Kweli maendeleo lakini hii ya Dr Karume ni mpya.

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Karume ahutubia kupitia mkanda wa video

2008-06-25 10:26:48
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar


Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, jana aliwashangaza wanahabari, baada ya kuwaita kwenye mkutano lakini hakuzungumza nao moja kwa moja na badala yake mkanda wa video uliokuwa umerekodi hotuba yake ndiyo uliofunguliwa ili waisikilize.

Katika mkutano huo uliofanyika Ikulu, wapiga picha za magazeti hawakuambulia chochote, huku waandishi wakishindwa kuuliza maswali.

Waandishi walioshiriki mkutano huo walisema walifika kwenye viwanja vya Ikulu na kusubiri kuingia ndani kwa ajili ya kukutana na Rais Karume lakini wakati huo wakiwa nje Rais alikuwa anaongea na maelezo yake kurekodiwa.

\"Kutokana na sababu zisizoepukika hamtamuona Rais,\" alisema Msaidizi wa Rais, Bw. Haroub Said na kuwaacha wakiangalia video ya Rais inayoelezea kile alichokuwa amewaitia.

Katika mkanda huo, Rais alizungumzia ma suala ya umeme Zanzibar, kuwa serikali iko mbioni kununua majenereta ya kuzalisha umeme wa dharura iwapo kutatokea hitilafu katika gridi ya taifa ya umeme wa Bara.

Alisema serikali yake imeagiza vipuri kwa ajili ya kukarabati majenereta yaliyoko Unguja ambavyo baadhi ya vipuri vyake vilipelekwa Pemba kutengeneza mashine za kufua umeme zilizoharibika.

Rais Karume alisema tatizo la umeme litatatuliwa kwa kuwa na ufumbuzi wa kudumu na kwa sasa Marekani kupitia Akaunti ya Changamoto za Milenia (MCC) inaisaidia Zanzibar kutandaza waya mpya wa umeme wa chini ya bahari.

Akizungumzia kauli za watu waliosema serikali yake haitamaliza tatizo la umeme, aliwaambia waliotoa vijembe hivyo sasa watimize yale waliyotamka.

``Kuna watu waliosema kama umeme huu utarudi ndani ya mwezi mmoja watanyoa ndevu zao, tunataka sasa wanyoe kama hawana viwembe tutawapatia,`` alisema katika hotuba yake iliyorekodiwa.
 
he he heeee akutukanaye hakuchagulii tusi, kunakutia akili hapo.
 
Nafikiri amejitahidi sasa angalau anaanza kufikiri kuwa na mitambo ya Umeme wa dharura lakini mukumbushe asilete IPTL au Richmond zanzibar.

Lakini ya kuwawekea video ilikuwa kali.
 
Ndiyo jeuri ya ukubwa hiyo!! Ya nini ukutane na waandishi wa habari wakati unaweza kurekodi mkanda na kuwawekea wasikilize? Nao wafanye jeuri ya kutoandika au kutangaza chochote kilichomo ndani ya mkanda huo.
 
alikuwa mtoto wa kijiweni saana tena .... kwa mkojo wa firauni humwambii kitu ... sijui kama hawachafulii CCM maana kipindi chake kinayoyoma .... na kila kukicha anazidisha nyodo na kusema hovyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom