Kwanini ziitwe vita za Dunia wakati nchi za America ya Kusini hazikushiriki na zipo Duniani?

IKARAHANSI

JF-Expert Member
Jul 30, 2019
398
479
Wakuu habari ya muda huu, ni matumaini yangu kuwa mpo salama mkiendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa. Kwa wale wenye matatizo ya hapa na pale nawaombea kwa MUNGU awafanyie wepesi ili mfanikiwe kwa usalama. Tuje kwenye hoja.

Tuliopita shuleni enzi hizo na tuliopo sasa, tumefundishwa kupitia hisitoria kuwa kuna vita nyingi sana zilipiganwa baina ya makabila, himaya, falme hadi na nchi moja dhidi ya nyingine yote hiyo ilikuwa ni kugombea maslahi na mipaka ya utawala baina ya himaya moja na nyingine.

Moja wapo ya vita hizo kuna vita kubwa mbili ambazo zilijumuisha mataifa mengi ambazo ziliitwa vita za dunia (Vita ya kwanza ya dunia na vita ya pili ya dunia), vita za dunia zote mbili zilihusisha mataifa makubwa ya ulaya enzi hizo yaani Wajerumani na Waingereza pamoja na makoloni yao wakisaidiwa na baadhi ya mataifa ya America (USA) na Asia (Japan).

Binafsi nilipokuwa shule enzi hizo nilikubaliana kuwa kweli ilikuwa ni vita za dunia, lakini kadri ninapoendelea kukua na kutafakari naona kuwa tulidanganywa hakukuwahi kuwa na vita ya dunia. maana kama ingekuwa vita ya dunia basi mataifa yote yaliyopo Duniani yangeshiriki.

Swali langu ni je, Kwanini ziitwe vita za Dunia wakati nchi kama Brazil, Agentina, Paraguay, Colombia, Peru, Uruguay kwa ujumla America ya kusini hazikushiriki katika vita hizo na wakati zipo Duniani? Ukija kwa upande wa Asia sikuwahi kusikia China, Campodia au Iran zikitajwa katika vita hizo mbili za dunia.

karibuni kwa michango!!!
 
Ni sawa kabisa kuita vita hizo "vita ya dunia" maana zuligusa mabara yote.

Vita Kuu ya kwanza 1914 - 1918
1594979829629.png

Angalia nchi zilizoshiriki kwa namna fulani Vita Kuu ya Kwanza hadi 1918. Kibichi ni rangi ya "Mataifa ya Ushirikiano" (Allied, Uingereza, Ufaransa, Urusi, tangu 1917 pia Marekani n.k.), kichungwa ni "Mataifa ya Kati" (Central Powers, yaani Ujerumani, Austria-Hungaria, Milki ya Osmani (=Uturuki), Bulgaria. Pale juu Iran haina rangi lakini Warusi, Waingereza na Waosmani walipigana sana katika nchi ile.

Halafu
Vita kuu ya pili 1939 - 1945:
1594980290573.png

Hizi ni nchi zilizoshiriki kwa namna fulani katika Vita Kuu ya Pili.
Kichungwa ni Ujerumani, Italia (+koloni), na Japani na nchi ndogo za Ulaya upande wao (Ufini, Bulgaria, Romania, Hungaria) na Uthai pale Asia;
Kibichi cheusi ni nchi shiriki (pamoja na koloni) katika awamu la kwanza la vita dhidi yao, hasa Poland, Ufaransa, Uingereza, halafu tangu 1941 Urusi.
Kibichi cheupe ni mataifa yaliyoingia tangu Marekani kushambuliwa 1941, mengine yalifuata tu kwenye mwisho wa vita wakuitangaza vita dhidi ya Ujerumani bila kufanya kitu chochote (k.m. Uturuki, Argentina, Chile) kwa sababu walitaka kusimama upande wa washindi walioanza kuonekana tayari.

Hali halisi kwa ufahamu wangu vita ya kwanza inayostahili kuitwa "vita ya dunia" ilitokea tayari mwaka 1760, inayojulikana kama "Vita ya Miaka saba". Ilikuwa hasa vita ya nchi za Ulaya, lakini wakati ule ukoloni ulikuwa ukianza kwa hiyo Waingereza, Wahispania, Wareno na Wafaransa walipigana pia hasa Amerika ya Kaskazini na Uhindini, lakini pia kote baharini na kwenye koloni za Amerika kusini.

Angalia ramani: Vita ya Miaka Saba 1756 -1763
1594981193973.png

Buluu: Maeneo chini ya Uingereza, Prussia na Ureno
Kibichi: Maeneo chini ya Ufaransa, Urusi, Hispania, Austria, Uswidi (pamoja nchi ndogo za Ulaya)
 
Ni sawa kabisa kuita vita hizo "vita ya dunia" maana zuligusa mabara yote.

Vita Kuu ya kwanza
View attachment 1509295
Angalia nchi zilizoshiriki kwa namna fulani Vita Kuu ya Kwanza hadi 1918. Kibichi ni rangi ya "Mataifa ya Ushirikiano" (Allied, Uingereza, Ufaransa, Urusi, tangu 1917 pia Marekani n.k.), kichungwa ni "Mataifa ya Kati" (Central Powers, yaani Ujerumani, Austria-Hungaria, Milki ya Osmani (=Uturuki), Bulgaria. Pale juu Iran haina rangi lakini Warusi, Waingereza na Waosmani walipigana sana katika nchi ile.

Halafu
Vita kuu ya pili:
View attachment 1509301
Hizi ni nchi zilizoshiriki kwa namna fulani katika Vita Kuu ya Pili.
Kichungwa ni Ujerumani, Italia (+koloni), na Japani na nchi ndogo za Ulaya upande wao (Ufini, Bulgaria, Romania, Hungaria) na Uthai pale Asia;
Kibichi cheusi ni nchi shiriki (pamoja na koloni) katika awamu la kwanza la vita dhidi yao, hasa Poland, Ufaransa, Uingereza, halafu tangu 1941 Urusi.
Kibichi cheupe ni mataifa yaliyoingia tangu Marekani kushambuliwa 1941, mengine yalifuata tu kwenye mwisho wa vita wakuitangaza vita dhidi ya Ujerumani bila kufanya kitu chochote (k.m. Uturuki, Argentina, Chile) kwa sababu walitaka kusimama upande wa washindi walioanza kuonekana tayari.

Hali halisi kwa ufahamu wangu vita ya kwanza inayostahili kuitwa "vita ya dunia" ilitokea tayari mwaka 1760, inayojulikana kama "Vita ya Miaka saba". Ilikuwa hasa vita ya nchi za Ulaya, lakini wakati ule ukoloni ulikuwa ukianza kwa hiyo Waingereza, Wahispania, Wareno na Wafaransa walipigana pia hasa Amerika ya Kaskazini na Uhindini, lakini pia kote baharini na kwenye koloni za Amerika kusini.

Angalia ramani: Vita ya Miaka Saba 1756 -1763
View attachment 1509311
Buluu: Maeneo chini ya Uingereza, Prussia na Ureno
Kibichi: Maeneo chini ya Ufaransa, Urusi, Hispania, Austria, Uswidi (pamoja nchi ndogo za Ulaya)
 
Ni sawa kabisa kuita vita hizo "vita ya dunia" maana zuligusa mabara yote.

Vita Kuu ya kwanza
View attachment 1509295
Angalia nchi zilizoshiriki kwa namna fulani Vita Kuu ya Kwanza hadi 1918. Kibichi ni rangi ya "Mataifa ya Ushirikiano" (Allied, Uingereza, Ufaransa, Urusi, tangu 1917 pia Marekani n.k.), kichungwa ni "Mataifa ya Kati" (Central Powers, yaani Ujerumani, Austria-Hungaria, Milki ya Osmani (=Uturuki), Bulgaria. Pale juu Iran haina rangi lakini Warusi, Waingereza na Waosmani walipigana sana katika nchi ile...

Nakuwa mgumu kuamini kuwa Brazil na mataifa mengine ya America ya kusini eti yalikuwa yakisubiri mshindi apatikane wasimame upande wake (kama nimekuelewa vizuri), ikiwa hivyo basi ni kuwa hawakushiriki bali walikuwa watazamaji na wasilikizaji.
 
Mkuu ukumbuke na great depression during and after war maana iyo ndo vita kuu ata kama huna silaha utakufa njaa tu.
 
Mkuu ukumbuke na great depression during and after war maana iyo ndo vita kuu ata kama huna silaha utakufa njaa tu.

Naomba kujua kuhusu hiyo "Great Depression" maana mimi ninazungumzia vita ya kutumia silaha na kumwaga damu, njaa ni kitu kingine japo nayo kuna wakati huchangiwa na vita.
 
Swali langu ni je, Kwanini ziitwe vita za Dunia wakati nchi kama Brazil, Agentina, Paraguay, Colombia, Peru, Uruguay kwa ujumla America ya kusini hazikushiriki katika vita hizo na wakati zipo Duniani? Ukija kwa upande wa Asia sikuwahi kusikia China, Campodia au Iran zikitajwa katika vita hizo mbili za dunia.

karibuni kwa michango!!!
Ni kweli vita ya kwanza na pili ya dunia havikupiganwa na kila nchi, isipokuwa ni kwamba kila vita kwa nafasi yake iliweka record ambazo hazikuwahi na hazijawahi kuwekwa na vita nyingine yoyote, hivyo kuzifanya vita hizi ziitwe hivyo

Baadhi ya record hizo ni:
1. Eneo: kila bara lilishiriki vita hizi mbili (ulaya, Asia, America, Afrika etc ukiondoa Antaktika) Bahari zote kuu pia zilikua battlefields
2. Idadi ya askari walioshiriki ni kubwa zaidi ukilinganisha na vita nyingine yoyote (60 million ww1, zaidi ya 70m ww2 walitoka kila pande ya dunia, kila bara)
3. Teknolojia ya vita ilikuwa ya kipekee mf. Matumizi ya chemical weapons na mahandaki kwa mara ya kwanza (ww1) huku bomu pekee la nyuklia likitumkka ww2
4. Madhara i.e vifo vingi zaidi, uharibifu wa kipekee (mfano Hiroshima)

Kiufupi kila nchi iliathiriwa na vita hizi na pia ilishiriki kwa namna yake. Mfano mzuri kwetu ni Msumbiji (Mozambique) wakati wa WW1 ilikuwa "neutral" lakini iligeuka kuwa uwanja wa mapambano baina ya wajerumani dhidi ya waingereza na washirika wao
 
Ni kweli vita ya kwanza na pili ya dunia havikupiganwa na kila nchi, isipokuwa ni kwamba kila vita kwa nafasi yake iliweka record ambazo hazikuwahi na hazijawahi kuwekwa na vita nyingine yoyote, hivyo kuzifanya vita hizi ziitwe hivyo

Baadhi ya record hizo ni:
1. Eneo: kila bara lilishiriki vita hizi mbili (ulaya, Asia, America, Afrika etc ukiondoa Antaktika) Bahari zote kuu pia zilikua battlefields.
2. Idadi ya askari walioshiriki ni kubwa zaidi ukilinganisha na vita nyingine yoyote (60 million ww1, zaidi ya 70m ww2 walitoka kila pande ya dunia, kila bara)
3. Teknolojia ya vita ilikuwa ya kipekee mf. Matumizi ya chemical weapons na mahandaki kwa mara ya kwanza (ww1) huku bomu pekee la nyuklia likitumkka ww2
4. Madhara i.e vifo vingi zaidi, uharibifu wa kipekee (mfano Hiroshima)

Kiufupi kila nchi iliathiriwa na vita hizi na pia ilishiriki kwa namna yake. Mfano mzuri kwetu ni Msumbiji (Mozambique) wakati wa WW1 ilikuwa "neutral" lakini iligeuka kuwa uwanja wa mapambano baina ya wajerumani dhidi ya waingereza na washirika wao

Umetaja kuwa kila bara lilishiriki vita hivyo na kuorodhesha mabara yote ukaacha America ya Kusini (huu ni ushahidi kuwa bara hilo halikushiriki) kwa upande wa Africa sikukatalii kwa maana tulikuwa chini yao hivyo hatukuwa na ujanja.

Hivyo hoja yangu ya kuonyesha kuwa vita hiyo haikuwa ya Dunia bado ina mashiko. mengine ni propaganda za wazungu.
 
Umetaja kuwa kila bara lilishiriki vita hivyo na kuorodhesha mabara yote ukaacha America ya Kusini (huu ni ushahidi kuwa bara hilo halikushiriki) kwa upande wa Africa sikukatalii kwa maana tulikuwa chini yao hivyo hatukuwa na ujanja.

Hivyo hoja yangu ya kuonyesha kuwa vita hiyo haikuwa ya Dunia bado ina mashiko. mengine ni propaganda za wazungu.
Sio kweli

Brazil ambayo ni Latin America iliingia vitani rasmi 26 April 1917 kidha nchi nyingine kama Guatemala, Haiti, Panama n.k zikafuata. Jaribu kufukua historia utathibitisha
 
Sio kweli

Brazil ambayo ni Latin America iliingia vitani rasmi 26 April 1917 kidha nchi nyingine kama Guatemala, Haiti, Panama n.k zikafuata. Jaribu kufukua historia utathibitisha
Acha kukariri na kujenga hoja zisizo na kichwa

Unavyosikia imeitwa vita ya dunia ni kwa sababu ya eneo, idadi ya askari, na teknology iliyotumika

Kiufupi ni hivyo,

LKN ukipiga eti kwa sababu Kuna vinchi havikushiriki hapo utaonekama mweupe sanaaa

Mfano, tanzania tulivyopigana na Uganda tulipigana watz wote?

AU vita ilipiganwa tz mzima?.
Jibu ni hapana

LKN ht hiyo Germany nayo haikupiganwa nchi nzima, Bali kweny baadhi ya maeneo tuh,

Bado hoja yako ni dhaifu sana mbele ya wanahistiry

Na hapo nimekuonesha kiufupi kwa uhalisia wa kawaida, sijakupeleka kule kweny fact zenyewe
 
Acha kukariri na kujenga hoja zisizo na kichwa

Unavyosikia imeitwa vita ya dunia ni kwa sababu ya eneo, idadi ya askari, na teknology iliyotumika

Kiufupi ni hivyo,

LKN ukipiga eti kwa sababu Kuna vinchi havikushiriki hapo utaonekama mweupe sanaaa

Mfano, tanzania tulivyopigana na Uganda tulipigana watz wote?

AU vita ilipiganwa tz mzima?.
Jibu ni hapana

LKN ht hiyo Germany nayo haikupiganwa nchi nzima, Bali kweny baadhi ya maeneo tuh,

Bado hoja yako ni dhaifu sana mbele ya wanahistiry

Na hapo nimekuonesha kiufupi kwa uhalisia wa kawaida, sijakupeleka kule kweny fact zenyewe
Ndo unaamka nini? Kwahiyo ulivyosoma umeona hoja yangu nyeupe?? Una fact gani mpya hapo ambayo sijaisema? Waafrika tuna matatizo.

Fuatilia thread kuanzia juu, unachochangia ndo nilichosema, sasa hizo kashfa zote za nini? Haya nipe hizo deep facts nisizozijua. Mijitu mingine sifuri kabisa
 
Acha kukariri na kujenga hoja zisizo na kichwa

Unavyosikia imeitwa vita ya dunia ni kwa sababu ya eneo, idadi ya askari, na teknology iliyotumika

Kiufupi ni hivyo,

LKN ukipiga eti kwa sababu Kuna vinchi havikushiriki hapo utaonekama mweupe sanaaa

Mfano, tanzania tulivyopigana na Uganda tulipigana watz wote?

AU vita ilipiganwa tz mzima?.
Jibu ni hapana

LKN ht hiyo Germany nayo haikupiganwa nchi nzima, Bali kweny baadhi ya maeneo tuh,

Bado hoja yako ni dhaifu sana mbele ya wanahistiry

Na hapo nimekuonesha kiufupi kwa uhalisia wa kawaida, sijakupeleka kule kweny fact zenyewe

Naomba unipeleke kwenye fact (sijui ndiyo nini!!) zenyewe.
 
Nakuwa mgumu kuamini kuwa Brazil na mataifa mengine ya America ya kusini eti yalikuwa yakisubiri mshindi apatikane wasimame upande wake (kama nimekuelewa vizuri), ikiwa hivyo basi ni kuwa hawakushiriki bali walikuwa watazamaji na wasilikizaji.
Brazil nadhani walishiriki lakini sio kwenye combat, walishiriki kutoa vitu Kama vyakula, madawa na vifaa vingine kwenye nchi zilizokuwa zikipigana na Ujerumani na washirika wake
 
Umetaja kuwa kila bara lilishiriki vita hivyo na kuorodhesha mabara yote ukaacha America ya Kusini (huu ni ushahidi kuwa bara hilo halikushiriki) kwa upande wa Africa sikukatalii kwa maana tulikuwa chini yao hivyo hatukuwa na ujanja.

Hivyo hoja yangu ya kuonyesha kuwa vita hiyo haikuwa ya Dunia bado ina mashiko. mengine ni propaganda za wazungu.
Sio propaganda, Vita Kama ilihusisha robo tatu ya nchi zote Duniani na players wakubwa wote Duniani walishiriki hiyo Ni Vita ya Dunia
Kuna mdau kaelezea vizuri Sana hapo juu
 
Umetaja kuwa kila bara lilishiriki vita hivyo na kuorodhesha mabara yote ukaacha America ya Kusini (huu ni ushahidi kuwa bara hilo halikushiriki) kwa upande wa Africa sikukatalii kwa maana tulikuwa chini yao hivyo hatukuwa na ujanja.

Hivyo hoja yangu ya kuonyesha kuwa vita hiyo haikuwa ya Dunia bado ina mashiko. mengine ni propaganda za wazungu.
Brazil ipo America kusini, na ilishiriki vita.
 
The Brazilian Expeditionary Force kilikuwa ni kikosi cha kupigana.

Naomba uielezee vizuri hii kama hautojali, maana sioni kama maslahi yao yaliguswa, ukizingatia hawakuwa na koloni wala kutajwa kama zilivyotajwa Japan, Italy na wengineo.
 
Naomba uielezee vizuri hii kama hautojali, maana sioni kama maslahi yao yaliguswa, ukizingatia hawakuwa na koloni wala kutajwa kama zilivyotajwa Japan, Italy na wengineo.
Samahani sijaelewa.
Unamaanisha nini "maslahi yao" na "koloni"?
Kama hautojali tumia kiswahili kirahisi.
 
Samahani sijaelewa.
Unamaanisha nini "maslahi yao" na "koloni"?
Kama hautojali tumia kiswahili kirahisi.

Mheshimiwa mbona nimetumia kiswahili chepesi au ni vile wewe umezoea kingereza na kiswanglish!!?😁😁
Maslahi = Mambo au utaratibu unayoiletea faida za kiuchumi nchi au kikundi fulani cha watu au mtu mmoja-mmoja. Mfano China wana maslahi kwetu kwa kuwa sisi ni soko la bidhaa zao.
Koloni au Makoloni = Nchi zilizotawaliwa na nchi nyingine mfano Kenya ilikuwa koloni la Mwingereza, Brazil ilikuwa koloni la Ureno.
 
Back
Top Bottom