenye siha na tabia njema. Muache akupende na akuoe kwa hilo tu.

Acha kuhangaika na kupigania mwanaume kukuoa. Kuwa wewe kama wewe. Nimegundua wanawake wengi wanaotamani ndoa wako vizuri kitabia sasa kutokana na pressure za marafiki, hofu ya umri na msukumo wa jamii kiujumla wanalazimisha ndoa kwa kufanya vitu ambavyo baadae vinawagharimu!

Kuwa mwanamke ambae ataona ni vigumu kwake bila wewe....usimpe mambo ambayo mwanamke mwingine yeyote anaweza kumpa.

Kama atakupenda wewe kama ulivyo na sio kwa sababu ya nywele za brazil au the way unavovaa basi hawezi kupenda kwingine.

Na hapo atakuwa na kila sababu ya kukuoa wewe. Na kama asipokuoa huyo mwanaume akapimwe akili huenda uvulana bado upo kichwani mwake!

My sister be real...and go get your man!!

By henry
 
Y.O.L.O: Wanawake wengi wamekua wakiuliza wafanye nini ili wanaume zao wa-propose?

Nafikiri hili si swali sahihi.

Sababu zinazofanya niseme sio swali sahihi ni kwa sababu linawaweka wanawake katika pressure kubwa ya kufanya jambo lolote alimradi mwanaume amuoe.

Na bahati mbaya jamaa haoi. Mwanamke anaishia kuchanganyikiwa na kujiuliza "pamoja na yote niliyomfanyia ameniacha na kuoa mwingine?"

Ndio! ni kwa sababu ni vigumu sana kumlazimisha mwanaume akuoe labda kama ameamua kuoa. Na kiuhalisia kadiri unavyomlazimisha ndivyo unavyomuweka mbali kabisa na wewe.

Kwaio lipi swali sahihi sasa?

Nafikiri swali sahihi ni: Kwanini akuoe wewe? Sasa tunaweza tukalijibu hili swali. Lakini kabla ya kulijibu, ngoja niulize swali lingine:

Kama kwa mfano wewe mwanamke unae mtoto wa kiume na huyo mtoto wako amekuletea mwanamke aliye kama wewe nikimaanisha mnafanana tabia na mambo mengine na kukwambia 'mama, nataka kumuoa huyu mwanamke..' utamkubalia kwa moyo mweupe kabisa amuoe??

Jitizame tabia yako, mambo unayofanya, attitude yako juu ya wazazi na ndugu wa huyo mwanaume wako...je ni aina ya mwanamke ambae ungekubali mwanao amuoe?. Baada ya kujijibu hilo swali. Jijibu na hili:

Kwanini akuoe wewe?..na tatizo unafikiri mwanaume wako haoni attitude mbaya au nzuri uliyonayo..anaiona sana sema amebaki kimya kwa vile anajua utambishia kama utakavyoipinga hii makala yangu...hivyo amekuacha tu huku akiangalia mwanamke mwingine wa ku-propose!

Pia ni nini mtizamo wako wa kimaisha? Dada yangu kila mwanamke anao uwezo wa kuweka foundation na make ups usoni, kila mwanamke anao uwezo wa kuweka nywele, kila mwanamke anao uwezo wa kuongeza hips ma makalio yake.

Kila mwanamke endapo atafundishwa anao uwezo wa kumpagawisha mwanaume kitandani mpaka aka-vibrate kama Nokia tochi ya zamani.

Lakini unajua nini? Yote hayo yananunulika na pesa tu! Mwanaume anao uwezo wa kumlipia mwanamke na akayapata yote hayo bila ya kelele na stress za kila siku!

Hivyo basi, kwanini akuoe wewe?

Anatafuta mwanamke mwenye attitude na mtizamo bora. Tabia na siha njema hazifundishwi wala kununuliwa...mwanaume bora anatafuta mwanamke mwenye attitude nzuri..hayo mengine yananunulika na kufundishika.

Jambo bora kabisa kwako ni kuwa mwanamke wa msimamo mwenye siha na tabia njema. Muache akupende na akuoe kwa hilo tu.

Acha kuhangaika na kupigania mwanaume kukuoa. Kuwa wewe kama wewe. Nimegundua wanawake wengi wanaotamani ndoa wako vizuri kitabia sasa kutokana na pressure za marafiki, hofu ya umri na msukumo wa jamii kiujumla wanalazimisha ndoa kwa kufanya vitu ambavyo baadae vinawagharimu!

Kuwa mwanamke ambae ataona ni vigumu kwake bila wewe....usimpe mambo ambayo mwanamke mwingine yeyote anaweza kumpa.

Kama atakupenda wewe kama ulivyo na sio kwa sababu ya nywele za brazil au the way unavovaa basi hawezi kupenda kwingine.

Na hapo atakuwa na kila sababu ya kukuoa wewe. Na kama asipokuoa huyo mwanaume akapimwe akili huenda uvulana bado upo kichwani mwake!

My sister be real...and go get your man!!

By henry
Huoo ndo ukweli halisi be carefully madadaz
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom