Kweli watu wema bado wapo

Chwekamu

JF-Expert Member
Nov 1, 2017
507
491
Tulihama Nachingwea mwaka 1986,I was so young by then.
Marehemu mama Yangu aliwahi nunua Shamba kubwa,But wakati tunahama kule mama Alimuachia Shamba rafiki yake mama Mbwana,
Na akamwambia,naondoka rafiki Yangu ila nakuachia Shamba langu,ila tumia na litunze wanangu wakiwa wakubwa Wape.Tena alimkabidhi bila Maandishi yeyote.

Ni zaidi ya miaka 31 Now,Na Tukiwa Atujuhi lolote juu ya ilo Shamba, huyu mama Amenitafuta kupitia mtandao Wa Kijamii Facebook,
Kiukweli alikuwa na uwezo Wa kukaa kimya na pia Kutudhurumu but Akufanya hivyo.

Jamani Huyu mama ni Mfano Wa Kuigwa.

Hongera sana Mama Mbwana na pia now naamini kweli ulikuwa rafiki bora Wa MAMA.

NDUGU ZANGU WANA JF WATU WEMA BADO WAPO.

JE UNA MKASA GAN AMBAO UNAFANANA NA HUU?
 
Baba mkubwa alifariki(ghafla na katka mazngra tata sana) dk za mwisho akiwa anafuatilia kiinua mgongo chake, wakuu wakawa wanataka waimalize juu kwa juu na vitisho kwa wanaoifuatilia, rafki mkubwa wa baba mkubwa kazini na nje ya kazi alipigana kimya kimya bila sisi kujua na huku familia ikiwa imeshakata matumaini siku ya siku anamuita mamkubwa na mshua watie sain baada ya siku nne account ya mamkubwa ikasoma 136M, alikataa kuchukua hata mia,

MARAFIKI WA KWELI WAPO. Na asikwambie mtu rafki wa kweli ni wa jinsia yako. MEN TO MEN, WOMEN TO WOMEN.
 
Nilikua nimekaa siku moja sina hili wa lile, basi kuna bi dada mmoja nilikua nimesahau ata kama niliwahi kumtongoza, hamadi napigiwa simu niende nikapewe papuchi, kweli wanawake wema bado wapo.
kweli huyo dada mtu mwema asee
 
Nilikua nimekaa siku moja sina hili wa lile, basi kuna bi dada mmoja nilikua nimesahau ata kama niliwahi kumtongoza, hamadi napigiwa simu niende nikapewe papuchi, kweli wanawake wema bado wapo.
Umetisha mkuu.
 
MIMI SINA MKASA ILA NAKUUNGA MKONO MKUU,WEMA WAPO TENA WENGI TUU
hata katili anajifunza either baada ya kufanyiwa ukatili au kushuhudia ukatili,watu kama hawa.watu wa media wangetengeneza vipindi reality shows za kuwatanabaisha watu hawa ili wengine wajifunze kupitia wao.
 
mie nilijifanyaga mwema baada ya kuokota simu kwenye daladala maeneo ya makumbusho miaka ya 2005 au 2006. Mwenye simu (mdada) akanipigia na kuniambia mume wake atakuja kuichukua ofisini kwangu posta DSM. Jamaa alipokuja nilipompa ile simu akaniuliza umefahamiana vp na mke? nikabaki nashangaa nikamuuliza kwani akukwambia kuwa nimeokota simu ile njemba ikaniambia achana na wake za watu utakuja kufa. Wema unaponza wakati mwingine
 
"... wema wangu umeniponza sasa machungu ya dunia nayaonja..."

Ameimba Ferouz sikumbuki kwenye wimbo gani
 
Mwaka 2010 Nilimfanyia kazi ya Mageti Jamaa mmoja Mkazi wa Mbeya sehemu moja inaitwa Sayi hakunilipa hela yote kwa sababu ambazo sikuwahi kuzijua kupindi kile maana ilibakia sh.400,000 Nilipiga cm mpaka nikakata tamaa nikafuta namba yake maisha yakaendelea Mwezi ulioisha Nikiwa pale kariakoo Nimepigika na huu Usawa wa Mjomba nilipigiwa Cm namba Ngeni baada yakupokea aliniambia za siku nyingi Fundi nami nikamjibu Nzuri akaniuza uko wapi nikamwambia nipo Ofisini Akasema Ofisini kwako nimepasahau njoo unifuate niko hapa Mtaa wa Narung'ombe nikaenda kusema kweli sikuamini macho yngu Alikua ni yule jamaa Tukaenda mpaka Ofisini Baada ya salaam akaingia mfukoni na kutoa milioni moja kisha akasema "Samahani sana kijana Wngu kipindi kile nilifukuzwa kazi nikayumba kimaisha nisamehe pia Chukua hiki kidogo" Ahsante sana Asulwise mpaka leo siamini kabisa
 

Similar Discussions

22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom