Kwanini wazazi wanaosomesha watoto wao chuo wasilipe ada wao wenyewe kuliko kuwapatia watoto wao

blackcrow

Member
Sep 24, 2020
21
43
Kweli leo nimeamini maneno ya mwanamziki wa kizazi kipya BANDO MC kwamba "ata chuo kuna wajinga ndiyo maana kuna mtihani" ni sahihi kabisa. Wazazi wengi wakitanzania wanaosomesha watoto zao vyuo vikuu huwa wana mtindo wa kuwapa watoto zao pesa za ada wakalipe wao wenyewe. Kwa asilimia kubwa mimi naona wanakosea kwani asilimia nyingi ya watoto hupewa ada na wazazi wao na kufanyia mambo mengine. Japo siyo wote kwani tunatofautiana kimalezi lakini wengi huwa na tabia hiyo.

Hii inapelekea wanafunzi kulimbikiza deni la ada na pindi inapofika kipindi cha mtihani anakuwa na jukumu la kuitafuta ile ada ili aweze kufanya mtihani wa kumalizia chuo au kufunga muhula na kama atakosa kufanya mtihani itabidi arudie mwaka. Hatua hii hupelekea wanafunzi wengi kuuza vitu vyao vya thamani kwa gharama ya bei ya chini sana. Unaweza kukuta mwanafunzi alinunuliwa na baba yake PC ya laki 9 anakuja kuiuza laki 1 na nusu au laki 2 ili tuu alipe pesa ya ada aliyotumia. Siyo PC tuuu wengine huuza mpaka vitu vyote alivyonavyo mpaka nguo ili alipe deni la ada asije kukosa mtihani.

Sasa hiyo ni kwa watoto wa kiume vipi kuhusu hawa dada zetu. Kwao huwa ni hatari zaidi kwani wao huamini kuwa miili yao inatosha kabisa kuweza kumaliza tatizo hilo na ndiyo maana ukiingia mjini wanawake wengi wanaojiuza huwa wanafunzi wa chuo na huwa hawajali atatembea hata na lecture ili asije kukosa kufanya mtiani bila kujali kuwa kuna magonjwa.

Wazazi wanapaswa kulitathmini hili kweli unaweza kusema mwangu anajielewa lakini kumbuka mazingira pia humbadilisha mtu anaweza kufika chuo akakutana na mazingira tofauti mwishowe akabadilika kwani vishawishi pia chuo ni vingi.

Hivyo ni muhimu wazazi kwenda kulipa ada wao kama wao na kuwakabidhi watoto zao slip kuliko kumpa ada mtoto akalipe kama kweli unampenda na unataka amalize chuo kama alivyomaliza lasaba, form4, na form 6.

USHAURI WA BURE TUUU.
 
Makosa kusema mtu akifikisha miaka 18 no mtu mzima

Tuseme miaka 21 ndo mtu mzima..
Akifika umri huo ndo apige kura na achukuliwe kuwa ni mtu mzima
Chini ya hapo hata Ada asipewe mkononi
 
Mswahili akipata hua matak.o hulia mbwata...

Mtoto hajawahi shika pesa nyingi, anafika chuo anapewa pesa kibao za ada kwa nini asile...





Cc: mahondaw
 
Kuna watu mnaaandika kama hamjawai kufika chuo... chuo gani kikubalie Usome tu kabla hujamaliza ada.. yao ya muhala husika?
 
Mkuu unachosema ni kweli vyuoni hali ni tata kuna wanafunzi unaweza dhani ni yatima au wametelekezwa na wazazi kumbe ni tofauti kabisa na tatizo kubwa la wanafunzi wengi kuishi maisha ya kuigiza tofauti na uhalisia wao vijana wanataka waonekane kwa girls kwamba wapo vizuri ada wanatembea nazo kwenye wallet wao ni kununua nguo na perfume wanukie ili watoto wa kike wamuone yeye ndio yeye,pia watoto wakike alivyotoka uvinza mtoto wa watu kaingia dar baada ya kuijua mlimani city na Pizzahut,kidimbwi pia Tecno pop 2 aliyonunuliwa haitaki tena anataka iphone hapo hela ada anatumia mdogo mdogo na kuna baadhi ya vyuo kuna kitu inaitwa gatepass kama hujalipa ada hupiti getini na kipindi cha mitihani usisogee kabisa sasa hapo ndio balaa.Jambo la msingi watulize vichwa vyao wasome na waangalie hali za wazazi wao wengine tulikuwa class lakini mwisho wa mwezi salio linasoma na tulikuwa kawaida tu.
 
Back
Top Bottom