Vesuvius
JF-Expert Member
- Jun 27, 2021
- 1,550
- 2,783
Ni kama wamarekani weusi wasivyojiona waafrika tena. Ni athari za makovu ya utumwa ambayo hutweza asili na utu wa mtumwaKatika sehemu mbali mbali nimeona wazanzibar weusi na machotara wakikataa asili yao ya kutokea huku bara, sasa sijajua wanaukataa ukweli kwanini.
Hapo zamani wafanya biashara wa watumwa walifika visiwa vya zanzibar na kulikuwa na watu wenye asili ya kibantu wachache kwenye visiwa hivyo, hawa wafanya biashara wakaanza kuwatumia machifu na mamwinyi kuwauzia watumwa katika jamii zao na kisha kuwasafirisha kwenda nchi nyingine,
Kwa kuwa idadi yao ilikuwa ni ndogo, ikabidi wafanya biashara hao waje huku bara kutafuta soko jipya la kununua watumwa.
Sasa huku kwetu kulikuwa na makabila yalikuwa madogo ama hayana majeshi yenye nguvu, haya makabila mara nyingi yalikuwa yakipigwa basi mateka wa vita na wakimbizi waliokamatwa walikuwa wakiuzwa kwa wafanya biashara wa watumwa, Hata pale makabila makubwa yenye nguvu yalipopigana basi mateka na wakimbizi waliuzwa kwa wafanya biashara hawa.
Baada ya kuuzwa kwa wafanya biashara hawa, walisafirishwa kwenda zanzibar lilipokuwa soko mojawapo maarufu la watumwa walionunuliwa kwa bei ya juu na kupelekwa kufanya kazi amerika ya kusini, afrika ya kaskazini, n.k
Sasa kuna kipindi kilifika, kukawa na mashamba ya karafuu hapo zanzibar na ikaonekana ni vyema kutumia watumwa hao waliofika hapo zanzibar na kuwatumikisha katika mashamba badala ya kuwauza wote, Kwa hio baadhi wakifika zanzibar waliendelea kuuzwa kwenda nchi nyingine ila wengine walibaki katika mashamba ya karafuu.
Walikuwa ni ma elfu waliotumikishwa kwenye mashamba hayo, mazingira ya kazi yalikuwa magumu sana. Kazi zilifanywa kwa mijeredi, Watu walitukanwa, wengine kuuawa, wanawake walibakwa na kuzaa machotara, matibabu yalikuwa ya hali ya chini, n.k
Hata lugha zao asili walizotoka nazo huku , wengi wakaacha kutumia kabisa na kugeukia kiswahili na pia wengi waliacha kutumia majina yao ya ukoo waliyotoka nayo huku ikabidi waanza kutumia majina ya huko zanzibar, Wengi lugha yao ni kiswahili, lugha za kikabila ni shughuli pevu kuzikuta
Ni miaka mingi ilipita ya manyanyaso haya, ila kufikia mwisho ya miaka ya 1800, Muingereza alishinikiza kukoma kwa biashara hio haramu na hapa ndipo pakawa na nafuu,