Kweli vizuri havidumu!! Pumzikeni kwa amani mashujaa wetu!! Wazalendo wa kweli...

maisha magumu ya kula ugali wa njano.bia kunywa mwisho mbili,sabuni mpaka foleni,sitalki kukumbukaaa
Kwa kweli ile ndiyo ilikuwa KUISOMA NAMBA KWELI. ..NA KWA IMANI YANGU NINAAMINI VIZURI VINAISHI. ..maana kuna KARMA. .unavuna uliyoyapanda. ..Hiyo ndiyo UNIVERSAL LAW...hamna ujanja PERIOD
 
Mbona hamuwasemi hawa walioko madarakani. Penye ukweli usemwe tu; Mmeona huyu wetu alivyo wanyong'onyesha wapiga dili?? Mmeona waziri mkuu alivyo komesha figisu zote za ujangili?? Kila mmoja analo lake buanaa. Kha!
Mpiga dili wa tanzania ni nani? Tajiri au masikini? Anayelalamika maisha magumu ni tajiri au masikini? Baada ya kunipa hayo majibu ndiyo nitajua wapiga dili wapi waliokomeshwa
 
Ni Kosa kisheria kumlinganisha Hayati Edward Moringe Sokoine na Wanafiki.

Huyu alikuwa akisema kitu Ana maanisha!

1983 kwny Operation Wahujumu Uchumi aliwatia Ndani Baadhi ya wana familia wa John Rupia Mwalimu akiwa Likizo ya X mass Butiama, aliakatiza Mapumziko na kuamuru waachiwe huru Mara moja kwa kuwa tu walikuwa Wafadhili wa Chama na Serikali tangu Zama za kupigania Uhuru na pia ni Family friend na Familia yake.

Sokoine hakuwahi kuwa Mnafiki hata kwa utani ndio sababu inasemekana na kuaminiwa na baadhi ya watu kuwa alipata 'ajali' iiyomletea Majeraha ya Risasi na kupoteza Maisha

Kile ndio kilikuwa Chuma kweli kweli
 
Sokoine alikuwa kiongozi wa kawaida sana tu,binafsi sioni cha maana cha kumwonyesha mwanangu eti ni matunda ya sokoine,huyu ni mtu ambaye alipigilia msumari wa mwisho katika jeneza la ujamaa,alizidisha hali ngumu ya uchumi kwa wananchi,

Bora Lowasa atakumbukwa kwa mradi wa maji wa ziwa victoria
Good
 
Kinachonishangaza zaidi hotuba za Waziri huyu sijawahi kuziona mahali. Sijajua ni aina ya teknolojia ilikua chini ama la! Hata kwenye vitabu hakuna.
 
Kinachonishangaza zaidi hotuba za Waziri huyu sijawahi kuziona mahali. Sijajua ni aina ya teknolojia ilikua chini ama la! Hata kwenye vitabu hakuna.
Walizifuta na kuzichoma kwani zilikuwa mkuki kwa viongozi wenzake na hata mkubwa wake. Kutokana na misimamo yake palikuwa na uadui mkubwa baina yake na mawaziri wengine kama msuya,kawawa,malecela n.k
 
Mkuu wangu huyu Jamaa alileta shida nchini sijawai ona..nilikuwa Mdogo kipindi hcho ila nakumbuka Kabisa kaka zangu kuna wakati walikuwa wanafua nguo za shule kwa kutumia majani ya Papai...hela unayo ila pa kuipata sabuni sasa???

Nakumbuka mama yangu alikuwa ananipeleka kwenye duka la ushirika kuniweka kwenye foleni naye anarudi nyumbani kufanya shughuli nyingine maana akikaa mwenyewe siku itaishia hapo..cha kusikitisha unapanga foleni siku nzima kwa ajili ya kilo Mbili Sijui za Unga wa yanga.

Inawezekana sokoine alikuwa na nia Nzuri na hii nchi ila approach yake kwa kweli ilikuwa sio kabisa...iliwapa mateso makubwa has a has a wananchi wa kawaida..

Samahani hivi kati ya rais na waziri mkuu nani mkubwa?
 
Samahani hivi kati ya rais na waziri mkuu nani mkubwa?

Mkuu mbona jibu rahisi tu ni rais...ila ukiona waziri mkuu anafanya kitu fulani na rais anamkalia kimya basi elewa kitu hcho kina Baraka Zote za rais
 
Mkuu wangu huyu Jamaa alileta shida nchini sijawai ona..nilikuwa Mdogo kipindi hcho ila nakumbuka Kabisa kaka zangu kuna wakati walikuwa wanafua nguo za shule kwa kutumia majani ya Papai...hela unayo ila pa kuipata sabuni sasa???

Nakumbuka mama yangu alikuwa ananipeleka kwenye duka la ushirika kuniweka kwenye foleni naye anarudi nyumbani kufanya shughuli nyingine maana akikaa mwenyewe siku itaishia hapo..cha kusikitisha unapanga foleni siku nzima kwa ajili ya kilo Mbili Sijui za Unga wa yanga.

Inawezekana sokoine alikuwa na nia Nzuri na hii nchi ila approach yake kwa kweli ilikuwa sio kabisa...iliwapa mateso makubwa has a has a wananchi wa kawaida..

Mazuri ya Utawala wa Nyerere hupewa Nyerere Mwenyewe na Yale Mabaya ya Utawala wake husukumiwa Mawaziri Wake. Kwa Kiswahili huu unaitwa Unafiki
 
Mkuu mbona jibu rahisi tu ni rais...ila ukiona waziri mkuu anafanya kitu fulani na rais anamkalia kimya basi elewa kitu hcho kina Baraka Zote za rais
Asante kwa jibu lako mujarabu kabisa hivyo wanaomsema yeye alisababisha hali fulani wanakosea na lawama zao wazipeleke kwa mkuu wake
 
Walizifuta na kuzichoma kwani zilikuwa mkuki kwa viongozi wenzake na hata mkubwa wake. Kutokana na misimamo yake palikuwa na uadui mkubwa baina yake na mawaziri wengine kama yona,malecela n.k

Acha uongo, Malecela, Yona na Sokoine wapi na wapi?
 
Mi ninamkumbuka Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kwa kuongeza pato la wananchi na ajira.nawakumbuka viongozi wote wa sasa na waliopita
 
Kina yona, malecela wameanza kutumikia serikali mwaka gani?

Acha Uongo, Daniel Yona kaingia kwny Cabinet Sokoine kishakufa

Waliokuwa Rank sawa na Sokoine walikuwa Rasheed Kawawa na Cleopa David Msuya uwe unauliza Wakubwa zako kabla ya kuleta usiyoyajua
 
Back
Top Bottom