Kwanini wa'Zanzibari tunalalamika kwamba Tanganyika inatudhulumu?

Bin Faza

JF-Expert Member
Jun 12, 2013
502
191
Wana Ukumbi,Kila mtanganyika anasikika akisema wazanzibari tunalalamika sana. Sijui ndio tunalalamika kweli au tunasema ukweli tu tu. Tanganyika ni ndugu zetu, tena ndugu wa kidamu, hili halifichiki. Lakini kuna baadhi ya mambo walioifanyia zanzibar yanakera sana na haya ndio yanayosema wao wakahisi tunalalamika.

1. Kusema uwongo kwamba waarabu walikuwa wakiwatesa waafrika, hii ni kampeni chafu zilizotoka tanganyika. Kumbe watanganyika walikuwa wakiheshimiwa na kupewa kazi za serikali kama raia wengine. Mfano ninazo hapa nyaraka za mishahara ya Ali Hassan Mwinyi na Aboud Jumbe walipokuwa wizara ya Elimi ya Dola ya Zanzibar. Hawa ni watanganyika

2. Kuanzisha siasa za machafuko zanzibar kuanzia 1957, na kufanya mauwazi ya wazanzibari wasio na hatia wapatao 17,000 kwa usiku mmoja. Mapinduzi ya zanzibar yalifanywa na watanganyika, tunao ushahidi kamili juu ya hili.

3. Kumuuwa Rais wa zanzibar, ijapokuwa wao ndio waliomweka kwa maslahi yao na kuuufanya muungano ni wa kudumu, kumbe muungano ulikuwa wa miaka 10 tu.

4. Kuzidi kuingilia siasa za zanzibar kwa kutumia kichaka cha CCM

5. Kutupora mali zetu zote, kutupora jina letu na kuifanya nchi yetu ni mkoa tu katika kichaka cha CCM.na mambo tani kwa tani wanayoifanyia znz yanawaudhi sana wazanzibari
 
Wana Ukumbi,Kila mtanganyika anasikika akisema wazanzibari tunalalamika sana. Sijui ndio tunalalamika kweli au tunasema ukweli tu tu. Tanganyika ni ndugu zetu, tena ndugu wa kidamu, hili halifichiki. Lakini kuna baadhi ya mambo walioifanyia zanzibar yanakera sana na haya ndio yanayosema wao wakahisi tunalalamika.1. Kusema uwongo kwamba waarabu walikuwa wakiwatesa waafrika, hii ni kampeni chafu zilizotoka tanganyika. Kumbe watanganyika walikuwa wakiheshimiwa na kupewa kazi za serikali kama raia wengine. Mfano ninazo hapa nyaraka za mishahara ya Ali Hassan Mwinyi na Aboud Jumbe walipokuwa wizara ya Elimi ya Dola ya Zanzibar. Hawa ni watanganyika2. Kuanzisha siasa za machafuko zanzibar kuanzia 1957, na kufanya mauwazi ya wazanzibari wasio na hatia wapatao 17,000 kwa usiku mmoja. Mapinduzi ya zanzibar yalifanywa na watanganyika, tunao ushahidi kamili juu ya hili.3. Kumuuwa Rais wa zanzibar, ijapokuwa wao ndio waliomweka kwa maslahi yao na kuuufanya muungano ni wa kudumu, kumbe muungano ulikuwa wa miaka 10 tu. 4. Kuzidi kuingilia siasa za zanzibar kwa kutumia kichaka cha CCM5. Kutupora mali zetu zote, kutupora jina letu na kuifanya nchi yetu ni mkoa tu katika kichaka cha CCM.na mambo tani kwa tani wanayoifanyia znz yanawaudhi sana wazanzibari

Ali Hassan Mwinyi na Abood Jumbe walikuwa watanganyika? kivipi?

Mnatakiwa kuichukia ccm na sio kuwachukia watanganyika
 
Likud,

Mimi siwachukii CCM wala siwachukii watanganyika. Mimi ni binadamu kama wao na siwezi kusema mimi ni bora zaidi au kujitia umbele wa aina yoyote kwani sote tutakufa na kwenda mbele ya haki kwa Allah SW.

Kwahivo usije ukadhani ninakuchukia wewe kwa sababu moja ua nyinge.

Ninachokisema ni kwamba chuki walioipandikiza dhidi ya zanzibar ilikuwa ni sumu kubwa na mbaya sana, leo bado sana.

Ali Hassan na Aboud Jumbe walikuwa katika lile kundi liitwalo WAZANZIBARA. Yaani watanganyika waliohamia zanizbar kwa muda mrefu. Fikra zao walipokuwa katika ASP zilikuwa against na znz kama walivokuwa watanganyika wengine, kama vile Nyerere.
 
Simbamzeewamwakidlila,

Pesa za akiba za zanzibar zilokuwa katika bank za nje, Nyerere alizifanyia mipango juu nchini mpaka zikaletwa BOT na ndio maasalama hadi leo.

Ukitaka zaidi sema
 
Waarabu hawakuwatesa waafrika....! Nadhani utakuwa unatoka kufufuka, una maruwe ruwe hata historia ya sultan huijui.
 
Can you please link this ---- to your other thread claiming ownership of 1000 acres of land in Morogoro! Toka umejoin JF kazi yako ni kulalamika tu.,hivi kuna Mtanganyika anauwezo wa kumiliki maeneo makubwa kama hayo huko nchini kwenu! Usiwatafutie watu Ban zisizo na ulazima
 
Wana Ukumbi,Kila mtanganyika anasikika akisema wazanzibari tunalalamika sana. Sijui ndio tunalalamika kweli au tunasema ukweli tu tu. Tanganyika ni ndugu zetu, tena ndugu wa kidamu, hili halifichiki. Lakini kuna baadhi ya mambo walioifanyia zanzibar yanakera sana na haya ndio yanayosema wao wakahisi tunalalamika.1. Kusema uwongo kwamba waarabu walikuwa wakiwatesa waafrika, hii ni kampeni chafu zilizotoka tanganyika. Kumbe watanganyika walikuwa wakiheshimiwa na kupewa kazi za serikali kama raia wengine. Mfano ninazo hapa nyaraka za mishahara ya Ali Hassan Mwinyi na Aboud Jumbe walipokuwa wizara ya Elimi ya Dola ya Zanzibar. Hawa ni watanganyika2. Kuanzisha siasa za machafuko zanzibar kuanzia 1957, na kufanya mauwazi ya wazanzibari wasio na hatia wapatao 17,000 kwa usiku mmoja. Mapinduzi ya zanzibar yalifanywa na watanganyika, tunao ushahidi kamili juu ya hili.3. Kumuuwa Rais wa zanzibar, ijapokuwa wao ndio waliomweka kwa maslahi yao na kuuufanya muungano ni wa kudumu, kumbe muungano ulikuwa wa miaka 10 tu. 4. Kuzidi kuingilia siasa za zanzibar kwa kutumia kichaka cha CCM5. Kutupora mali zetu zote, kutupora jina letu na kuifanya nchi yetu ni mkoa tu katika kichaka cha CCM.na mambo tani kwa tani wanayoifanyia znz yanawaudhi sana wazanzibari
Mimi nafikiri umekosa kitu cha kupost ukaona uanzishe hadithi uone itapokelewaje.Ukweli ni kuwa hakuna hadithi ya kweli,na ya kwako hailingani hata na ukweli!Hakikisha unasoma historia vzr na unakuwa na uelewa mpana wa mambo kabla hujaanzisha thread!
 
mimi siwachukii ccm wala siwachukii watanganyika. Mimi ni binadamu kama wao na siwezi kusema mimi ni bora zaidi au kujitia umbele wa aina yoyote kwani sote tutakufa na kwenda mbele ya haki kwa allah sw.

kwahivo usije ukadhani ninakuchukia wewe kwa sababu moja ua nyinge.

ninachokisema ni kwamba chuki walioipandikiza dhidi ya zanzibar ilikuwa ni sumu kubwa na mbaya sana, leo bado sana.

ali hassan na aboud jumbe walikuwa katika lile kundi liitwalo wazanzibara. Yaani watanganyika waliohamia zanizbar kwa muda mrefu. Fikra zao walipokuwa katika asp zilikuwa against na znz kama walivokuwa watanganyika wengine, kama vile nyerere.



mkuu mzanzibar halisi ni yupi..??

maana kuna wengine wanadai karume sio mzanzibari halisi sababu wazazi wake sijui wanatokea msumbiji kama sikosei... Maelezo haya nayapata kutoka mzalendo kule kwenye comments za watu!.. Sasa naomba unambie weye mzanzibari halisi ni yupi..?!!
 
Wana Ukumbi,Kila mtanganyika anasikika akisema wazanzibari tunalalamika sana. Sijui ndio tunalalamika kweli au tunasema ukweli tu tu. Tanganyika ni ndugu zetu, tena ndugu wa kidamu, hili halifichiki. Lakini kuna baadhi ya mambo walioifanyia zanzibar yanakera sana na haya ndio yanayosema wao wakahisi tunalalamika.1. Kusema uwongo kwamba waarabu walikuwa wakiwatesa waafrika, hii ni kampeni chafu zilizotoka tanganyika. Kumbe watanganyika walikuwa wakiheshimiwa na kupewa kazi za serikali kama raia wengine. Mfano ninazo hapa nyaraka za mishahara ya Ali Hassan Mwinyi na Aboud Jumbe walipokuwa wizara ya Elimi ya Dola ya Zanzibar. Hawa ni watanganyika2. Kuanzisha siasa za machafuko zanzibar kuanzia 1957, na kufanya mauwazi ya wazanzibari wasio na hatia wapatao 17,000 kwa usiku mmoja. Mapinduzi ya zanzibar yalifanywa na watanganyika, tunao ushahidi kamili juu ya hili.3. Kumuuwa Rais wa zanzibar, ijapokuwa wao ndio waliomweka kwa maslahi yao na kuuufanya muungano ni wa kudumu, kumbe muungano ulikuwa wa miaka 10 tu. 4. Kuzidi kuingilia siasa za zanzibar kwa kutumia kichaka cha CCM5. Kutupora mali zetu zote, kutupora jina letu na kuifanya nchi yetu ni mkoa tu katika kichaka cha CCM.na mambo tani kwa tani wanayoifanyia znz yanawaudhi sana wazanzibari

wale wazanzibari wenye asili ya Tanganyika/weusi mnauona mtego huo??msidhani mnagombea pamoja uhuru wa Zanzibar mkae mkijua mkishajitenga na Tanganyika mtaitwa nanyi ni wabara mrudi kwenu Tabora,umanyema na kilwa...in 1950's kulikuwa na kutokuelewana kati ya ASP na ZNP ikiwa na maana ASP waliitwa Wazenji wenye maslahi na wabara na ZNP wakiitwa wazenji wenye kufungamana na Oman na Sultani...naona wewe Bin Faza umerudisha historia kwa kuwabagua hao wazenji weusi kuwaita wabara hapo kwenye red...kila la kheri kupigania dola huru ya Zanzibar.
 



mkuu mzanzibar halisi ni yupi..??

maana kuna wengine wanadai karume sio mzanzibari halisi sababu wazazi wake sijui wanatokea msumbiji kama sikosei... Maelezo haya nayapata kutoka mzalendo kule kwenye comments za watu!.. Sasa naomba unambie weye mzanzibari halisi ni yupi..?!!
Ni yule ambaye angalau ana damu ya kiarabu!!!Utumwa mpaka wa fikra!!!
 
kwa mujibu wa katika ya zamani ya zanzibar mgeni anaeweza kupata uraia wa zanzibar ni mjukuu wa mgeni alofika na kuishi zanizbar. yaani kama wewe umehamia zanizbr basi uowe hapo na uzae na mtoto wako aowe hapo na azae huyo mjukuu wako ndie anayepata uraia wa moja kwa moja.

Mzee karume hakuzaliwa zanzibar, wengine wanasema ametokea Malawi. Allahuyalaam

Lakini kwa mujibu wa katika ya znz yeye hakustahiki urai wala watoto wake.
 
Cio akili yake mtoa mada amekariri alivyofundishwa

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sasa taratibu boss wangu

hebu jijibu swala lako mweyewe

yule Raj Kumar aliyeko tabora, mababu na mabii zake wamekwenda huko miaka 150 iliyopita. Wewe unamtambuwa kuwa ni nani? usipendelee na useme ukweli humwiti huyo Raj Kumar Muhindi?

nadhani nimekujibu swala lako
 
Sasa taratibu boss wangu

hebu jijibu swala lako mweyewe

yule Raj Kumar aliyeko tabora, mababu na mabii zake wamekwenda huko miaka 150 iliyopita. Wewe unamtambuwa kuwa ni nani? usipendelee na useme ukweli humwiti huyo Raj Kumar Muhindi?

nadhani nimekujibu swala lako

Nilikwambia mapema Bin faza,hakuna mdanganyika atakaeweza kukujibu hoja zako,kubwa utaambulia matusi na kejeli.
 
Bobwe

Nakubali maneno yako

hawa watanganyika ni maprofesa tai tu, kwengine kweupe.
 
kuna kosa gani na mimi kumiliki ardhi katika tanganyika

kwa taarifa yako bibi yangu anatoka kilwa kivinje

usione vibaya mimi kumiliki kama na wewe unataka kumuliki ardhi kama hiyo nitakupeleka kwa wanaohusika mhimu uweze kuilipia malipo madogo tu na kila mwaka uliilipie kodi, ukiifanyia kazi au ukiiwacha kama ulivoikuta
 
Mimi sikusoma historia ulioandikwa na wana watanganyika na waingereza sababu walidanganya kiyama.

Nitajie mwafrika mmoja tu aliyeteswa na mwarabu, ikiwa huna ni bora kwako ukikokoa uchafu katika akili yako.

Pia hayo usemayo wewe ndio yalokuwa mafunzoi wakipewa wanajesho wa tanganyika, yaani ni mafunzo ya TANU/ASP/CCM...uzushi mkubwa huo
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom