Kwenda kwa mumeo na vitu vyote au kwenda na begi?

ofkozi,ikiwezekana wape,,,,,,wenyewe watajipanga watanunua tu kiwanja watajenga,,,,,,,

Ndo maanake kama huna nyumba wawezeshe basi angalau uwanunulie kiwanja na tofauli mpaka kupaua wasaidie ili maisha yasonge
 
mimi nisie na hata na kijiko na mama yangu yupo hoi kitandani .. nitapata mtu kweli maana naona wakaka hapa ??????????????
 
mmmh wanaume wa sasa hivi kumbe ndo maana sipati mpenzi ..ngoja nianze kusema nina nyumba namalizia mbezi beach

ukipiga sana fiksi utaishia kupata wanaume wa kukumega na kuchapa mwendo wakikuacha unanung'unika
mwanamke wa kuolewa anajulikana tu kama ilivyo kwa mwanaume muoaji anajulikana pia
 
Smile hakuna ubaya kwenda na vitu ulivyokuwa navyo kwenye maisha ya ndoa tatizo linakuja pale kutakapokuwa na ugomvi kati yenu na kuanza manyanyaso kwa mumeo
 
Last edited by a moderator:
mimi nisie na hata na kijiko na mama yangu yupo hoi kitandani .. nitapata mtu kweli maana naona wakaka hapa ??????????????

kwa uzoefu wako hebu tuambie,ni wasichana wangapi ambao wameenda kwa waume zao na kila kitu,na ni wasichana wangapi ambao wameenda kwa waume zao na mabegi au MALI ZAO ZISIZOHAMISHIKA?????
hadi wewe unapata shaka kuwa hutaolewa eti kwakua HUNA KIJIKO?????huyo jamaa wakat anamtongoza binti sidhan kama aliyajua hayo yote,,,,,,,,
 
aya maaaa..i wish ungekuwa mamamkwe wangu

ona ungekuwa na bahati jamani, manake ungekuwa daughter wangu kipenzi. Na mumeo akileta za kuleta tnamnyooshaje?
Ila wewe ukileta za kuleta nakupotezea adili na wewe kivyake.
maisha marahisi mama, ni unavyojiweka tu. mwanaume anaejiamini hawezi kuwa na tatizo kuwa umekuja na vitu manake nae anajitahidi kuwa navyo. Lazy men ndo wabaya, ila hata akiwa maskini as long as he is hardworking, mbona mtatoka tu siku isiyo na jina?
Ngoja nikizalie mchumba basi, usizeeke basi.
 
Kumpa nyumba mkweo ya kuishi na bintiyo ni ishara ya ukomavu wa makuzi na malezi ukiwa mzazi

Huko ni kumfuga. Mwanaume anatakiwa ajenge nyumba na mkewe, sio ya kupewa. Mie na Paw wangu hata tupewe nyumba masaki na mzee Mtambuzi staki ng'oo, tutapanga mbagala, tukizichanga tuhamie sinza afu tujenge mbezi. Ila nikipewa nyumba ya kazini hapo tutaenda kuishi na l'aziz wangu kipenzi. Nitahakikisha namsaidia mume wangu na kum-push tufikie level niliyozoea na sio kwa kubebwa. Aibu gani, hata apewe na mamake nyumba staki hadi mamake afe ndo tuirithi. Aweke mpangaji ale penshion yake!
 
Dah! ulimwengu umebadilika sana na mambo yanaenda kutoka stage moja kwenda nyingine ni kama vile kutoka homo sapians to homo erectus etc... na kuendelea...
Kwa mtazamo wangu tangu nimeanza kupata ufahamu kwenye akili yangu zamani ili mwanaume aoe au apewe mke alikuwa anatakiwa awe na uwezo wa kulisha familia yaani mke na watoto watakao zaliwa. Awe na mahali pa kuishi either amejenga au amepanga ila sio nyumba ya familia au wanayokaa wazazi wa mume. Pia mume huyo alitakiwa awe na vitu kadhaa vya ndani ya nyumba ambavyo ni godoro, kitanda, angalau stuli au kigoda kwa wageni na mwanamke ili aweze kuolewa alikuwa anaangaliwa kwanza anauwezo wa kuzaa?, kulea watoto?, anajua kupika kwa njia zote yaani kuni, mkaa, jiko la mchina, anajua kufua, kuhudumia wagonjwa na usafi kwa ujumla. Na suala la mwanamke kuwa na kitu au kwenda na kitu kwa mume halikuwepo. Mtaji wa mwanamke kwenye ndoa ilikuwa ni uchapa kazi, usafi, kulea familia n.k. na mwanaume mtaji wake kwenye ndoa ilikuwa ni ujasiri, mtafutaji wa chakula na vitu vya familia.
Matatizo yanayotokea kwenye ndoa mengine yanafikia wenye ndoa kuachana na hapo kwenye kuachana baada ya miaka kadhaa ya kuishi kwenye ndoa ndipo ikaonekana mwanamke anafukuzwa na kirago cha nguo zake tu kama alivokuja wakati anaolewa. Hii imeipa shida jamii na kuifanya jamii ijihami au itengeneza njia za kumnusuru mwanamke ili ikitokea wanaachana au anafukuzwa basi mwanamke huyo awe na kitu cha kutoka nacho kwenye ndoa na si kufukuzwa na kirago cha nguo. Isingekuwa shida na matatizo yaliyowahi kutokea kwenye ndoa ambazo nimeshuhidia au wewe umezisikia basi hadi leo mwanamke angekuwa anatoka kwao na nguo tuu na khanga kibao na jukumu la nyumba na vitu vyake na kula likabaki kwa mwanaume. Ila kwa sababu ya matatizo hayo hata pale mume anapofariki ndugu wa mume kumnyanyasa mwanamke na kumfukuza mwanamke na nguo zake tuu wakati mali walizochuma mwamamke aliwekeza nguvu zake za uchapakazi, usafi, kulea n.k
Mabadiliko haya ndo yameleta leo wamama au wazazi kwa ujumla kuwafungasha mabinti zao wanapoenda kwa waume zao na vitu vyote vya ndani japo hapa uwezo unazingatiwa. Kwasababu wale ambao wanatoka kwenye familia duni bado wanaenda kwa waume zao na nguo tuu. Tatizo ni pale binti anapojishebedua kabla hata hajateswa na mume au ndugu wa mume, utasikia, ''eeeh usinibabaishe kama umenichoka naita fuso sasa hivi na ninasepa na kilakitu changu cha kichen party''. Hapo mwanaume akisikia hivi na akiangalia nyumba ibaki wazi anaona bora soo liishe na binti hapa anakuwa anakosea kwani unamfanya mwanaume kuwa mdogo na kutojiamini.
Ni vizuri kuwafungasha mabinti na vyombo vya ndani kwani jiko linaaminika ni sehemu ya mama na si baba ndo maana wanaume wachache sana hata waliojenga wanakuwa na vyombo vingi vya ndani. Utakuta hata kama anajipikia atakuwa na sahani moja au kikombe kimoja na sufuria moja. Kumpa binti sofa, dining table, coffe table, makabati ya ndani, godoro vitanda n.k vya ndani ili kuwasaidia wanandoa hawa kujikwamua kimaisha na si kwenda kunyanyasana.
Nimeongea kwa kireeefu but hope nimeeleweka, wanaume msiwanyanyase wake zenu waliokuja na nguo tuu na kuwakuta nyie wanaume na kilakitu ndani. Na nyie mabinti mnaoolewa na mmefungashiwa kila kitu na wazazi wenu yaani mmejaza fuso kwenda kwa waume zenu msijishebedue kwa kujiona nyumba nzima umeijaza wewe.
ZINGATIA: mwanaume na ampende mke wake, mwanamke na amtii mume wake, for sure ukiweza kuitimiza hii rule in all ur marriage life hutapata shida. Kila mtu atimize wajibu wake na kufanya yanayompasa. Play ur part in ur marriage and enjoy....!
Ni mtazamo wangu tuu.
Ever remaining,
Sakapal.
 
Kwa maisha ya sasa yasivotabirika especially kiuchumi mi naona kama haikuwa muimu kusomba hayo mavitu kuwapa na watu wanaenda kuishi nyumba ya kupanga.ngemuona uyo mama ana busara kama angempa hizo fedha binti yake na kumshauri azifanyie biashara ili ziwasaidie katika ujenzi na maendeleo kwa ujumla.kitu cha muimu kuingia nacho kwenye ndoa ni kazi/biashara yako,hayo mengine matokeo.

Labda mama alifanya ivo kuepusha wale wanaoleta vitu vibaya kwenye zawadi,mfano mtu anaweka lichupi la period ndani yaboksi la zawadi,au makonokono etc.
 
Smile hakuna ubaya kwenda na vitu ulivyokuwa navyo kwenye maisha ya ndoa tatizo linakuja pale kutakapokuwa na ugomvi kati yenu na kuanza manyanyaso kwa mumeo
mi nauliza ni sawa kwenda na kila kitu ? yaani kila kitu ndani kinakuwa ni chako ni sawa?
 
Kabla ya kujibu hili swali, kitu cha kujiuliza ni 'kwa nini unaolewa'?
Ukipata jibu hapa, ndilo litakuwa vission ya ndoa yako

Haya mengine makelele tu.

Kama vission ya ndoa kwako ni mume kukutunza kwa kila kitu, basi usiende hata na nduo maana atakununulia zingine.

Kama vission yako ni kutafuta mwenza wa kufurahi pamoja na kuijaza dunia wakati unasubiri kuingia makao yako ya milele, nenda hata na Ubungo Plaza zako 5 achia mbali masufuria.

Ni sawa kwenda na vyombo au si sawa kutegemea na dira ya ndoa yenu.
 
Dah! ulimwengu umebadilika sana na mambo yanaenda kutoka stage moja kwenda nyingine ni kama vile kutoka homo sapians to homo erectus etc... na kuendelea...
Kwa mtazamo wangu tangu nimeanza kupata ufahamu kwenye akili yangu zamani ili mwanaume aoe au apewe mke alikuwa anatakiwa awe na uwezo wa kulisha familia yaani mke na watoto watakao zaliwa. Awe na mahali pa kuishi either amejenga au amepanga ila sio nyumba ya familia au wanayokaa wazazi wa mume. Pia mume huyo alitakiwa awe na vitu kadhaa vya ndani ya nyumba ambavyo ni godoro, kitanda, angalau stuli au kigoda kwa wageni na mwanamke ili aweze kuolewa alikuwa anaangaliwa kwanza anauwezo wa kuzaa?, kulea watoto?, anajua kupika kwa njia zote yaani kuni, mkaa, jiko la mchina, anajua kufua, kuhudumia wagonjwa na usafi kwa ujumla. Na suala la mwanamke kuwa na kitu au kwenda na kitu kwa mume halikuwepo. Mtaji wa mwanamke kwenye ndoa ilikuwa ni uchapa kazi, usafi, kulea familia n.k. na mwanaume mtaji wake kwenye ndoa ilikuwa ni ujasiri, mtafutaji wa chakula na vitu vya familia.
Matatizo yanayotokea kwenye ndoa mengine yanafikia wenye ndoa kuachana na hapo kwenye kuachana baada ya miaka kadhaa ya kuishi kwenye ndoa ndipo ikaonekana mwanamke anafukuzwa na kirago cha nguo zake tu kama alivokuja wakati anaolewa. Hii imeipa shida jamii na kuifanya jamii ijihami au itengeneza njia za kumnusuru mwanamke ili ikitokea wanaachana au anafukuzwa basi mwanamke huyo awe na kitu cha kutoka nacho kwenye ndoa na si kufukuzwa na kirago cha nguo. Isingekuwa shida na matatizo yaliyowahi kutokea kwenye ndoa ambazo nimeshuhidia au wewe umezisikia basi hadi leo mwanamke angekuwa anatoka kwao na nguo tuu na khanga kibao na jukumu la nyumba na vitu vyake na kula likabaki kwa mwanaume. Ila kwa sababu ya matatizo hayo hata pale mume anapofariki ndugu wa mume kumnyanyasa mwanamke na kumfukuza mwanamke na nguo zake tuu wakati mali walizochuma mwamamke aliwekeza nguvu zake za uchapakazi, usafi, kulea n.k
Mabadiliko haya ndo yameleta leo wamama au wazazi kwa ujumla kuwafungasha mabinti zao wanapoenda kwa waume zao na vitu vyote vya ndani japo hapa uwezo unazingatiwa. Kwasababu wale ambao wanatoka kwenye familia duni bado wanaenda kwa waume zao na nguo tuu. Tatizo ni pale binti anapojishebedua kabla hata hajateswa na mume au ndugu wa mume, utasikia, ''eeeh usinibabaishe kama umenichoka naita fuso sasa hivi na ninasepa na kilakitu changu cha kichen party''. Hapo mwanaume akisikia hivi na akiangalia nyumba ibaki wazi anaona bora soo liishe na binti hapa anakuwa anakosea kwani unamfanya mwanaume kuwa mdogo na kutojiamini.
Ni vizuri kuwafungasha mabinti na vyombo vya ndani kwani jiko linaaminika ni sehemu ya mama na si baba ndo maana wanaume wachache sana hata waliojenga wanakuwa na vyombo vingi vya ndani. Utakuta hata kama anajipikia atakuwa na sahani moja au kikombe kimoja na sufuria moja. Kumpa binti sofa, dining table, coffe table, makabati ya ndani, godoro vitanda n.k vya ndani ili kuwasaidia wanandoa hawa kujikwamua kimaisha na si kwenda kunyanyasana.
Nimeongea kwa kireeefu but hope nimeeleweka, wanaume msiwanyanyase wake zenu waliokuja na nguo tuu na kuwakuta nyie wanaume na kilakitu ndani. Na nyie mabinti mnaoolewa na mmefungashiwa kila kitu na wazazi wenu yaani mmejaza fuso kwenda kwa waume zenu msijishebedue kwa kujiona nyumba nzima umeijaza wewe.
ZINGATIA: mwanaume na ampende mke wake, mwanamke na amtii mume wake, for sure ukiweza kuitimiza hii rule in all ur marriage life hutapata shida. Kila mtu atimize wajibu wake na kufanya yanayompasa. Play ur part in ur marriage and enjoy....!
Ni mtazamo wangu tuu.
Ever remaining,
Sakapal.
thax mdau@Sakapal but sio lazima kumpa vitu vyote eti au unasemaje?
 
Kabla ya kujibu hili swali, kitu cha kujiuliza ni 'kwa nini unaolewa'?
Ukipata jibu hapa, ndilo litakuwa vission ya ndoa yako

Haya mengine makelele tu.

Kama vission ya ndoa kwako ni mume kukutunza kwa kila kitu, basi usiende hata na nduo maana atakununulia zingine.

Kama vission yako ni kutafuta mwenza wa kufurahi pamoja na kuijaza dunia wakati unasubiri kuingia makao yako ya milele, nenda hata na Ubungo Plaza zako 5 achia mbali masufuria.

Ni sawa kwenda na vyombo au si sawa kutegemea na dira ya ndoa yenu.
aisee! hata wewe mamamdogo?
 
mi nauliza ni sawa kwenda na kila kitu ? yaani kila kitu ndani kinakuwa ni chako ni sawa?

vitu vyote ulivyopewa kama zawadi kuanzia kwenye kichen party, send off hadi harusi ni vyenu wooote mume na mke. Nisawa kumfungasha binti yako kwenda na kila kitu kwa mume wake ila, umkalishe huyo binti afahamu na atimize wajibu wake kama mke na si kwenda kujihami na kujishebedua na kuonyesha utajiri kwa mume wake. Hapa uwezo unaangaliwa kama huna uwezo huhitaji kukopa ili tu umfungashe binti yako na kila kitu, mpe kile unauwezo nacho cha muhimu amtii mumewe na kuijenga nyumba yake na aende kuibomoa kwa kujihami na zawadi alizojaza kwenye fuso.
hapo kwenye bold na underline si sawa, vitu vinakuwa vyenu wooote.
kwani mnakuwa mwili mmoja...
 
Kwa maisha ya sasa yasivotabirika especially kiuchumi mi naona kama haikuwa muimu kusomba hayo mavitu kuwapa na watu wanaenda kuishi nyumba ya kupanga.ngemuona uyo mama ana busara kama angempa hizo fedha binti yake na kumshauri azifanyie biashara ili ziwasaidie katika ujenzi na maendeleo kwa ujumla.kitu cha muimu kuingia nacho kwenye ndoa ni kazi/biashara yako,hayo mengine matokeo.

Labda mama alifanya ivo kuepusha wale wanaoleta vitu vibaya kwenye zawadi,mfano mtu anaweka lichupi la period ndani yaboksi la zawadi,au makonokono etc.
kweli angempa hata hela za biashara
 
thax mdau@Sakapal but sio lazima kumpa vitu vyote eti au unasemaje?

sio lazima ila kama unauwezo utatamani kumpa kila kitu hata wafanyakazi utatamani kumuwekea na mshahara ulipe wewe, ila je? jiulize utakuwa unamjengea binti yako huyo akili gani? ataweza kuchakarika in life na kutafuta in her own? au atakuwa ansema tu aah nikiishiwa mama atanipa na binti huyu utakuta hata kupika maandazi au chapati hajui.
Kama umemlea binti yako kisaikolojia na kimaadili vizuri na unauwezo mfungashie tuu kila kitu anachohitaji, ila kama huna uwezo usije ukakopa au ukaiba, uwezo wako ukoje? na huyu binti unataka akaishije kwa mume wake? anyenyekewe na mume na ndugu wote wa mume au...? reason behind ya kumfungashia mazagazaga yote haya ni nini?
 
Sio vibaya kukuta kila kitu pia,
sasa kama mwanamme anavyo avitupe??

Yote inategemea kwa nini mwaoana.

kongosho,sa ukute mwanaume ana mpaka chujio la nazi kweli?mimi sitakuwa comfortable,ningependa zaidi hivo vitu nivinunue mimi kwa kweli!
 
Back
Top Bottom