Kwenu Viongozi wa Umoja Party

Unazungumzia kitu ambacho huna uelewa wa ndani. Uchumi wa China umeshikiliwa na mataifa ya Magharibi. Tafuta kwenye orodha ya makampuni makubwa kabisa 10 ya nchini China, niambie ni mangapi yanamilikiwa na wachina/China. Unaelewa kilichofanyika nchini China miaka 2000 kilichosababisha China yenye uchumi hohe hahe mpaka kufikia ukuaji wa 12% kwa mwaka?

Hivi unajua kuwa katika real development (human development), China ni nchi ya 89, ikizidiwa na nchi kama Botswana? Usione wachina wanazurura Duniani kote, ukadhani wanapenda. Hali zao za kimaisha na duni sana, japo Serikali ina pesa nyingi.

Huko Urusi kuna makampuni zaidi ya 1000 ya nchi za Magharibi. Unafuu wa uchumi wa Urusi, ulikuja baada ya kuachana na Leninism, na kuruhusu uwekezaji wa nje na uchumi huria lakini bado kuna pengo kubwa sana la maendeleo ukilinganisha na nchi kama US, UK, Belgium, Germany, Japan, Italy, Norway, n.k.

Hakuna nchi hata moja ya kidikteta ambayo wananchi wana maendeleo halisi. Urusi ni nchi ya 52 kwenye human development.
Kutokana na kufundishwa uzalendo wa kweli na wakawa wamefaulu kweli kweli ndio maana huwezi kumpata mchina ameiibia nchi pesa na Kwenda kuziweka nchi za ng'ambo !! Ukiiba pesa za Umma wanakunyonga! Ukijihusisha na madawa ya kulevya wanakunyonga ! Investment ya kutoka nchi za nje haikatazwi mradi ufuate sheria za nchi !!
 
Magufuli hakuamini uhuni wa vyama vya upinzani lakini watu makini waliokuwa upinzani aliwateua katika nyazifa mbalimbali
Aliwateua baada ya kuhamia CCM, Kikwete kidogo ndio alimteua Mbatia kuwa mbunge japo alikuwa upinzani

Kwa Magufuli Upinzani ilikuwa ni sawa na ushetani
 
Unazungumzia kitu ambacho huna uelewa wa ndani. Uchumi wa China umeshikiliwa na mataifa ya Magharibi. Tafuta kwenye orodha ya makampuni makubwa kabisa 10 ya nchini China, niambie ni mangapi yanamilikiwa na wachina/China. Unaelewa kilichofanyika nchini China miaka 2000 kilichosababisha China yenye uchumi hohe hahe mpaka kufikia ukuaji wa 12% kwa mwaka?

Hivi unajua kuwa katika real development (human development), China ni nchi ya 89, ikizidiwa na nchi kama Botswana? Usione wachina wanazurura Duniani kote, ukadhani wanapenda. Hali zao za kimaisha na duni sana, japo Serikali ina pesa nyingi.

Huko Urusi kuna makampuni zaidi ya 1000 ya nchi za Magharibi. Unafuu wa uchumi wa Urusi, ulikuja baada ya kuachana na Leninism, na kuruhusu uwekezaji wa nje na uchumi huria lakini bado kuna pengo kubwa sana la maendeleo ukilinganisha na nchi kama US, UK, Belgium, Germany, Japan, Italy, Norway, n.k.

Hakuna nchi hata moja ya kidikteta ambayo wananchi wana maendeleo halisi. Urusi ni nchi ya 52 kwenye human development.
Asante kwa taarifa mkuu
 
Pokeeni pongezi zangu za dhati kwanza kwa kuwaza na kuamua kutengeneza chama chenye mlengo na falsafa anuia za Hayati na Kipenzi chetu Dr. Magufuli. Hakika mmefanya jambo kubwa nala kutukuka sana.

Pamoja na pongezi zangu nyingi napenda kuwatahadharisha na kuwaasa kuwa makini sana kwa kila hatua mnayoiendea kwa maana dhamana na imani ya watanzania inakwenda kuwekwa juu yenu. Ni ombi langu kwenu kuwa na dhamiri ile ile ya upendo kwa Tanzania na watu wake huku mkijibidiisha kwa kila namna kuhakikisha Tanzania inapata viongozi wenye kiu na dhamira ya kweli kufikia maono makubwa ya kipenzi chetu Magufuli.

Ni vizuri kufahamu ya kuwa Tanzania ya sasa haina upungufu wa vyama vya siasa au sera nzuri za uendeshaji wa nchi. Hivyo ni budi kwenu kuyasoma na kuyapatia ufumbuzi yote ambayo ni maidhafu ya vyama vya siasa vilivyopo sasa ambavyo vimeshindwa kuonesha dira ya kweli ya Taifa letu kwa miaka 50 hadi 100 ijayo. Magufuli aliipenda Tanzania na kuchukizwa kabisa kwa maneno na vitendo na hali mbaya ya umaskini, ufisadi na dharau ya watawala/mabwenyenye waliojimilikisha nchi dhidi ya tabaka kubwa la watanzania wanyonge.

Ni ombi langu kwenu kutanguliza uzalendo na elimu ya kisiasa kwa watanzania wote wapate kufahamu dira, muelekeo na falsafa za chama. Katika hatua hizi za mwanzo ni muhimu sana kuhakikisha mnatengeneza misingi imara ya kitaasisi kwanza kwa kuhubiri na tena kuonesha kwa vitendo ili watanzania wayaamini hayo mnayapeleka kwao. Pasiwepo na hila midomoni mwenu tena Amani, Upendo,Haki na Mshikamano visipungue katika majukwaa yenu. Njoo na majibu ya namna ambavyo Tanzania itaweza kuendelea kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni muhimu sana kuzisema changamoto zote na kuueleza uma watanzania ni kwa njia gani tutafikia maendeleo ya kweli. Watafuteni wazee wazalendo wawapatie hekima zao, wapongezeni wanaostahili pongezi, wakemeeni wanastahili makaripio.

Karibuni kwenye ulingo wa siasa za Tanzania, karibuni kwenye figisu za CCM, karibuni kwenye hila za CHADEMA, karibuni kwenye kichaka cha wahuni na watakatishaji wa udhalimu.

Umoja ni nguvu, Umoja ni Ushindi, Umoja ni Maendeleo.
You sound like the current broken party. You have to sound like a revolutionalist not a puppet.
Keep the energy high not low.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Kiuhalisia hayati Magufuli alikua ni kiongozi jasiri na shupavu kweli, lakini hakua na sifa za kuwa Rais.Nafasi ya juu kimamlaka kwa mtu kama yule ilikua ni uwaziri mkuu tu.Yaani juu yake inapaswa kuwa na mtu aliepevuka kwa hekima na maono ya kuvumilia kupishana maono na watu na kukubali kushaurika.

Lakini kiongozi aina ya Magufuli ni mtu mwenye kutumia maguvu mengi hata mahala pasipohitaji maguvu, mwisho wa siku mnaibomoa nchi badala ya kuijenga.Mungu amlaze pema huko alipo maana ametuachia somo kama taifa!!!
Strategy ya hekima imetumika sana lakini discipline makazini bado ikawa chini. Mpaka utumie fujo ndo discipline inarudi

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Wenzako hawawalengi wananchi wenye uelewa,la hasha wanawalenga walalahoi,wanyonge na hohehahe

Wanawalenga watu ambao hawajui kuhoji yanayoendea Tanzania

Wanawalenga watu ambao wana chuki na watumishi wa umma,matajiri na wenye nacho

Hivyo nina uhakika watapata wajinga wengi

Watawapata wanyonge wengi wa Magufuli
Nimekuelewa. Kuwa watawapata wengi wanyonge wa akili? Kitakuwa ni chama cha wajinga.
 
You sound like the current broken party. You have to sound like a revolutionalist not a puppet.
Keep the energy high not low.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Mambo ya unaharakati waachie Chadema, UP ipo kwa ajili ya kushika dola maneno na vitendo lazima yaendane na dhana ya uwajibikaji.
 
Urusi haipo kwenye nchi
Unazungumzia kitu ambacho huna uelewa wa ndani. Uchumi wa China umeshikiliwa na mataifa ya Magharibi. Tafuta kwenye orodha ya makampuni makubwa kabisa 10 ya nchini China, niambie ni mangapi yanamilikiwa na wachina/China. Unaelewa kilichofanyika nchini China miaka 2000 kilichosababisha China yenye uchumi hohe hahe mpaka kufikia ukuaji wa 12% kwa mwaka?

Hivi unajua kuwa katika real development (human development), China ni nchi ya 89, ikizidiwa na nchi kama Botswana? Usione wachina wanazurura Duniani kote, ukadhani wanapenda. Hali zao za kimaisha na duni sana, japo Serikali ina pesa nyingi.

Huko Urusi kuna makampuni zaidi ya 1000 ya nchi za Magharibi. Unafuu wa uchumi wa Urusi, ulikuja baada ya kuachana na Leninism, na kuruhusu uwekezaji wa nje na uchumi huria lakini bado kuna pengo kubwa sana la maendeleo ukilinganisha na nchi kama US, UK, Belgium, Germany, Japan, Italy, Ç, n.k.

Hakuna nchi hata moja ya kidikteta ambayo wananchi wana maendeleo halisi. Urusi ni nchi ya 52 kwenye human developmen

Watanzania wote wanajua Magufuli alikua CCM lakini hakujinasibisha na CCM. Mlengo wake siku zote ulikua Tanzania kwanza amefanya juhudi nyingi kupitia CCM lakini hakufanikiwa kwa sababu CCM has been broken beyond repair.
Binafsi ninaona CCM kupitia kwa muasisi wake Baba wa taifa Mwl. Nyerere imefanya kazi kubwa naya kutukuka ya kusimika mizizi ya taifa na kutengeneza misingi imara ya umoja na Mshikamano.
Kwa sasa mahitaji ya taifa ni tofauti kabisa na yale ya kipindi cha ukombozi hivyo yanahitaji fikra tofauti kuvuka kwenye mkwamo uliopo Sasa.
Magufuli alitengeneza blue print na sisi kama wana UP tunakwenda kiiteleza. Jambo hili litapingwa sana na wote wanaofurahia/kunufaika na hali mbaya umaskini uliopo nchi, wala rushwa, wahujumu uchumi, wapiga madili na wenye vyeti feki, wabadhirifu na wahuni wote.
Lakini yeyote mwenye nia njema hakika hawezi acha kuunga mkono harakati za UP.

Umoja ni Nguvu, Umoja ni Upendo, Umoja ni Maendeleo.
Nawapongeza sana kwa kutumia haki za kikatiba kuanzisha hicho chama,ila angalieni ni flagship ipi mnaitumia Kuiingia mioyo ya wananchi,sababu ulizitoa hapo za kwamba JPM alipigania haki za watanzania huku hajajifungamanisha sana na CCM,hiyo ni sababu ya kisomi,Nina maana ni watu waliosoma kama wewe ndiyo wanaweza kutanabahisha hivyo,lakini kwa wale watanzania wakawaida ambao ndiyo wengi hawana uwezo wa kutenganisha kati ya CCM na JPM,nawatakia mafanikio mema katika kuanzisha chama ambacho kinaeeza kurudisha matumaini ya watanzania yaliyopptea.
 
Mungu amevichagua vinyonge na vidhaifu vya dunia hii ili adhihirishe ukuu wake.
Ujinga siyo sehemu ya utakatifu. Mungu hujivunia watu wake walio werevu na wakweli wa nafsi zao.
 
Watanzania wengi ni mazuzu. Eti wana imani na Umoja Party chama kilichoanzishwa na mwanachama wa chama cha AAAFP, na mgombea urais Zanzibar Bwana Seif Maalim Seif (jina linaendana na la hayati Maalim Seif S. Hamad).

Aisee au basi!
 
Samia toka lini akamuenzi Jiwe? Hukusikia akiwa marekani alivyosema kuwa walikuwa hawaelewani?
Pia aliwahi kusema kuwa Yeye na marehemu ni kitu kimoja. Kuna mengine bado anayaenzi. Aliuenzi ubambikiaji kesi, akampeleka Mbowe gerezani.

Anamuenzi marehemu kwa kutoruhusu vyama vya siasa kufanya mikutano.
 
Ujinga siyo sehemu ya utakatifu. Mungu hujivunia watu wake walio werevu na wakweli wa nafsi zao.
Habari za ujinga wako usizilete hapa. Mimi nimezungumza namna Mungu hutumia vitu dhaifu vya duniani.
1 Wakorintho 1:27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;
Hili jawabu langu la mwisho kwako sipendi kujinasibisha na wapumbavu
 
Urusi haipo kwenye nchi



Nawapongeza sana kwa kutumia haki za kikatiba kuanzisha hicho chama,ila angalieni ni flagship ipi mnaitumia Kuiingia mioyo ya wananchi,sababu ulizitoa hapo za kwamba JPM alipigania haki za watanzania huku hajajifungamanisha sana na CCM,hiyo ni sababu ya kisomi,Nina maana ni watu waliosoma kama wewe ndiyo wanaweza kutanabahisha hivyo,lakini kwa wale watanzania wakawaida ambao ndiyo wengi hawana uwezo wa kutenganisha kati ya CCM na JPM,nawatakia mafanikio mema katika kuanzisha chama ambacho kinaeeza kurudisha matumaini ya watanzania yaliyopptea.
Angalizo zuri naimani viongozi watalifanyia kazi. Tuwaombee kheri michakato ya usajili ikamilike salama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom