Kwanini watu wenye viherehere, wanaojiongeza nje ya majukumu yao na wanaongea kwa ujasiri hata kama ni uongo ni rahisi kufanikiwa?

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,571
15,321
Wakuu nimefanya utafii uchwara nimegundua

Watu wenye viherehere, wanaojiongeza nje ya majukumu yao, wanaoongea kwa ujasiri na kujiamini mambo ambayo hawayafahamu vizuri ni rahisi kufanikiwa.

Nimeona watu wa namba hii katika mazingira tofauti zaidi ya watu kumi.

USHAURI NINI UFANYE.

1:Usiwe na aibu za kijinga, jiongeze kuwa mwepesi wa kupata habari na taarifa sahihi zieleze kwa watu wenye ushawishi, Wenye vyeo, wenye pesa kwa ujasiri mkuu kana kwamba wewe ulikuwepo.

2: Usiwaamrishe wape kama mapendekezo nini kifanyike. Wakipata majanga na matatizo kuwa wa kwanza kuwapa pole, Shiriki katika mazishi, kuchimba makaburi, kubeba majeneza.

3: Kama unauweza pendeza sana unapokutana na watu wenye ushawishi. au unapotaka kufanikiwa katikati ya watu wa kawaida ili uaminike. Siku zote napanda mabus jamaa wanakusanya sadaka wa (wahubiri kwenye mabasi), Ila Juzi kapanda jamaa mmoja mchaga kapiga suti kali, kaongea kwa kujiamini sana kana kwamba hana shida, alipokusanya sadaka alikomba za kutosha basi zima.

4: Uwe makini katika kiherehere na kujiongeza usichongee watu au kuwasema vibaya sana maana unaweza kweli kufanikiwa lakn kwa Mta mfupi utafeli.

5: Ufurahie watu. Yaani ukikutana na mtu mfurahie mchangamkie kana kwamba mnamiaka mingi mnafahamiana japo hamjuani. Utakokota maelfu.

6: Ongea maneno yatamkike na kusikika kila herufi. Pia Ongea kwa mtazamo wa kutoa suluhisho hata kama ni la uongo.

7: Kuna watu wanaakili za kizamani eti kama ni Muhasibu basi hataki kujua kinachoendelea engineering, sheria, etc. utakufa Muhasibu. Ila sifa ya kiongozi ni kujua mambo hata kwa kupapasa kutoka katika almost kila tasnia. Mtu anayejiongeza nje ya eneo lake huaminiwa mapema kuwa kiongozi mahali popote.


hizi mbinu na za ziada ukijaribu huwezi kulala njaa...


ongeza na zako
 
Mfano mzuri ni DAB, anaongea upupu hadi unashindwa kumshangaa, sometimes akiongea uliyekaa kando ya TV unaona aibu but look where he is now, RC wa jimbo kubwa kuliko yote Yunani
hahaha
lazima uwe na PHD ya kula na vipofu.
uwe na controlled kiherehere na kimbelembele huku ukiwa na uwezo mkubwa wa kutatua matatizo bila kumkwaza aliye juu.

hii ni zaidi ya PHD 7 kichwani maana hata wenye PHD watakusujudia
 
wakuu nimefanya utafii uchwara nimegundua

Watu wenye viherehere, wanaojiongeza nje ya majukumu yao, wanaoongea kwa ujasiri na kujiamini mambo ambayo hawayafahamu vizuri ni rahisi kufanikiwa.

Nimeona watu wa namba hii katika mazingira tofauti zaidi ya watu kumi.

USHAURI NINI UFANYE.

1:Usiwe na aibu za kijinga, jiongeze kuwa mwepesi wa kupata habari na taarifa sahihi zieleze kwa watu wenye ushawishi, Wenye vyeo, wenye pesa kwa ujasiri mkuu kana kwamba wewe ulikuwepo.

2: Usiwaamrishe wape kama mapendekezo nini kifanyike. Wakipata majanga na matatizo kuwa wa kwanza kuwapa pole, Shiriki katika mazishi, kuchimba makaburi, kubeba majeneza.

3: Kama unauweza pendeza sana unapokutana na watu wenye ushawishi. au unapotaka kufanikiwa katikati ya watu wa kawaida ili uaminike. Siku zote napanda mabus jamaa wanakusanya sadaka wa (wahubiri kwenye mabasi), Ila Juzi kapanda jamaa mmoja mchaga kapiga suti kali, kaongea kwa kujiamini sana kana kwamba hana shida, alipokusanya sadaka alikomba za kutosha basi zima.

4: Uwe makini katika kiherehere na kujiongeza usichongee watu au kuwasema vibaya sana maana unaweza kweli kufanikiwa lakn kwa Mta mfupi utafeli.

5: Ufurahie watu. Yaani ukikutana na mtu mfurahie mchangamkie kana kwamba mnamiaka mingi mnafahamiana japo hamjuani. Utakokota maelfu.

6: Ongea maneno yatamkike na kusikika kila herufi. Pia Ongea kwa mtazamo wa kutoa suluhisho hata kama ni la uongo.

7: Kuna watu wanaakili za kizamani eti kama ni Muhasibu basi hataki kujua kinachoendelea engineering, sheria, etc. utakufa Muhasibu. Ila sifa ya kiongozi ni kujua mambo hata kwa kupapasa kutoka katika almost kila tasnia. Mtu anayejiongeza nje ya eneo lake huaminiwa mapema kuwa kiongozi mahali popote.


hizi mbinu na za ziada ukijaribu huwezi kulala njaa...


ongeza na zako
Dare-devils! Anayethubutu hufanikiwa. Anayethubutu ni jasiri wa kutafuta mali na ndiyo maana akaitwa mjasiriamali!
 
Katika kujiongeza kwao inawasaidia kujua mambo mengi zaidi tofauti na yule aliyestick tu kwenye ishu inayomhusu.
Pia watu wa hivi kuna namna wanakua wanajiamini sana na wanapenda kuthubutu so ni rahisi kufanikiwa.
 
Dare-devils! Anayethubutu hufanikiwa. Anayethubutu ni jasiri wa kutafuta mali na ndiyo maana akaitwa mjasiriamali!
Kweli mkuu.
Hii ndiyo elimu kuu ya kumsisitizia mtoto kabla hujamsisitizia kujua kuimba ABCD alafu akabaki teketeke.
ndivyo walivyofanya wafamle wa zamani walipowaandaa watoto wao kuwa watawala baadae.
 
Ongezea kwenye uzi wako mfano hai ni DAUD ALBERT BASHITE , huyu jamaa na maujinga yake na bado watu wanamuongelea na kumuombea mabaya lakini haki huyu jamaa anatoboa na kuishi vizuri sana duniani hapa, hatujui kwa muumba huko.
 
Ongezea kwenye uzi wako mfano hai ni DAUD ALBERT BASHITE , huyu jamaa na maujinga yake na bado watu wanamuongelea na kumuombea mabaya lakini haki huyu jamaa anatoboa na kuishi vizuri sana duniani hapa, hatujui kwa muumba huko.
😅😆 na jamaa anajiamin balaa
 
Safari ya mafanikio huwa ni ndefu, unakuta mtu Kasomea Computer Engineering lakini mafanikio anayapata katika kilimo..

Ila kiherehere si tabia nzuri...wenye viherehere mara nyingi wanaongea pumba nyingi mchele kiduchuu - hawana aibu ..wao ni kubwabwaja tu 80% upupu
 
Hata makazini wapo watu kama hao
HAHAHA
huko ndio kwenyewe mkuu.
Namkumbuka jamaa mmoja, baada tu ya kujua ABCD za kazi alijikuta ameshateka viongzoi wote.
Wanamuamini hata akiwa likizo anafanya kazi za watu ambao wapo kazini. Yaani kawapanga kukamini yeye ndiye anayejua kila kitu na anasiri za watu.
Aliingizwa Interview ya kupanda cheo na degree holders jamaa na form four yake kumbe alikuwa meshakula kontract kimyakimya interview ilikuwa zuga.

Ukikutana naye kukupa ofa, ukiugua wa kwanza kukuona, ukifiwa anatoa mchango kuliko wote, ukifiwa anaweza kulala kabisa kijijini kwenu. AnaPHD ya kutumia uongo kujinufaisha.

Yule jamaa telented hadi kesho huwa nampa saluti. Ukimpigia hta kama hamjaonana miaka sita anakumbuka majina ya watu wote, mitaa yote , story zote na kila kitu kilichokuwa kinafanyika.

Ila kiukweli Boss akiwa na kijana kama yule kazi karibu robo tatu zinaweza kufanywa na mtu mmoja. Anaumbea mwingi balaa, hakuna tukio asilolijua details zake, nyingine hata wahusika hawana. Muda wote simu iko active. Hata umuamshe saa ti usiku umpe kazi ya kufanya, ataamka akomae utadhani saa tatu asubuhi.


dunia inamambo
 
Unawezea kuwa mjasiriamali asiye na Kiherehere.

Sent using Jamii Forums mobile app
Bila kiherehere hata ujasiliamali unakuwa Butu.
Ila kiwe controlled kiherehere na kimbelembele.
Watu wanapenda kujaliwa, kufurahiwa, kuthaminiwa na kupewa kipaumbele hata kama hawasemi.
sasa ukijifanya unauchuna, hujiongezi wataenda wanapoweza kupata hizi ofa mkuu.


Kama huwezi inabidi ufeki hadi iwe automatic
 
Wakuu nimefanya utafii uchwara nimegundua

Watu wenye viherehere, wanaojiongeza nje ya majukumu yao, wanaoongea kwa ujasiri na kujiamini mambo ambayo hawayafahamu vizuri ni rahisi kufanikiwa.

Nimeona watu wa namba hii katika mazingira tofauti zaidi ya watu kumi.

USHAURI NINI UFANYE.

1:Usiwe na aibu za kijinga, jiongeze kuwa mwepesi wa kupata habari na taarifa sahihi zieleze kwa watu wenye ushawishi, Wenye vyeo, wenye pesa kwa ujasiri mkuu kana kwamba wewe ulikuwepo.

2: Usiwaamrishe wape kama mapendekezo nini kifanyike. Wakipata majanga na matatizo kuwa wa kwanza kuwapa pole, Shiriki katika mazishi, kuchimba makaburi, kubeba majeneza.

3: Kama unauweza pendeza sana unapokutana na watu wenye ushawishi. au unapotaka kufanikiwa katikati ya watu wa kawaida ili uaminike. Siku zote napanda mabus jamaa wanakusanya sadaka wa (wahubiri kwenye mabasi), Ila Juzi kapanda jamaa mmoja mchaga kapiga suti kali, kaongea kwa kujiamini sana kana kwamba hana shida, alipokusanya sadaka alikomba za kutosha basi zima.

4: Uwe makini katika kiherehere na kujiongeza usichongee watu au kuwasema vibaya sana maana unaweza kweli kufanikiwa lakn kwa Mta mfupi utafeli.

5: Ufurahie watu. Yaani ukikutana na mtu mfurahie mchangamkie kana kwamba mnamiaka mingi mnafahamiana japo hamjuani. Utakokota maelfu.

6: Ongea maneno yatamkike na kusikika kila herufi. Pia Ongea kwa mtazamo wa kutoa suluhisho hata kama ni la uongo.

7: Kuna watu wanaakili za kizamani eti kama ni Muhasibu basi hataki kujua kinachoendelea engineering, sheria, etc. utakufa Muhasibu. Ila sifa ya kiongozi ni kujua mambo hata kwa kupapasa kutoka katika almost kila tasnia. Mtu anayejiongeza nje ya eneo lake huaminiwa mapema kuwa kiongozi mahali popote.


hizi mbinu na za ziada ukijaribu huwezi kulala njaa...


ongeza na zako

Usilazimishe mtu awe na personality isiyo natural kwake

Kila mtu awe na personality yake,comfort yake ni next to none!

Wote wanafanikiwa labda muda tu

Trust me,watu wenye viherehere hawajafanikiwa kama unavyodai,wao wanajua kujionyesha kupita uwezo wao,ndio maana unaona kama wamefanikiwa sana

Halafu trust me,watu wenye viherehere na kujionesha sana huwa hawapendwi generally,michongo mingi hawapati wao kama tunavyodhani!
 
Back
Top Bottom