Maramla
JF-Expert Member
- Jan 8, 2014
- 581
- 642
Na Nathaniel Ndilito, DSM.
Nimesoma andiko linalodaiwa kuandikwa na Zitto Kabwe akihoji kama Rais Magufuli amemtumbua Kangi Lugora kwa kusaini Mkataba ambao "haujapita Bungeni," mbona kuna mikataba mingi "haijapota Bungeni" na watu hawajachukuliwa hatua?
Kama kawaida yake Zitto akataja mifano ya yale yale makubwa ya JPM yanayomuumiza kichwa; SGR, ununuzi wa ndege na mengineyo. Anataka tuamini nayo "hayakupitia Bungeni."
Nianze kwa kusema Zitto ameshajenga dhana ya kupinga kila kinachofanywa na Serikali. Hivyo ni kazi yake kupinga lakini asitufanye sisi raia ni wajinga. Tunaielewa dhamira ya Rais na tunafuatilia.
Kiufupi katika hili Zitto hakumsikiliza wala hakutaka kumwelewa JPM. Ametoka kuwa mjenga hoja hadi pingapinga tu. Sasa asome hapa:
Mosi, Kwa nini naamini hakumsikiliza Rais kuhusu issue ya Kangi Lugola. Rais amelaumu mambo 2 kuingiwa mkataba wa mkopo ambao kwa mujibu wa Sheria ya Bunge ya Madeni na Misaada, mkataba huo ulitakiwa ushughulikiwe na Kamati ya Madeni iliyopo Wizara ya Fedha. Kosa la kwanza na Rais alitaja wazi. Zitto anafanya propaganda kwenye facts!
Pili, Rais akazungumzia kosa la "Hata Bungeni" mkopo huo haukupelekwa. Zitto tena hakutaka kusikiliza.
Muktadha wa Rais hapa kwa Sheria ya Bajeti ni kuwa mkopo unapokuwa umepitia hatua zote za Wizara ya fedha (sio kupelekwa mkataba) bali Bunge linahusika kwa maana ya kupitisha mkopo huo kama chanzo rasmi cha mapato katika Bajeti ya wizara na taasisi husika.
Kama ni mradi utaelezwa kuwa utaketewa USD au Euro kadhaa, source inatajwa. Huu ni mfumo wa kawaida wa Bajeti ambao Rais ndio anahoji chanzo cha kina Lugola mbona hakimo hata ktk vilivyoidhinishwa na Bunge? Kosa nini hapo?
Zitto yuko nyuma ya wakati sana, Serikali ya Tanzania ilishaachana na ubabaishaji huu wa kila Wizara au Tasisi kukopa kivyake kwanza inaweza kuleta shida kwenye uchumi maana mikopo hata ya sekta binafsi na taasisi za umma inasomeka kwenye uwiano wa deni la Taifa.
Sasa cha ajabu Zitto huyu huyu anayelalamikaga deni la Taifa linakua na kutaka udhibiti, leo hapa anadhihirisha unafiki wake kwa kumtetea Lugola kuwa kaonewa? Alitaka mkopo ukopwe hivyo kihohela halafu aje apate kete ya kisiasa kuwa deni la Taifa liongezeke aibuke kuponda!!! Kweli Magu Chuma. Watu wanakosa hoja hadi sasa wanakula ubuyu tu
Nimegundua Zitto anapitia wakati mgumu katika utawala huu, hakuna pa kufanya unafiki, kila mahali watu wanasimamia principles. Anataabika.
Lakini licha ya kutomwelewa Rais, pia bado hajaelewa hata muktadha wa hoja. Suala la kina Lugola linahusu mkopo.
Zitto anatoa mfano wa SGR kuwa nayo "haikupita Bungeni," wapi na wapi kwani SGR kuna mtu kakopa? Kakopa wapi? Au ndege? Zimekopwa wapi???Ili hata kama mkataba wake ungetakiwa kupita Bungeni tuseme haukupita???
Ununuzi wa ndege na bajeti za SGR zinapitishwa Bungeni kupitia vifungu vya Bajeti za kila mwaka, Zitto haoni hapo?Au yeye anajua kukataa tu Bajeti hasomi ndani!
Lakini pia Akasome the Government Loans Guarantees and Grants Act (as ammended) na kisha akasome the Budget Act ataziona hoja mbili za Magufuli dhidi ya upuuzi wake.
Hapa ndio naamini yule Zitto mjenga hoja wa enzi za Buzwagi akikutana na huyu Zitto mjenga vihoja wa zama hizi, vita yake itakuwa sawa na vita ya III ya dunia.
Sent from my iPhone using JamiiForums
Nimesoma andiko linalodaiwa kuandikwa na Zitto Kabwe akihoji kama Rais Magufuli amemtumbua Kangi Lugora kwa kusaini Mkataba ambao "haujapita Bungeni," mbona kuna mikataba mingi "haijapota Bungeni" na watu hawajachukuliwa hatua?
Kama kawaida yake Zitto akataja mifano ya yale yale makubwa ya JPM yanayomuumiza kichwa; SGR, ununuzi wa ndege na mengineyo. Anataka tuamini nayo "hayakupitia Bungeni."
Nianze kwa kusema Zitto ameshajenga dhana ya kupinga kila kinachofanywa na Serikali. Hivyo ni kazi yake kupinga lakini asitufanye sisi raia ni wajinga. Tunaielewa dhamira ya Rais na tunafuatilia.
Kiufupi katika hili Zitto hakumsikiliza wala hakutaka kumwelewa JPM. Ametoka kuwa mjenga hoja hadi pingapinga tu. Sasa asome hapa:
Mosi, Kwa nini naamini hakumsikiliza Rais kuhusu issue ya Kangi Lugola. Rais amelaumu mambo 2 kuingiwa mkataba wa mkopo ambao kwa mujibu wa Sheria ya Bunge ya Madeni na Misaada, mkataba huo ulitakiwa ushughulikiwe na Kamati ya Madeni iliyopo Wizara ya Fedha. Kosa la kwanza na Rais alitaja wazi. Zitto anafanya propaganda kwenye facts!
Pili, Rais akazungumzia kosa la "Hata Bungeni" mkopo huo haukupelekwa. Zitto tena hakutaka kusikiliza.
Muktadha wa Rais hapa kwa Sheria ya Bajeti ni kuwa mkopo unapokuwa umepitia hatua zote za Wizara ya fedha (sio kupelekwa mkataba) bali Bunge linahusika kwa maana ya kupitisha mkopo huo kama chanzo rasmi cha mapato katika Bajeti ya wizara na taasisi husika.
Kama ni mradi utaelezwa kuwa utaketewa USD au Euro kadhaa, source inatajwa. Huu ni mfumo wa kawaida wa Bajeti ambao Rais ndio anahoji chanzo cha kina Lugola mbona hakimo hata ktk vilivyoidhinishwa na Bunge? Kosa nini hapo?
Zitto yuko nyuma ya wakati sana, Serikali ya Tanzania ilishaachana na ubabaishaji huu wa kila Wizara au Tasisi kukopa kivyake kwanza inaweza kuleta shida kwenye uchumi maana mikopo hata ya sekta binafsi na taasisi za umma inasomeka kwenye uwiano wa deni la Taifa.
Sasa cha ajabu Zitto huyu huyu anayelalamikaga deni la Taifa linakua na kutaka udhibiti, leo hapa anadhihirisha unafiki wake kwa kumtetea Lugola kuwa kaonewa? Alitaka mkopo ukopwe hivyo kihohela halafu aje apate kete ya kisiasa kuwa deni la Taifa liongezeke aibuke kuponda!!! Kweli Magu Chuma. Watu wanakosa hoja hadi sasa wanakula ubuyu tu
Nimegundua Zitto anapitia wakati mgumu katika utawala huu, hakuna pa kufanya unafiki, kila mahali watu wanasimamia principles. Anataabika.
Lakini licha ya kutomwelewa Rais, pia bado hajaelewa hata muktadha wa hoja. Suala la kina Lugola linahusu mkopo.
Zitto anatoa mfano wa SGR kuwa nayo "haikupita Bungeni," wapi na wapi kwani SGR kuna mtu kakopa? Kakopa wapi? Au ndege? Zimekopwa wapi???Ili hata kama mkataba wake ungetakiwa kupita Bungeni tuseme haukupita???
Ununuzi wa ndege na bajeti za SGR zinapitishwa Bungeni kupitia vifungu vya Bajeti za kila mwaka, Zitto haoni hapo?Au yeye anajua kukataa tu Bajeti hasomi ndani!
Lakini pia Akasome the Government Loans Guarantees and Grants Act (as ammended) na kisha akasome the Budget Act ataziona hoja mbili za Magufuli dhidi ya upuuzi wake.
Hapa ndio naamini yule Zitto mjenga hoja wa enzi za Buzwagi akikutana na huyu Zitto mjenga vihoja wa zama hizi, vita yake itakuwa sawa na vita ya III ya dunia.
Sent from my iPhone using JamiiForums