Kweli dunia inazunguka jua au jua ndo linazunguka dunia?

ulimi waupanga

JF-Expert Member
Aug 31, 2014
470
1,161
Nimekuwa nikijiuliza swali hili kwa muda sasa, Wanasayansi wanadai Jua ni moja kati ya nyota zinazoipatia mwangaza na nishati Dunia. Wanaendelea kudai Jua limesimama wima na Dunia iko kwenye mwendo ikilizunguka jua, kudhibitisha ilo wamekuwa wakitoa nadharia mbalimbali kama vile mtu akiwa kwenye gari jinsi anavyoona miti inatembea wakati gari alilomo ndo linatembea. Kwa kusoma kitabu cha Enoch anadai alionesha na malaika wa mungu kuhusu siri za uumbaji wa ulimwengu yakwamba Jua linaizunguka Dunia na mwezi pia unaizunguka Dunia na pia mwezi na Jua vinalingana ukubwa sema mwanga wa Jua ni x7 ya mwanga wa mwezi. Nimekuwa na maswali machache juu nadharia ya wanasansi wetu kuwa Dunia inazunguka Jua:

I) Kama ni kweli kwa nini nyota za Usiku tusione zinatembea kama lilivyo Jua? Maana Dunia inazunguka muda wote.

ii) Kwa nini mwezi husionekane umesimama ili kuapprove point ya mtu alopanda gari lililo kwenye mwendo maana wanadai na mwezi nao unaizunguka Dunia ina maana vyote viko kwenye mwendo. Mfano fanya jaribio ukiwa kwenye basi chungulia nje wakati mna overtake basi jingine utaliona kama limesimama lakini kiukweli liko kwenye mwendo.

iii) Kwa vile tuko kwenye uso wa Dunia na hatujafunikwa na chochote dhidi ya upepo( yaani hewa iliyo kwenye mwendo) kwa nini tusihisi effect ya kukatiza kwenye upepo wakati tukizunguka na Dunia kama inavyotekea ukipanda gari lililowazi?

Mwenye ufafanuzi wa haya tafadhali tusaidiane maana nikitafakari sana naona Enoch yuko sahihi.
 
Sasa hivi siyo nadharia tena, na satelites na vyombo vinavyoelea angani hivyo vimeprove hilo.
Usisahau planet x ya bwana Elon Musk anataka apeleke watu Mars 2022.
Soon anajiandaa na utalii wa kwenda kuzunguka mwezini mkuu kama vipi lipia ukashuhudie
 
he he! ngoja nijikune mgongo!

jua lizunguke sayari tisa:D is this logic true..? tatizo huwa mnaifikiria dunia tu! Ooops!! sasa jua 1 linazunguka dunia,jupiter,saturn n.k.. nafikiri unataka kuja na logic mpya!:eek:.

mkuu dunia inatabaka hewa i mean ozon layer,hili limezunguka dunia ili kuzuia hewa n.k visitoke na ndio linalokinga hata hivyo unavyosema dunia kupata maupepo ha ha ha.. sasa ndugu hayo maupepo yatokee wapi wkt after ozon layer kuna space tu! ha ha ha.. tabaka la ozon layer lisinge kuwepo hata hewa tungekuwa tumeshapoteza ingesambaa kwenye space ha ha ha.. sayansi inawenyewe jamani! ndo maana hata kwenye ule uzi wa earth flat niliupuuza tu zile fact silolote!.

umbali uliopo toka dunia na hizo nyota nyengine ni ngumu kuona zinamove kama unavyodhani ila zina move ndio lkn it take a long time kiasi,wataka prove? go outside ziangalie zikalili.. and then amka saa kumi na moja ziangalie leta jibu.. pia hata baada ya miezi kadhaa huwa zinachange position unatakiwa uwe unazifatilia tu utaona.
 
Sayansi na vitabu vya dini havijawahi kuelewana kuna upande mmoja facts upande mwingine imani tu
 
Ndugu zangu, Mimi nimekua nikisoma shuleni kuwa dunia ni mviringo, na inazunguka jua. Lakini ndani ya kitabu cha Biblia ambacho Mungu anayeelezewa humo ndiye ninayemuamini, (JEHOVA), jua ndiyo linalozunguka dunia, wakati dunia imetilia tuli. Tena dunia ni flat disc, na sio globe. Katika kitabu cha Joshua agano la kale Joshua alipokuwa vitani, alimuomba Mungu usiku usiingie hadi atakapowashinda adui zake. Kweli maandiko yanasema jua lilisimama mpaka alipowamaliza adui zake. Vile vile, maandiko katika zaburi yanaonyesha kuwa dunia imejengwa kwenye misingi yake, isiyoyumba wala kutikisika. Tena cha kushangaza maandiko yanasema katika kitabu cha Ayubu kuwa dunia imefunikwa na mfuniko wa kioo unaon'gaa ( molten glass dome)... Kitabu cha Enoch, kinaongelea mambo mengi ikiwa ni pamoja na dunia kuwa flat, pia sehemu ya chini ya dunia( Bara la Antarica) ambamo inasemekana malaika 200 walifungwa huko. Kwa vile kitabu cha Enoch sio sehemu ya vitabu vya Biblia, ni makosa kuungnisha maelezo ya Biblia na kitabu cha Enoch kwa sababu hatujui mwandishi wa kitabu hicho ni nani. Yawezekana mwandishi akawa ni Malaika waliofukuzwa Mbinguni(fallen angels au demons)..Vyovyote vile, uwe dunia inazunguka jua, au jua linazunguka dunia ndani au nje ya dome,au dunia ni flat au ni globe, badoneno la Mungu linabaki kuwa dunia imewekwa juu ya misingi na yeye aliyeiumba. Jitenge na kitabu cha Enoch; kama wewe ni Mkristo usipende kupekua ndani ya kitabu hicho yamo mambo yanayomuelekeza Mtu katika kuabudu demons na fallen angels.
 
Ndugu zangu, Mimi nimekua nikisoma shuleni kuwa dunia ni mviringo, na inazunguka jua. Lakini ndani ya kitabu cha Biblia ambacho Mungu anayeelezewa humo ndiye ninayemuamini, (JEHOVA), jua ndiyo linalozunguka dunia, wakati dunia imetilia tuli. Tena dunia ni flat disc, na sio globe. Katika kitabu cha Joshua agano la kale Joshua alipokuwa vitani, alimuomba Mungu usiku usiingie hadi atakapowashinda adui zake. Kweli maandiko yanasema jua lilisimama mpaka alipowamaliza adui zake. Vile vile, maandiko katika zaburi yanaonyesha kuwa dunia imejengwa kwenye misingi yake, isiyoyumba wala kutikisika. Tena cha kushangaza maandiko yanasema katika kitabu cha Ayubu kuwa dunia imefunikwa na mfuniko wa kioo unaon'gaa ( molten glass dome)... Kitabu cha Enoch, kinaongelea mambo mengi ikiwa ni pamoja na dunia kuwa flat, pia sehemu ya chini ya dunia( Bara la Antarica) ambamo inasemekana malaika 200 walifungwa huko. Kwa vile kitabu cha Enoch sio sehemu ya vitabu vya Biblia, ni makosa kuungnisha maelezo ya Biblia na kitabu cha Enoch kwa sababu hatujui mwandishi wa kitabu hicho ni nani. Yawezekana mwandishi akawa ni Malaika waliofukuzwa Mbinguni(fallen angels au demons)..Vyovyote vile, uwe dunia inazunguka jua, au jua linazunguka dunia ndani au nje ya dome,au dunia ni flat au ni globe, badoneno la Mungu linabaki kuwa dunia imewekwa juu ya misingi na yeye aliyeiumba. Jitenge na kitabu cha Enoch; kama wewe ni Mkristo usipende kupekua ndani ya kitabu hicho yamo mambo yanayomuelekeza Mtu katika kuabudu demons na fallen angels.
Ivi Leo hii hao wanasayansi huwa wanasema.

(a) Jua litachomoza saa 12 Asubuhi na kuzama saa 1 Jioni.

(b) Au huwa wanasema dunia itazunguka na kuwezesha Jua kuonekana saa 12 asubuhi na kutoonekana saa 1 jioni.

Au ulitaka Joshua aseme dunia ilisimama ?

Ujue kuna matendo ya Kisayansi na lugha inayotumika kuelezea matukio ya Kisayansi.

Lugha zote huwa zinaliweka Jua kuwa Subject yaani (mtenda) na dunia inawekwa ktk Object (mtendewa)

Hivyo hata ukisikiliza utabiri wa hali ya hewa, Wanasayansi wa dunia yote leo, huwa wanasema na wanaendelea kusema,
Jua litachomoza au litazama au Litapatwa, pamoja na kujua kuwa Jua halitembei.

Hivyo Joshua alikuwa Sahihi kabisa kusema Jua lilisimama, maana hata leo angesema vivyohivyo kama wanavyoendelea kusema hao wanasayansi.
 
Tulikuwa na mwalimu wetu Mjapani alikuwa anafundisha Basic Mathematica, usipo elewa na alikuelekeza anakuambia Utakuja Kuelewa Siku ya Kufa. Huwa nilikuwa ninajiuliza inamaana siku ya kufa mambo mengi mtu aliyekuwa ajuih atakuja kuelewa hiyo siku ya kufa. Siku ya kufa ndo siku pekee ya kuelewa na kujua ukweli Lakin hatutakuwa na muda Tena.
 
Tulikuwa na mwalimu wetu Mjapani alikuwa anafundisha Basic Mathematica, usipo elewa na alikuelekeza anakuambia Utakuja Kuelewa Siku ya Kufa. Huwa nilikuwa ninajiuliza inamaana siku ya kufa mambo mengi mtu aliyekuwa ajuih atakuja kuelewa hiyo siku ya kufa. Siku ya kufa ndo siku pekee ya kuelewa na kujua ukweli Lakin hatutakuwa na muda Tena.
Hapo umezungumza Falsafa nzito sana.
Baadhi yetu tuna bahati mbaya sana, tumejikuta tupo katika jamii au ulimwengu wa, sio tu Kijinga bali wa Kipumbavu kabisa, na tutaangamia nao huo upumbavu.

Kuna mahali kwenye Biblia pameandikwa.
Wana Masikio lakini hawasikii, wana Macho lakini hawaoni, wamefanywa hivyo ili wasielewe kinachoendelea na waishie kuangamizwa.

Hakika Siku ya kufa ndio itakayo wafumbua macho watu wengi na siku hiyo ndipo watakapo uelewa ukweli.

Huyo Mwalimu wako wa Kijapani alikuwa na maarifa mapana sana. Iko mijitu hata ukiionya vipi haionyeki, ukiifundisha namna gani haifundishiki.
Leo hii watu wanawadharau na kuwafanyia ubaya watu bila hatia, wengine wanawatukana hata wazazi wao, watu ni wakatili, wezi, wafitini na ubaya mwingi, wamefikia hatua ya kuchinja watu wasio na hatia kama wanachinja kuku na wanafurahia hilo tendo,
wao wanajua hakuna madhara watakayoyapata kwa hayo matendo yao.
Wengine wamefikia hatua ya kumtukana Mungu muumba Mbingu na Nchi na kutamka hadharani
"Hakuna Mungu "

Hakika Siku ya Kufa ndiyo itakayotoa majibu.

Ngoja tukisubiri KIFO.
 
Ndugu zangu, Mimi nimekua nikisoma shuleni kuwa dunia ni mviringo, na inazunguka jua. Lakini ndani ya kitabu cha Biblia ambacho Mungu anayeelezewa humo ndiye ninayemuamini, (JEHOVA), jua ndiyo linalozunguka dunia, wakati dunia imetilia tuli. Tena dunia ni flat disc, na sio globe. Katika kitabu cha Joshua agano la kale Joshua alipokuwa vitani, alimuomba Mungu usiku usiingie hadi atakapowashinda adui zake. Kweli maandiko yanasema jua lilisimama mpaka alipowamaliza adui zake. Vile vile, maandiko katika zaburi yanaonyesha kuwa dunia imejengwa kwenye misingi yake, isiyoyumba wala kutikisika. Tena cha kushangaza maandiko yanasema katika kitabu cha Ayubu kuwa dunia imefunikwa na mfuniko wa kioo unaon'gaa ( molten glass dome)... Kitabu cha Enoch, kinaongelea mambo mengi ikiwa ni pamoja na dunia kuwa flat, pia sehemu ya chini ya dunia( Bara la Antarica) ambamo inasemekana malaika 200 walifungwa huko. Kwa vile kitabu cha Enoch sio sehemu ya vitabu vya Biblia, ni makosa kuungnisha maelezo ya Biblia na kitabu cha Enoch kwa sababu hatujui mwandishi wa kitabu hicho ni nani. Yawezekana mwandishi akawa ni Malaika waliofukuzwa Mbinguni(fallen angels au demons)..Vyovyote vile, uwe dunia inazunguka jua, au jua linazunguka dunia ndani au nje ya dome,au dunia ni flat au ni globe, badoneno la Mungu linabaki kuwa dunia imewekwa juu ya misingi na yeye aliyeiumba. Jitenge na kitabu cha Enoch; kama wewe ni Mkristo usipende kupekua ndani ya kitabu hicho yamo mambo yanayomuelekeza Mtu katika kuabudu demons na fallen angels.
Uliposema tisikisome hicho kitabu cha Enoch
Naona unataka kuwaweka watu mbali na ukweli wenyewe kitabu kile kina sina siri hao waliyo kufanya uamini hivyo wamefanya kwa sababu unajua hata kitabu cha ufunuo kilitakiwa kisiwepo kwenye biblia kilipona kwa sababu ya ugumu wake wa kutokueleweka kirahisi
 
Uliposema tisikisome hicho kitabu cha Enoch
Naona unataka kuwaweka watu mbali na ukweli wenyewe kitabu kile kina sina siri hao waliyo kufanya uamini hivyo wamefanya kwa sababu unajua hata kitabu cha ufunuo kilitakiwa kisiwepo kwenye biblia kilipona kwa sababu ya ugumu wake wa kutokueleweka kirahisi
Naomba nichangie katika hili, hata sisi waislamu tunasoma kwenye Kurani kwamba jua nalo linaenda kwenye mzunguko wake. sura 36 aya 38 inasema, "Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua."
 
Quran imebeba majibu yote ambayo sayansi ya leo ina prove ni kweli hakuna scientific error katika kitabu kisicho na shaka ndani yake....

Allah anasema na tumeiumba dunia kwa mfano wa yai la mbuni...yaan (geospherical) sio duara kabisa complete kama flat kidogo juu na chini halafu kati kati mi umbo la duara.

Kuhusu jua Quran inasema dunia,jua mwez vyote vinazunguka kwenye orbit yake..leo sayans inasema pamoja na dunia kuizunguka jua na jua nalo linazunguka kwemye orbit yake na limachukua siku 26 kumakiza mzunguko wake kuna kitu wanakiita black spot ndio alama ya kupimia mzunguko wa jua.!

Haya yameandikwa miak 1400 iliyopita akateremshiwa mtume asiejua kusoma wala kuandika ili Mungu kudhihurishs uwepo wake na ukubwa wake na ndio maana kayasema haya kipind cha giza kabla hamna vyombo vya uchunguzi huko angani ambavyo vinathibitisha yaliosemwa na Allah
 
he he! ngoja nijikune mgongo!

jua lizunguke sayari tisa:D is this logic true..? tatizo huwa mnaifikiria dunia tu! Ooops!! sasa jua 1 linazunguka dunia,jupiter,saturn n.k.. nafikiri unataka kuja na logic mpya!:eek:.

mkuu dunia inatabaka hewa i mean ozon layer,hili limezunguka dunia ili kuzuia hewa n.k visitoke na ndio linalokinga hata hivyo unavyosema dunia kupata maupepo ha ha ha.. sasa ndugu hayo maupepo yatokee wapi wkt after ozon layer kuna space tu! ha ha ha.. tabaka la ozon layer lisinge kuwepo hata hewa tungekuwa tumeshapoteza ingesambaa kwenye space ha ha ha.. sayansi inawenyewe jamani! ndo maana hata kwenye ule uzi wa earth flat niliupuuza tu zile fact silolote!.,

umbali uliopo toka dunia na hizo nyota nyengine ni ngumu kuona zinamove kama unavyodhani ila zina move ndio lkn it take a long time kiasi,wataka prove? go outside ziangalie zikalili.. and then amka saa kumi na moja ziangalie leta jibu.. pia hata baada ya miezi kadhaa huwa zinachange position unatakiwa uwe unazifatilia tu utaona.

mkuu hizi uloweka hapa ni nukuu za vitabu tu,hebu tujaribu tuviweke pembeni hivi vitabu kwa muda mfupi tu na tuangalie vitu kwa macho yetu
hapo chini kuna picha halisi ya jua likiwa angani linakaribia kuzama litazame jua kisha uangalie nyuma ya jua kuna mawingu,itazame picha kwa makini sana itazame mistari y mawingu iliyo nyuma ya jua kisha ujiulize kama kweli jua lipo 93 mil mile away tungeliona kama hivi.
science ya kweli ya ulimwengu haijulikani ipo vipi, lakini mimi imani yangu ni kuwa jua,mwezi nyota na sayari zote zimo ndani ya dunia,anga ya dunia ina mzunguko ambao unalizungusha jua,mwezi nyota na sayari kila siku,mchana na usiku, na hakuna aliyewahi kuona nje ya dunia kwa maana ya outter space,wala hakuna outter space,, yaani hii ni sawa na kifo hakuna mtu aliewahi kuona upande wa pili wa kifo kwa maana sisi binadamu hatuna uwezo wa kujua upande wa kifo upo vipi, na kwa dunia sheria zake zipo hivo hivo kuwa hamna anaweza kutoka hapa wala kuona nje ya dunia,tulobakia nazo ni propaganda na misinformation tu.

hapo umegusia nyota na mie niseme kuhusu maajabu ya nyota,wanasayansi wanasema nyota zilizo karibu ni 4.2 light yrs away kwa maana ya masafa ya 40 trillion km away, cha ajabu hapa ni kuwa sisi binadamu tunaziona nyota kila siku lakini tujiulize hivi kweli macho yetu ya binaadamu yana uwezo wa kuona kitu kilicho umbali wa 40 tri km,tena hizo ndio za karibu,uhalisi ni kuwa sisi binadamu macho yetu hayana uwezo wa kuona hata umbali wa km laki moja,kwa ufupi vitu vyote vipo karibu sana, ndio mana tunaviona kwa macho yetu,mpaka wazee wakongwe wanaziona nyota.



Capturez.JPG
 
Dunia ndio ulizunguka jua,na Kuna mizunguko mikuu miwili ambao ni;
✓dunia kulizunguka jua,na ndio upelekea kuweza kupata usiku na mchana(day&night).
✓dunia kujizungusha katika muhimili wake,na ndio upelekea kuwa na majira{season} Kama vile, summer, winter, autumn
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom