Kwasababu CCM wanapenda uongo na magoli ya mikono, COVID-19 haipendi uongo itawaondoa madarakani!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Utaratibu wa ccm kutawala nchi yetu umekuwa ukigubikwa na usiri mwingi, uchakachuaji wa data, uongo uongo, propaganda, wasiojulikana na magoli ya mikono! Vyote hivyo ni adui namba moja pale inapokuja kwenye corona virus(covid-19) šŸ¦ 

Hivyo ccm lazima ipoteze uchaguzi mkuu ujao, hata kama wakiwapa wanachama wao barakoa za bure badala ya kofia, t-shirts ama pilau!

Lakini kwa haya yanayoendelea, baadaye mtakuja kusema labda rais alifanya makusudi ili aendelee kutawala... Kwanza ikifika wakati wa uchaguzi hali inaweza kuwa mbaya zaidi na minamba ikawekwa kujustify uchaguzi kufutwa indefinitely. Pamoja na campaign. Pesa itasemekana zinaenda kwenye corona. Kwasababu hata sasa namba zinatolewa kwa kauli kutoka juu!

Hii corona bila shaka itaondoka na serikali nyingi sana, maana gonjwa limekuja karibia na uchaguzi mkuu. Huku kwetu tumeambiwa tujifukize na kuchapa kazi...Hata Marekani, Trump naye ka panic hivyo hivyo anasema watu wajipige sindano za bleach na pia wajianike juani watapona corona!šŸ¤¦šŸ¾ā€ā™‚ļø

Kiongozi wa ukweli anapimwa wakati wa mgogoro kama huu. Na siyo tu kwenye mabavu ya kukusanya kodi na kuzitumia anavyotaka! Kabla hata ya corona, huu mwaka ulikuwa wa changamoto kubwa sana kwa ccm. Sasa corona imeingia, kama hakuna hatua madhubuti, ni bora wapinzani nao waanze kuja na mawazo mbadala ya namna tutakayokabiliana na corona, maana ni wazi gonjwa hili litakuwepo kwa muda, hivyo tunahitaji mikakati ya muda mfupi na mrefu. Siyo kutegemea miujiza! Lakini kwa hali hii ya sasa, tutaenda kuuzika uchumi wetu!

Kwamfano hata hao watalii tunaowategemea, wakati huko kwao kukiwa sawa, unadhani serikali zao zita recommend raia wake waje nchini? Kwasababu hao watu wanakwenda na statistics, halafu pia wanafahamu yanayoendelea. Hata ufiche vipi kwanza now days kuna satellites mnaonekana wazi tu huko makaburini mkiwazika waliopatikana na covid-19 na kupoteza maisha yao...hata kama ni usiku wa manane kama wananchi wanavyodai mnaonekana. Kuna picha zinasambaa zikiwaonyesha wazikaji wa usiku.

Kuficha haisadii! Mnadhani Marekani, Italy na Spain walipenda kuoneakana wakiwa vile? Waliamuwa kuonyesha ili kuweza ku create enough awareness. Huwezi kuwa na hofu kubwa kama unafuata maelekezo ya wataalam. Kuficha kunaondoa ile tahadhari ambayo ni muhimu kuweza kuokoa maisha ya wananchi.

Mods tafadhali musiichinjie baharini hii ni angalizo tu kwa uchaguzi mkuu ujao. Wananchi wanahitaji wasikie alternative ideas. Tuuachie usambae kama tunavyofanya, ambayo ni model ya ā€œThe fittest surviveā€, ambapo asilimia 70-90 ya wananchi wote wanatakiwa kupata covid-19 ndo tuanze kusema tuko salama, ama tuende na partial lockdowns huku tukiongeza uwezo wa kupima ili Idara yetu ya afya isizidiwe kwenye kutoa huduma? Hii ndo inayoitwa ā€œflattening the curveā€

Siyo ajabu wananchi tukaja kuzuiwa kupiga kura kama kina Pasco wamekuwa wakisema hakuna haja ya uchaguzi bali Maghufuli kisha muda wake ukiisha amkabidhi Makonda.
 
Watu wanachojari ni mapenzi ya vyama vyao na hawana sababu zengine na hiyo ni kwa ccm na upinzani,kama watu wangekuwa wanaangalia sababu zengine basi hadi leo ccm ngekuwa historia.
 
Utaratibu wa ccm kutawala nchi yetu umekuwa ukigubikwa na usiri mwingi, uchakachuaji wa data, uongo, propaganda na magoli ya mikono! Vyote hivyo ni adui namba moja pale inapokuja kwenye corona virus šŸ¦ 

Hivyo ccm lazima ipoteze hata wakiwapa wanachama wao barakoa za bure badala ya kofia ama t-shirts.

Lakini kwa haya yanayoendelea, baadaye mtakuja kusema labda rais alifanya makusudi ili aendelee kutawala. Kwanza ikifika wakati wa uchaguzi hali inaweza kuwa mbaya zaidi na minamba ikawekwa kujustify uchaguzi kufutwa indefinitely. Pamoja na campaign. Pesa itasemekana zinaenda kwenye corona.

Hii corona bila shaka itaondoka na serikali nyingi sana, maana gonjwa limekuja karibia na uchaguzi mkuu hata Marekani Trump naye ka panic hivyo hivyo anasema watu wajipige sindano za bleach na pia wajianike juani watapona corona!šŸ¤¦šŸ¾ā€ā™‚ļø

Kiongozi wa ukweli anapimwa wakati wa mgogoro kama huu. Kabla hata ya corona, huu mwaka ulikuwa wa changamoto kubwa sana kwa ccm. Sasa corona imeingia, kama hakuna hatua madhubuti, ni bora wapinzani nao waanze kuja na mawazo mbadala ya namna tutakayokabiliana na corona, maana ni wazi litakuwepo kwa muda. Lakini kwa hali hii ya sasa, tutaenda kuuzika uchumi wetu!

Kwamfano hata hao watalii tunaowategemea, wakati huko kwao kukiwa sawa, unadhani serikali zao zita recommend raia wake waje nchini? Kwasababu hao watu wanakwenda na statistics, halafu pia wanafahamu yanayoendelea. Hata ufiche vipi kwanza now days kuna satellites mnaonekana uchi tu.

Mods tafadhali musiichinjie baharini hii ni angalizo tu kwa uchaguzi mkuu ujao. Wananchi wanahitaji wasikie alternative ideas. Tuuachie usambae ambayo ni mode ya ā€œThe fittest surviveā€, ama tuende na partial lockdowns huku tukiongeza uwezo wa kupima.

Siyo ajabu wananchi tukajazuiwa kupiga kura kama kina Pasco wamekuwa wakisema hakuna haja ya uchaguzi bali Maghufuli kisha amkabidhi Makonda.
Natamani sana ifike chato na kongwa
 
Utaratibu wa ccm kutawala nchi yetu umekuwa ukigubikwa na usiri mwingi, uchakachuaji wa data, uongo, propaganda na magoli ya mikono! Vyote hivyo ni adui namba moja pale inapokuja kwenye corona virus

Hivyo ccm lazima ipoteze hata wakiwapa wanachama wao barakoa za bure badala ya kofia ama t-shirts.

Lakini kwa haya yanayoendelea, baadaye mtakuja kusema labda rais alifanya makusudi ili aendelee kutawala. Kwanza ikifika wakati wa uchaguzi hali inaweza kuwa mbaya zaidi na minamba ikawekwa kujustify uchaguzi kufutwa indefinitely. Pamoja na campaign. Pesa itasemekana zinaenda kwenye corona.

Hii corona bila shaka itaondoka na serikali nyingi sana, maana gonjwa limekuja karibia na uchaguzi mkuu hata Marekani Trump naye ka panic hivyo hivyo anasema watu wajipige sindano za bleach na pia wajianike juani watapona corona!

Kiongozi wa ukweli anapimwa wakati wa mgogoro kama huu. Kabla hata ya corona, huu mwaka ulikuwa wa changamoto kubwa sana kwa ccm. Sasa corona imeingia, kama hakuna hatua madhubuti, ni bora wapinzani nao waanze kuja na mawazo mbadala ya namna tutakayokabiliana na corona, maana ni wazi litakuwepo kwa muda. Lakini kwa hali hii ya sasa, tutaenda kuuzika uchumi wetu!

Kwamfano hata hao watalii tunaowategemea, wakati huko kwao kukiwa sawa, unadhani serikali zao zita recommend raia wake waje nchini? Kwasababu hao watu wanakwenda na statistics, halafu pia wanafahamu yanayoendelea. Hata ufiche vipi kwanza now days kuna satellites mnaonekana uchi tu.

Mods tafadhali musiichinjie baharini hii ni angalizo tu kwa uchaguzi mkuu ujao. Wananchi wanahitaji wasikie alternative ideas. Tuuachie usambae ambayo ni mode ya ā€œThe fittest surviveā€, ama tuende na partial lockdowns huku tukiongeza uwezo wa kupima.

Siyo ajabu wananchi tukajazuiwa kupiga kura kama kina Pasco wamekuwa wakisema hakuna haja ya uchaguzi bali Maghufuli kisha amkabidhi Makonda.
Mkuu Mushi, janga la Corona limekuja hivyo imewashinda kufuata masharti ya kishetani ya kafara za mwenge wa uhuru, matokeo yake wamebakia kuona mauzauza na hata kukimbiakimbia hovyo. Ibilisi hajawahi kumuacha mtumwa wake salama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ccm iondolewe madarakani na nani?

Chadema

Vijana acheni mbege za marangu zinaharibu ubongo
Mkuu kwanini unasahau kuwa nchi hii ina watu zaidi ya milioni 55? Unadhani miaka yote watu hawa wataendelea kupelekeshwa na kikundi cha watu wasiozidi milioni kumi kinachoitwa ccm?

Wanao shiriki maigizo yenu ya uchaguzi ni wajinga wenzenu wanaccm na wanachama na mashabiki wachache wa vyama ambao jumla yao hata haifiki 20 milioni sasa tell me hawa wengine zaidi ya milioni 40 wako wapi na wanafikiria Nini kuhusu siasa uchwara mnazoendesha hapa Tanzania
 
Naomba Mungu Hali isiwe mbaya na kutosha hadii tiba ipatikane watu tuwe huru.

Sent using Jamii Forums mobile app
Bila hatua stahiki hakuna lolote. Hatua za kupunguza maambukizi zitapunguza vifo na kuokoa uchumi kuliko hivi sasa. Wapinzani wana nafasi kutoa mwelekeo wao maana Taifa lina hitaji uongozi madhubuti.

Ukizingitia corona is here to stay na kwa utaratibu uliopo ni bora self quarantine iendelee hadi uchaguzi uje tusikie mawazo mbadala ya namna ya kukabiliana na huyu adui ambaye ni hatari kwa mustakabali wa Taifa na dunia kwa ujumla.
 
Acha masikhara Mangi. Magufuli amkabidhi Makonda wapi na wapi? By the way, mshua wako wa "Got Poop?" aka Nyani Ngabu kaishia wapi?
Pascal Mayalla ndiye aliyesema hayo mkuu.

Kuhusu Ngabu, hata kumtag siwezi labda alishani block who knows? Hata hivyo nimemuulizia sana sijapata jibu. Yeye yuko Atalanta ambapo hali ilikuwa mbaya huko na yeye ni mtu mzima.

Tuendelee kumuombea pengine ni quarantine tu ya kawaida! Pamoja na kwamba sijui inawezekana vipi kwenye hii lockdown apotee? Sana sana ilitakiwa awe more available if anything.
 
Sasa nchi yetu uchumi kwanza corona iwepo tu maana mpaka Sasa hamna mipango yoyote ya kuokoa uchumi hasa kipindi hichi Cha corona I thought juzi Mr. President angeongelea hatua gani ambazo wamejiandaa ili ku boost uchumi, hasa sector binafsi ambayo imepata madhara, utalii ambao ni chanzo Kikuu Cha mapato na feza za kigeni, maana hatuna lockdown Ila vitu na biashara nyingi zimepata madhara.

Pia serikali nayo hatua za kudhibiti guidelines ni Kama imepuuza guidelines za WHO Sasa huku nchi nyingine zikifanikiwa kudhibiti corona sisi si ndo tutapigwa stop kabisa Mana tutaonekana ni supplier wacorona, nafikiria serikali ifikirie future zaidi, maana serikali watenda maamuzi akili zimegoma wanawaza uchaguzi mkuu zaidi, kuliko hata kudhibiti hii corona.
Bila hatua stahiki hakuna lolote. Hatua za kupunguza maambukizi zitapunguza vifo na kuokoa uchumi kuliko hivi sasa. Wapinzani wana nafasi kutoa mwelekeo wao maana Taifa lina hitaji uongozi madhubuti. Ukizingitia corona is here to stay na kwa utaratibu uliopo ni bora self quarantine iendelee hadi uchaguzi uje tusikie mawazo mbadala ya namna ya kukabiliana na huyu adui ambaye ni hatari kwa mustakabali wa Taifa na dunia kwa ujumla.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa nchi yetu uchumi kwanza corona iwepo tu maana mpaka Sasa hamna mipango yoyote ya kuokoa uchumi hasa kipindi hichi Cha corona I thought juzi Mr. President angeongelea hatua gani ambazo wamejiandaa ili ku boost uchumi, hasa sector binafsi ambayo imepata madhara, utalii ambao ni chanzo Kikuu Cha mapato na feza za kigeni, maana hatuna lockdown Ila vitu na biashara nyingi zimepata madhara.

Pia serikali nayo hatua za kudhibiti guidelines ni Kama imepuuza guidelines za WHO Sasa huku nchi nyingine zikifanikiwa kudhibiti corona sisi si ndo tutapigwa stop kabisa Mana tutaonekana ni supplier wacorona, nafikiria serikali ifikirie future zaidi, maana serikali watenda maamuzi akili zimegoma wanawaza uchaguzi mkuu zaidi, kuliko hata kudhibiti hii corona.

Sent using Jamii Forums mobile app
Serikali iliyochoka itapata wapi hela za kuboost sector binafsi,au mnataka watumishi wa umma wasipate mishahara?
 
Watumie njia mubadala waandike proposal huko kwenye mashirika makubwa jinsi wanavokabiliana na corona, pia njia za ku boost uchumi, mbona Kuna nchi ka Msumbiji, Malawi zimefutiwa madeni na kupewa msaada wa kupambana na covid, Sasa sie tukijfanya donor country tutaumia
Serikali iliyochoka itapata wapi hela za kuboost sector binafsi,au mnataka watumishi wa umma wasipate mishahara?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom