barafuyamoto
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 32,323
- 29,584
Inaondolewa na nani sasa?Utaratibu wa ccm kutawala nchi yetu umekuwa ukigubikwa na usiri mwingi, uchakachuaji wa data, uongo, propaganda na magoli ya mikono! Vyote hivyo ni adui namba moja pale inapokuja kwenye corona virus đź¦
Hivyo ccm lazima ipoteze hata wakiwapa wanachama wao barakoa za bure badala ya kofia ama t-shirts.
Lakini kwa haya yanayoendelea, baadaye mtakuja kusema labda rais alifanya makusudi ili aendelee kutawala. Kwanza ikifika wakati wa uchaguzi hali inaweza kuwa mbaya zaidi na minamba ikawekwa kujustify uchaguzi kufutwa indefinitely. Pamoja na campaign. Pesa itasemekana zinaenda kwenye corona.
Hii corona bila shaka itaondoka na serikali nyingi sana, maana gonjwa limekuja karibia na uchaguzi mkuu hata Marekani Trump naye ka panic hivyo hivyo anasema watu wajipige sindano za bleach na pia wajianike juani watapona corona!🤦🏾‍♂️
Kiongozi wa ukweli anapimwa wakati wa mgogoro kama huu. Kabla hata ya corona, huu mwaka ulikuwa wa changamoto kubwa sana kwa ccm. Sasa corona imeingia, kama hakuna hatua madhubuti, ni bora wapinzani nao waanze kuja na mawazo mbadala ya namna tutakayokabiliana na corona, maana ni wazi litakuwepo kwa muda. Lakini kwa hali hii ya sasa, tutaenda kuuzika uchumi wetu!
Kwamfano hata hao watalii tunaowategemea, wakati huko kwao kukiwa sawa, unadhani serikali zao zita recommend raia wake waje nchini? Kwasababu hao watu wanakwenda na statistics, halafu pia wanafahamu yanayoendelea. Hata ufiche vipi kwanza now days kuna satellites mnaonekana uchi tu.
Mods tafadhali musiichinjie baharini hii ni angalizo tu kwa uchaguzi mkuu ujao. Wananchi wanahitaji wasikie alternative ideas. Tuuachie usambae ambayo ni mode ya “The fittest survive”, ama tuende na partial lockdowns huku tukiongeza uwezo wa kupima.
Siyo ajabu wananchi tukajazuiwa kupiga kura kama kina Pasco wamekuwa wakisema hakuna haja ya uchaguzi bali Maghufuli kisha amkabidhi Makonda.