Kwanini WhatsApp group mwisho washiriki 256?

shirima Mathias

JF-Expert Member
Feb 9, 2017
451
1,319
WhatsApp wameweka kiwangao cha washiriki (Group member) kuwa ni 256.
Ni nini siri ya hii number 256 kwa WhatsApp.
Yaani kwa nini 256 na sio 255,254 nk.

Najua wangeweka number yoyote pia ningehoji na hata sasa wakibadilisha na kuwa 556 bado pia nitahoji.
JF ya wabobezi mtusaidie kuna siri gani iliyo nyuma ya number hii ya 256?.

Najua hawakuiweka tu bali kuna kitu waliangalia
ℳ𝒶𝓈𝓉ℯ𝓇
 
namba yoyote 0-255 (inclusive) ina byte moja, byte moja siyo 256
Elimu ya kukariri ina madhara sana; kwa hiyo wewe huamini kuwa namba 0 inatumika katika kujaza idadi ya byte moja. Digital counting huanzia 0, wakati natural counting huanzaia 1; yaani hujui fact hiyo?

Kwenye binary counting ya byte, number zinaazia 0x00 ambayo ni natural 0 hadi 0xFF ambayo ni natural 255. Jumla kwenye byte hiyo zinakuwa ni 256 ambayo ndiyo Whatsupp wanatumia kuwa kila group lina ukubwa wa byte moja tu. Hawaangalii namba ya juu bali wanaangalia idadi ya namba zinazoweza kuwekwa kwenye hiyo byte moja. Member 0x00 (0) ni wa kwanza na member 0xFF(255) ni wa 256.
 
Elimu ya kukariri ina madhara sana; kwa hiyo wewe huamini kuwa namba 0 inatumika katika kujaza idadi ya byte moja. Digital counting huanzia 0, wakati natural counting huanzaia 1; yaani hujui fact hiyo?

Kwenye byte countig number zinaazia 0x00 ambayo ni natural 0 hadi 0xFF ambayo ni natural 255. Jumla kwenye byte hiyo zinakuwa ni 256 ambayo ndiyo Whatsupp wanatumia kuwa kila group ni byte moja tu. Hakuna member 0 hadi member 255 bali wao wanaangalia idadi ya halisi ya watu kwa kutumia natural counting
hoja yangu ipo hapa "256 ni idadi kwenye byte moja"
kubali umeteleza
 
hoja yangu ipo hapa "256 ni idadi kwenye byte moja"
kubali umeteleza
Pumba kabisa; hapo ndipo unapoonyesha mapungufu katika ufahamu wako, kwani unaonyesha kuwa hujui hujui kuwa memory capacity ya byte moja ni 2^8; unaangalia namba ya mwisho inayoweza kuwekwa kwenye memory hiyo tu bila kuangalia kuwa ni idadi gani ya namba zinazoweza kutunzwa katika memory hiyo.

Ngoja nikufundishe kidogo (no tuition fee of course). Ungekuwa ma nibble ya bit 4,ungeweza kuhifadhi na namba zifuatazo: 0000, 0001, 0010, 0011, 0100, 0101, 0110, 0111, 1000, 1001, 1010, 1011, 1100, 1101 ,1110 na 1111 ambazo ni 16 (yaani 2^4) ingawa namba kubwa ni binary 1111 ambayo ina represent 15! Kwa hiyo ukiwa na byte, utaweza kuhifadhi 2^8 ingawa namba ya mwisho ni 0xFF (au 11111111) ambayo ni decimal 255, lakini idadi ya namba zinazoweza kuwekwa kwenye byte hiyo ni 256 kuanzia 0 hadi 255. Kwenye binary counting kuna formula tatu unabidi uzijue vizuri na matumizi yake: (2^n), ((2^n)-1) na (2^(n-1)); zina matumizi tofauti. Wewe umekariri ile ya ((2^n)-1) tu na ndiyo maana unakwama kuelewa mjadala huu. Elimu ya bure hiyo! Shindwa mwenyewe kuielewa!
 
Naona guess work kibao. WhatsApp inatumia XMPP protocol ambayo haina limitations zote mnazodai.
Very likely sababu yao ikawa business driven kuliko technical. Kuna watu wanadai kuwa ukishafika limit ya 256 unaweza kuongeza member kwa invitation link. Kama ingekuwa ni techie issue isingewezekana.

Anyway usikute hamna hata mmoja aliye program XMPP hapa ila mnabishana as if ... :)
 
WhatsApp wameweka kiwangao cha washiriki (Group member) kuwa ni 256.
Ni nini siri ya hii number 256 kwa WhatsApp.
Yaani kwa nini 256 na sio 255,254 nk.

Najua wangeweka number yoyote pia ningehoji na hata sasa wakibadilisha na kuwa 556 bado pia nitahoji.
JF ya wabobezi mtusaidie kuna siri gani iliyo nyuma ya number hii ya 256?.

Najua hawakuiweka tu bali kuna kitu waliangalia
ℳ𝒶𝓈𝓉ℯ𝓇
Mkuu Ingia Google mara moja tu utapata jibu ... hizi sio zama za kusumbuliwa na swali kama hilo kwa mud9a mrefu ikiwa watu wameuchuna. Lakini in short ni sera yao tu... ni kama vile Instagram wanaruhusu video fupi fupi around 14 seconds mpaka recently wakaongeza option ya 'Continue watching ' au twitter ambao wanaruhusu jumbe fupi fupi around 144 characters tu ...

Lakini pia sababu nyingine inaweza kuwa strategy ya kuzua wide spread of fake news...
 
Kwa hiyo ipo siku wataweka 3^8 au haiwezekani
May be lakini basis ya hiyo 2, ni binary number system ambapo computer inafanyia kazi namba mbili tuuu yaani 0 na 1. Ambazo ndio zinaruhusu signals za umeme kusafirisha data kwenye mfumo wa computer. Hizo namba mbili ndio zinathibiti mtiririko wa data 0 inafanya geti lifungwe yaani power off na 1 inaruhusu geti kufunguliwa ili data zipite yaani power on ....
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom