kiwalanikwagude
Member
- Jun 8, 2011
- 52
- 19
NIMEFURAHISHWA SANA NA KITENDO CHA MWANA JF KUHOJI KUHUSU KUONDOKA KWA MWANDISHI EZEKIEL KAMWAGA WA MWANAHALISI, INGAWAJE NIKO NJE YA NCHI NAOMBA NIWAONJESHE KIDOGO KUHUSU HUYU KAMWAGA ALIVYOANZA KUTUMIWA NA CCM NILIWAHI KUTUMIWA MAKALA HII NA RAFIKI YANGU AMBAYE YUKO TANZANIA ALIANDIKA MAKALA KWENDA MWANAHALISI LAKINI HAIKUCHAPWA, SASA KUBENEA ATWAMBIE KWANINI HAKUCHAPA MAKALA HII? NA EZEKIEL KAMWAGA YUPO SIMBA SASA HATUTAMWONA TENA MWANAHALISI!
EZEKIEL KAMWAGA MWANAHALISI SIO UWANJA WA POROJO NA PROPAGANDA
Katika gazeti la Mwanahalisi la jumatano,Machi30-Aprili5,2011 mwandishi Ezekiel Kamwaga aliandika makala yenye kichwa cha habari Msilale, CCM hawajaanza kugombana leo, nimeisoma mara tano makala hii ila nimeshindwa kuelewa iwapo makala hii kweli ilipaswa ichapwe kwenye gazeti la Mwanahalisi au Rai la Rostam Aziz?
Makala hiyo ya Ezekiel Kamwaga imetushangaza watu wengi hasa kwa jinsi ilivyoshindwa kuzama kwenye hoja za msingi kwanini CCM sasa inayumba kuliko wakati wowote katika historia ya chama hiko? Mimi nilitegemea Kamwaga atwambie kiundani je CCM ilipokumbwa na migogoro ilikuwa chini ya uwenyekiti wa nani? Chukulia mfano wa vuta nikuvute ya Nyerere na Kambona au kina Kassela Bantu, ikumbukwe kuwa wakati ule CCM ilikuwa chini ya Mwalimu Nyerere na hata ulimwengu mzima unamfahamu Nyerere ni nani katika unguli wa siasa za Afrika. Sasa Kamwaga anapodai tena kwa maneno rahisi tu kuwa kwa vile kipindi kile CCM au TANU ilipita salama basi hata awamu hii itapita salama! Hapa anatudanganya kwa maana anataka kumlinganisha Nyerere na Kikwete kiuongozi kitu aambacho hakiwezi kutuingia akilini hata kidogo.
Labda tuchukulie mfano rahisi tu utamlinganisha vipi Kikwete ambaye anadanganywa kila siku kiasi cha watu kumchakachulia mafuta ya gari na Nyerere ambaye hakutaka mzaha hata kidogo? Hapa ni dhahiri kuwa Nyerere na Kikwete hawana kinachowakutanisha kiuongozi hata kimoja kama Nyerere ni 70 basi Kikwete ni hasi (-)70 na hapa Kamwaga anapaswa kutambua kuwa uongozi huo uwe wa kitaifa au chama cha CCM.
Historia ipo wazi kuwa Kikwete hajapitia shida, hajui changamoto zozote ndio maana hata zinapoibuka hawezi kuzitatua, ndio maana kwa udhaifu wake huo ameshindwa kujipambanua yuko kwa wapinga ufisadi kina Mwakyembe na Sitta au kwa Lowassa na Rostam Aziz, huyu ndio Kikwete ambaye CCM inazidi kumfia mikononi mwake, huyu ndiyo Jakaya Kikwete aliyeshindwa kufanya kampeni kwa kutumia makada wa CCM badala yake akafannya kampeni za BMW yaani Baba, Mama na Watoto, au basi Kamwaga anataka kutuchekesha kwa kulinganisha uongozi wa Philipo Mangula na Makamba.
Lakini kuna la zaidi katika makala ile ya Ezekiel Kamwaga ambayo nathubutu kuiita ni ya kipuuzi tu kwa maana inaonyesha jinsi gani mwandishi anatoa hoja mfu ambazo hata kama kuna ufufuko siku ya mwisho basi haziwezi kufufuka, lakini mimi kama mtu mwenye uzoefu na wanahabari wa taifa hili ambao ninawafahamu vizuri halafu na uzoefu na watu wa propaganda wa CCM na michezo yao michafu huku wakijijigamba kuwa hakuna chombo cha habari Tanzania kisichokuwa na bei kwa maana kuwa wanaweza kumhonga mwandishi huyu au yule nitumie fursa hii kuweka wazi kuwa Ezekiel Kamwaga ameingia kwenye mtego huu na yeye amenaswa sasa sijui kwa shilingi ngapi? Kwa maana kwa mwandishi kijana wa aina yake nilimtegemea hata kama kweli analenga kuandika makala ya mtindo ule basi angeandika hoja za msingi kuliko kujaza kurasa za gazeti kwa manenno ya kutumwa na Yusuph Makamba au Hizza Tambwe.
Jinsi makala ya Kamwaga ilivyokuwa ya kusifia uimara wa CCM ambao kiuhalisia kwa hivi sasa haupo tena mimi nilidhani iimeandikwa na Ridhiwan Kikwete au Miraj Kikwete au hata Mama Salma Kikwete ambao wanakila sababu ya kutetea hata yale yasiyokuwepo kwavile tu CCM ndio inawapa kula si baba yao Kikwete ndio mwenyekiti? Sasa yeye Kamwaga amepewa nini mpaka afanye kazi isiyomhusu?
Nichukue fursa hii pia kumkubusha kuwa anachofanya anajiharibia mwenyewe na katu hawezi kuliharibu Mwanahalisi kama ametumwa kufanya hivyo, watanzania wanafahamu kuwa Saed Kubenea ni mtetezi wao, wanajua kuwa kina Mwangulumbi, Mbaga, Assenga na Ndimara Tegambwage ni watu makini sana. Watanzania wanakumbuka kuwa umaarufu wa Mwanahalisi haujaja kwa kujipendekeza kwa CCM bali kwa jasho na damu ya Kubenea na Tegambwage ,nani asiyekumbuka jinsi wanaharakati hawa walivyopigwa mapanga na kumwagiwa tindikali? Hivyo anapotokea mpuuzi kama Ezekiel Kamwaga ambaye ametumwa na wapuuzi fulanifulani ambao ikibidi tutawataja wanaotaka kutuharibia gazeti hili sisi ni lazima tuseme kwa maana tunajua fika kuwa bila Mwanahalisi au Raia Mwema tusingekuwa hapa tulipo, tusingekuwa na uwezo wa kumhoji Rostam au Lowassa, mchango wa magazeti haya mawili ni mkubwa sana katika kuelekea mageuzi ya kweli nchini hivyo hatuwezi kufungia macho kadudumtu yoyote anayeleta porojo na propaganda chafu kwenye gazeti hili la Mwanahalisi mtetezi wa wanyonge wa taifa hili.
Kwanza kwa taarifa yake Kamwaga asidhani kuwa hao walioumtuma huwa hawasomi Mwanahalisi, aache upuuzi kwa taarifa yake kila jumatano Salva Rweyemamu lazima anunue gazeti la Mwanahalisi na Raia Mwema na ampelekee huyo Kikwete, amini usiamini hata Ridhiwan, Miraj, Salma, Makamba, Tambwe na wabunge wote wakitoa tamko tu lazima wakimbilie kuona waandishi makini wa Mwanahalisi na Raia Mwema wameandika au kuchambua vipi hicho walichozungumza na mara nyingi wamekuwa wakibadili mienendo yao kwa kweli Mwanahalisi sio chombo cha kubeza hapa hakuna porojo kuna uchambuzi , hakuna propaganda kuna habari za kitafiti sasa iweje Ezekiel Kamwaga afanyie kazi ya Hizza Tambwe kwenye gazeti hili? Haiwezekani!
Najua kwavile huyu Ezekiel Kamwaga ameshalambishwa asali ya pesa mpya za benki kuu ataibuka harakaharaka na kunijibu lakini hii haina maana kama atashindwa kuweka bayana kwanini ameanza kuandika makala zisizofanana na Mwanahalisi au zilizo chini ya kiwango tena hali hii imejitokeza ghafla? Najua haya hawezi kujibu kwasababu anaujua ukweli, labda mimi naona kuliko kulumbana na ukweli ninaomwambia ni bora akahama Mwanahalisi kisha aende Mtanzania, Uhuru au Mzalendo huko na imani kuwa atafanya kazi yake vizuri lakini sio humu, akifanyia humu hatutamvumilia kwa maana porojo na propaganda hazitakiwi humu Mwanahalisi.
Halikadhalika labda nimpe siri moja Ezekiel Kamwaga ambayo itamsaidia kama kweli anataka kufanikiwa huko kwenye jukwaa lake jipya la CCM , kwa kawaida ukiwa bongo lala kama wewe wa kusifia tu watakudharau huko CCM hata wenyewe sikuhizi wanataka watu wenye uwezo wa kuhoji na kutoa changamoto hivyo jijengee utamaduni wa kuwa huru kimawazo ndio watakuheshimu huko CCM vinginevyo kwa jinsi upeo wako na maandiko yako yalivyo ya kishabiki bila shaka na wewe utaonekana gamba tu halafu watakuvua kwasababu huna faida kwao.
Hivi wewe Kamwaga unadhani kwa mwendo unaokwenda nao utadumu humu Mwanahalisi? Au unadhani kina Saed Kubenea watakuvumilia kupotosha umma? Bila shaka haiwezekani tayari maandishi yameshaandikwa ukutani siku zako za kukaa humu Mwanahalisi zinahesabika, na hata wakikutetea hatutakubali tutahoji na ikibidi tutajitokeza waziwazi hata kwenye TV kama umoja wa wasomaji wa Mwanahalisi na kuweka wazi kuwa HATUKUTAKI!
Fanya toba , omba msamaha anza upya vinginevyo utaangamia kwenye anga la habari za kiuchambuzi, mwishowe nitoe angalizo kuwa uchambuzi wangu umetawaliwa na hoja hivyo hata ikibidi kujibiwa iwe kwa misingi ya hoja hivohivyo lakini pia wakati ukijiandaa kujibu tuhuma hizi Bwana Ezekiel Kamwaga kumbuka kuwa hoja sio wewe kutetea CCM bali ni kwanini unafanya kazi ya Hizza Tambwe na Yusuph Makamba kwenye gazeti makini la Mwanahalisi?....Tafakari!
Mwandishi wa makala haya ni Ilunga Msekela , ni msomaji mkererketwa wa Mwanahalisi, aliwahi kusoma chuo kikuu Makerere cha nchini Uganda na ni mwanahabari katika moja ya mshirika ya kimataifa nchini ,anapatikana kwa anwani ya barua pepe; mpambanaji@live.com
EZEKIEL KAMWAGA MWANAHALISI SIO UWANJA WA POROJO NA PROPAGANDA
Katika gazeti la Mwanahalisi la jumatano,Machi30-Aprili5,2011 mwandishi Ezekiel Kamwaga aliandika makala yenye kichwa cha habari Msilale, CCM hawajaanza kugombana leo, nimeisoma mara tano makala hii ila nimeshindwa kuelewa iwapo makala hii kweli ilipaswa ichapwe kwenye gazeti la Mwanahalisi au Rai la Rostam Aziz?
Makala hiyo ya Ezekiel Kamwaga imetushangaza watu wengi hasa kwa jinsi ilivyoshindwa kuzama kwenye hoja za msingi kwanini CCM sasa inayumba kuliko wakati wowote katika historia ya chama hiko? Mimi nilitegemea Kamwaga atwambie kiundani je CCM ilipokumbwa na migogoro ilikuwa chini ya uwenyekiti wa nani? Chukulia mfano wa vuta nikuvute ya Nyerere na Kambona au kina Kassela Bantu, ikumbukwe kuwa wakati ule CCM ilikuwa chini ya Mwalimu Nyerere na hata ulimwengu mzima unamfahamu Nyerere ni nani katika unguli wa siasa za Afrika. Sasa Kamwaga anapodai tena kwa maneno rahisi tu kuwa kwa vile kipindi kile CCM au TANU ilipita salama basi hata awamu hii itapita salama! Hapa anatudanganya kwa maana anataka kumlinganisha Nyerere na Kikwete kiuongozi kitu aambacho hakiwezi kutuingia akilini hata kidogo.
Labda tuchukulie mfano rahisi tu utamlinganisha vipi Kikwete ambaye anadanganywa kila siku kiasi cha watu kumchakachulia mafuta ya gari na Nyerere ambaye hakutaka mzaha hata kidogo? Hapa ni dhahiri kuwa Nyerere na Kikwete hawana kinachowakutanisha kiuongozi hata kimoja kama Nyerere ni 70 basi Kikwete ni hasi (-)70 na hapa Kamwaga anapaswa kutambua kuwa uongozi huo uwe wa kitaifa au chama cha CCM.
Historia ipo wazi kuwa Kikwete hajapitia shida, hajui changamoto zozote ndio maana hata zinapoibuka hawezi kuzitatua, ndio maana kwa udhaifu wake huo ameshindwa kujipambanua yuko kwa wapinga ufisadi kina Mwakyembe na Sitta au kwa Lowassa na Rostam Aziz, huyu ndio Kikwete ambaye CCM inazidi kumfia mikononi mwake, huyu ndiyo Jakaya Kikwete aliyeshindwa kufanya kampeni kwa kutumia makada wa CCM badala yake akafannya kampeni za BMW yaani Baba, Mama na Watoto, au basi Kamwaga anataka kutuchekesha kwa kulinganisha uongozi wa Philipo Mangula na Makamba.
Lakini kuna la zaidi katika makala ile ya Ezekiel Kamwaga ambayo nathubutu kuiita ni ya kipuuzi tu kwa maana inaonyesha jinsi gani mwandishi anatoa hoja mfu ambazo hata kama kuna ufufuko siku ya mwisho basi haziwezi kufufuka, lakini mimi kama mtu mwenye uzoefu na wanahabari wa taifa hili ambao ninawafahamu vizuri halafu na uzoefu na watu wa propaganda wa CCM na michezo yao michafu huku wakijijigamba kuwa hakuna chombo cha habari Tanzania kisichokuwa na bei kwa maana kuwa wanaweza kumhonga mwandishi huyu au yule nitumie fursa hii kuweka wazi kuwa Ezekiel Kamwaga ameingia kwenye mtego huu na yeye amenaswa sasa sijui kwa shilingi ngapi? Kwa maana kwa mwandishi kijana wa aina yake nilimtegemea hata kama kweli analenga kuandika makala ya mtindo ule basi angeandika hoja za msingi kuliko kujaza kurasa za gazeti kwa manenno ya kutumwa na Yusuph Makamba au Hizza Tambwe.
Jinsi makala ya Kamwaga ilivyokuwa ya kusifia uimara wa CCM ambao kiuhalisia kwa hivi sasa haupo tena mimi nilidhani iimeandikwa na Ridhiwan Kikwete au Miraj Kikwete au hata Mama Salma Kikwete ambao wanakila sababu ya kutetea hata yale yasiyokuwepo kwavile tu CCM ndio inawapa kula si baba yao Kikwete ndio mwenyekiti? Sasa yeye Kamwaga amepewa nini mpaka afanye kazi isiyomhusu?
Nichukue fursa hii pia kumkubusha kuwa anachofanya anajiharibia mwenyewe na katu hawezi kuliharibu Mwanahalisi kama ametumwa kufanya hivyo, watanzania wanafahamu kuwa Saed Kubenea ni mtetezi wao, wanajua kuwa kina Mwangulumbi, Mbaga, Assenga na Ndimara Tegambwage ni watu makini sana. Watanzania wanakumbuka kuwa umaarufu wa Mwanahalisi haujaja kwa kujipendekeza kwa CCM bali kwa jasho na damu ya Kubenea na Tegambwage ,nani asiyekumbuka jinsi wanaharakati hawa walivyopigwa mapanga na kumwagiwa tindikali? Hivyo anapotokea mpuuzi kama Ezekiel Kamwaga ambaye ametumwa na wapuuzi fulanifulani ambao ikibidi tutawataja wanaotaka kutuharibia gazeti hili sisi ni lazima tuseme kwa maana tunajua fika kuwa bila Mwanahalisi au Raia Mwema tusingekuwa hapa tulipo, tusingekuwa na uwezo wa kumhoji Rostam au Lowassa, mchango wa magazeti haya mawili ni mkubwa sana katika kuelekea mageuzi ya kweli nchini hivyo hatuwezi kufungia macho kadudumtu yoyote anayeleta porojo na propaganda chafu kwenye gazeti hili la Mwanahalisi mtetezi wa wanyonge wa taifa hili.
Kwanza kwa taarifa yake Kamwaga asidhani kuwa hao walioumtuma huwa hawasomi Mwanahalisi, aache upuuzi kwa taarifa yake kila jumatano Salva Rweyemamu lazima anunue gazeti la Mwanahalisi na Raia Mwema na ampelekee huyo Kikwete, amini usiamini hata Ridhiwan, Miraj, Salma, Makamba, Tambwe na wabunge wote wakitoa tamko tu lazima wakimbilie kuona waandishi makini wa Mwanahalisi na Raia Mwema wameandika au kuchambua vipi hicho walichozungumza na mara nyingi wamekuwa wakibadili mienendo yao kwa kweli Mwanahalisi sio chombo cha kubeza hapa hakuna porojo kuna uchambuzi , hakuna propaganda kuna habari za kitafiti sasa iweje Ezekiel Kamwaga afanyie kazi ya Hizza Tambwe kwenye gazeti hili? Haiwezekani!
Najua kwavile huyu Ezekiel Kamwaga ameshalambishwa asali ya pesa mpya za benki kuu ataibuka harakaharaka na kunijibu lakini hii haina maana kama atashindwa kuweka bayana kwanini ameanza kuandika makala zisizofanana na Mwanahalisi au zilizo chini ya kiwango tena hali hii imejitokeza ghafla? Najua haya hawezi kujibu kwasababu anaujua ukweli, labda mimi naona kuliko kulumbana na ukweli ninaomwambia ni bora akahama Mwanahalisi kisha aende Mtanzania, Uhuru au Mzalendo huko na imani kuwa atafanya kazi yake vizuri lakini sio humu, akifanyia humu hatutamvumilia kwa maana porojo na propaganda hazitakiwi humu Mwanahalisi.
Halikadhalika labda nimpe siri moja Ezekiel Kamwaga ambayo itamsaidia kama kweli anataka kufanikiwa huko kwenye jukwaa lake jipya la CCM , kwa kawaida ukiwa bongo lala kama wewe wa kusifia tu watakudharau huko CCM hata wenyewe sikuhizi wanataka watu wenye uwezo wa kuhoji na kutoa changamoto hivyo jijengee utamaduni wa kuwa huru kimawazo ndio watakuheshimu huko CCM vinginevyo kwa jinsi upeo wako na maandiko yako yalivyo ya kishabiki bila shaka na wewe utaonekana gamba tu halafu watakuvua kwasababu huna faida kwao.
Hivi wewe Kamwaga unadhani kwa mwendo unaokwenda nao utadumu humu Mwanahalisi? Au unadhani kina Saed Kubenea watakuvumilia kupotosha umma? Bila shaka haiwezekani tayari maandishi yameshaandikwa ukutani siku zako za kukaa humu Mwanahalisi zinahesabika, na hata wakikutetea hatutakubali tutahoji na ikibidi tutajitokeza waziwazi hata kwenye TV kama umoja wa wasomaji wa Mwanahalisi na kuweka wazi kuwa HATUKUTAKI!
Fanya toba , omba msamaha anza upya vinginevyo utaangamia kwenye anga la habari za kiuchambuzi, mwishowe nitoe angalizo kuwa uchambuzi wangu umetawaliwa na hoja hivyo hata ikibidi kujibiwa iwe kwa misingi ya hoja hivohivyo lakini pia wakati ukijiandaa kujibu tuhuma hizi Bwana Ezekiel Kamwaga kumbuka kuwa hoja sio wewe kutetea CCM bali ni kwanini unafanya kazi ya Hizza Tambwe na Yusuph Makamba kwenye gazeti makini la Mwanahalisi?....Tafakari!
Mwandishi wa makala haya ni Ilunga Msekela , ni msomaji mkererketwa wa Mwanahalisi, aliwahi kusoma chuo kikuu Makerere cha nchini Uganda na ni mwanahabari katika moja ya mshirika ya kimataifa nchini ,anapatikana kwa anwani ya barua pepe; mpambanaji@live.com