Quemu
JF-Expert Member
- Jun 27, 2007
- 984
- 128
Jana nilihudhuria mazishi ya binamu yangu wa karibu.
Binamu yangu huyu alilelewa na mama wakambo karibu maisha yake yote.
Kilichonishangaza na kunisikitisha ni kuona kuwa mama yake wakambo alivyowekwa kando wakati wa mazishi. Ninachomaanisha ni kuwa, wakati wa kumwaga udongo na kuweka mashada kaburini, waliitwa mume wa marehemu, baba mzazi na mama mzazi, wadogo wa marehemu, na mpaka shangazi na wajomba zake. Lakini mama wakambo akarukwa!!
Hivi ni katika hatua gani mchango wa wazazi wakambo katika malezi ya watoto huanza kuthaminiwa? Binamu yangu amelelewa na mama wakambo toka akiwa mdogo. Lakini leo hii amefariki, ndugu hawaoni umuhimu wa kumhusisha mama huyu kwenye matukio muhimu ya kumwaga udongo na kuweka mashada. Kulikuwa kuna ugumu gani kuwashirikisha wote mama mzazi na wakambo?
Au ni mpaka pale mama mzazi anapokuwa hayupo (amefariki, nk), ndipo mama wakambo anapopewa heshima yake?
Na kwenye shughul za harusi mambo yanakuwa hivi hivi....kama mama mzazi yu hai, basi mama wakambo hakai kwenye meza ya wazazi, hatambulishwi, halishwi keki, hanyweshwi shampeni????
Inasikitisha kuona kuwa mpaka leo hii bado tunaendelea kuwabeza wazazi wakambo
Binamu yangu huyu alilelewa na mama wakambo karibu maisha yake yote.
Kilichonishangaza na kunisikitisha ni kuona kuwa mama yake wakambo alivyowekwa kando wakati wa mazishi. Ninachomaanisha ni kuwa, wakati wa kumwaga udongo na kuweka mashada kaburini, waliitwa mume wa marehemu, baba mzazi na mama mzazi, wadogo wa marehemu, na mpaka shangazi na wajomba zake. Lakini mama wakambo akarukwa!!
Hivi ni katika hatua gani mchango wa wazazi wakambo katika malezi ya watoto huanza kuthaminiwa? Binamu yangu amelelewa na mama wakambo toka akiwa mdogo. Lakini leo hii amefariki, ndugu hawaoni umuhimu wa kumhusisha mama huyu kwenye matukio muhimu ya kumwaga udongo na kuweka mashada. Kulikuwa kuna ugumu gani kuwashirikisha wote mama mzazi na wakambo?
Au ni mpaka pale mama mzazi anapokuwa hayupo (amefariki, nk), ndipo mama wakambo anapopewa heshima yake?
Na kwenye shughul za harusi mambo yanakuwa hivi hivi....kama mama mzazi yu hai, basi mama wakambo hakai kwenye meza ya wazazi, hatambulishwi, halishwi keki, hanyweshwi shampeni????
Inasikitisha kuona kuwa mpaka leo hii bado tunaendelea kuwabeza wazazi wakambo