Kweli hii ni Nchi ya ahadi

onyx

JF-Expert Member
Mar 17, 2016
1,587
1,306
Nimekaa nimetafakari mambo yanavyoenda katika hii nchi, nikaja kuifananisha na nchi ya ahadi. Katika nchi ya ahadi hakuna mwenye kuridhika na kile kinachoendelea. Huyu anaiba hela waziwazi tena za wananchi wanaovuja jasho, yule analalamika haki na usawa, yule analalamika kodi kubwa. Jamani nawaomba watanzania wenzangu tuwe kitu kimoja, maana sasa inakuwa kero. Inabidi tuwe na forums za kuelimisha kwa kila nyanja, ili tupeane mawazo mbadala ni namna gani tutaondokana na hii hali ya kila mtu haridhiki. Nashauri ianzishwe forum ya kutoa mawazo mbadala ya kila nyanja.


Nawasilisha
 
Back
Top Bottom