Canop
Senior Member
- Jan 8, 2014
- 175
- 28
Hatujui cha kufanya...ni baada ya kutaka kugomo kuingia madarasani kwa sababu ya ukosefu wa bumu, tumeshindwa kufikia hatima yetu ya kugoma baada ya kutishiwa na mkuu wetu wa idara pamoja na waalimu eti itatugharimu kama tukigoma....pia kutokuwa na umoja baina yetu pia kumefelish jitihada zetu za kufikia malengo. Baadhi yetu wameingia madarasani na wengine kutokuja ktk kikao kilichoitishwa na mwenyekiti wa jumuiya ya Wahandisi wa SUA. Kiukweli hali ni mbaya zaidi ya maelezo....imefikia hadi mabinti kujiuza (Wahandisi-mabinti wameyasema haya leo ktk kikao kuwa wenzao wanajiuza) inasikitisha sana hali ilipofikia kwa sasa, mikate ndio mkombozi wa wengi hapa SUA (NEW HOSTEL), wauza mahindi ya kuchomwa pia wanafurahi kwani soko lake lipo juu sana ka sasa.
Wahandisi tusikate tamaa tusonge mbele na msimamo wetu wakuto ingia madarasani hadi kieleweke.....! big up kwa mwaka wa tatu kwani wameonekana ndio chachu ya mgomo.
Wahandisi tusikate tamaa tusonge mbele na msimamo wetu wakuto ingia madarasani hadi kieleweke.....! big up kwa mwaka wa tatu kwani wameonekana ndio chachu ya mgomo.