Kwanini watu wengi hasa wanawake hawapendi majina ya kibantu? Ubaya wake uko wapi?

ni kweli,japo kwa mchanganuo wangu wanawake wamezidi

Kinachotusumbua sana ni utumwa wa kiakili
Angalia hata namna ya uvaaji uongeaji n.k

Mtu akiongea na kuchanganya lugha fulani ndio anaonekana binadamu lakini akiongea na kuchanganya lugha zetu za kuzaliwa anaonekana kama nusu binadamu hivi

Aibu hii kwetu Waafika sijui itakwisha lini...!!!!!!
 
Nadhani tunatawaliwa na Mkoloni mpaka leo,majina ya Chausiku,Sikudhani,Mwanahawa,Manka,Koku,
Haika,Ghati,Bhoke yanafaa.
 
NIKIWA NIMETULIA LEO TAREHE 02/01/2014 wazo la matumizi ya majina linanijia wakati nafikiria niweke topiki ipi ya kwanza ndani ya mwaka huu.
ni mada nyingi zinakuja kichwani lakini nimeona ni muhimu leo tujadili matumizi ya majina kwa namna tofauti tofauti.

IMANI JUU YA MAJINA YA WATU
1.kuna majina yanahusishwa na upole
2.kuna majina yanahusishwa na uzuri
3.kuna majina yanahusishwa na ukarimu
4.kuna majina yanahusishwa ufalme/utawala
5.kuna majina yanahusishwa na umalaya
6.kuna majina yanahusishwa na ukatiri
7.kuna majina yanahusishwa na uchoyo nk nk


UKWELI NI KWAMBA MAJINA PIA YANA MAANA ZAKE
1.kuna majina yanamaana ya upendo
2.kuna majina yana maana ya uzuri
3.kuna majina yana maana ya upole
4.kuna majina yana maana ya unyenyekevu
5.kuna majina yana maana ya vitu mbalimbali kama wanyama,miti,miamba nk


UKWELI MWINGINE.
kila kabila lina majina yenye maana mbalimbali karibu kila kundi.


CHA KUSHANGAZA.
watu wengi hawapendi kutumia majina ya kibantu hata kama yana maana nzuri kuliko yale ya watu weupe wanayotumia.
na ni-ukweli usiopingika kuwa wanawake ndio wanaongoza kuchukia majina ya kibantu na huwa hawapendi kuyasema hadharani majina hayo na kuna wakati mwingine wanayakana ama kukataa kuwa wao hawana majina ya kienyeji pamoja na ukweli kwamba majina wanayo na walipewa toka utotoni.
KWA SAMPULI YA HARAKAHARAKA hata hapa MMU ugonjwa huu upo kwa kiasi kikubwa na ninaomba nitumie MMU kama sampuli ya harakaharaka kwa ninachokisema.


binafsi natumia jina la kibantu na ninalipenda,wengine humu ni kama Mwallu,manka nk hawa ni wachache naowajua hapa wanatumia majina ya kibantu katika lugha za kibantu,hata signature nyingi humu hazitumii lugha zetu hata ile ya taifa,tatizo ni nini?



mfano.
ningependa kuweka majina machache ya kisukuma na maana zake tuone kama yana ubaya wowote kiasi cha wasichana na hata wanaume kuyakataa ama kukataa kuyatumia,tena wakiyaona ni majina ya kishamba


1.Kwangu(limetokana na neno kwangulija)-maana yake ni mtoto wa mwisho
2.Njile(neno njile lina maana ya kwenda,jina hili hupewa msichana kama ikitokea watoto wote wanaozaliwa wanakufa bila kukua,na hivyo wakizaa tena,wazazi wakuwa wanajua na huyu atakufa na hivyo wanampa jina hili)-maana ni msichana aliyetegemewa hatakua bali atakufa kama ilivyo kwa watangulizi wake.
3.Geni(limetokana na neno bhugheni)-huyu alizaliwa wakati wazazi wake walienda ugenini
4.Nyanzala(limetokana na neno nzala-njaa)-huyu alizaliwa wakati wa njaa
5.Kashinje-huyu alizaliwa akiwa ametanguliza miguu badala ya kichwa.
6.mshinga-ni staili ya dansi kama zilivyo chalanga,ama ile ya diamondi na nyingine nyingi,ni staili katika ngoma za kisukuma.
7.Nsabi(limetokna na neno nsabhi-tajiri)-lina maana ya tajiri
8.Mwigulu(imetokana na neno ng'wigulhu)-lina maana ya mbingu
9.Kamwa(limetokana na neno kang'wa-limetokana na mnyama SUNGURA)-msichana mwenye akili/SUNGURA
10.Nungu(limetokana na na neno nhunghu likimaanisha chungu cha kupikia)-lina maana ya chungu


mfano wa majina ya weupe.
1.Doricus
2.Irene-amani
3.Elizabeth-Kiapo cha Mungu
4.Tabitha-gazelle-swara.
5.Chelsea-chungu(port)
KWA NINI WATU WENGI HAWAYAPENDI MAJINA YA KIBANTU? MFANO MTU AKIITWA TABITHA(swara) atapenda kuliko akiitwa KAN'GWA(sungura) ama MTU ANAONA BORA NA FAHARI KUTUMIA JINA CHELSEA(chungu-port) kuliko kutumia Nungu(chungu-port)

kwanza mbona hujatuambia la kwako? Pili mbona shule ulikuwa unatumia beatus dominic na dada yako mkampa mary? Mbona yule mtoto wako umemwita carlos?
 
kwanza mbona hujatuambia la kwako? Pili mbona shule ulikuwa unatumia beatus dominic na dada yako mkampa mary? Mbona yule mtoto wako umemwita carlos?
jina langu hilihili hapa kwenye id. na nimeeleza maana ya mshinga hapo kwenye mada
alafu wewe unajidai kunifahamu. yote uloyoandika hayanihusu iwe jina ama shule amamajina ya dada zangu
hata kubahatisha hutaweza. majina wanayo yote ya kidini na ya kikabila na wanayatumia kama mimi
 
Wengi wanapenda kuitwaa Albet au Fredi kuliko Masanja au Sundi
 
jina langu la asili lina maana ya honey! asali- japo ni la kiume!

iam so sweet indeed! na hilo ndilo lililoko kwenye vyeti kuanzia chekechea mpaka cheti cha masters..!

proud to be born a kurya!!!

Dah! Hatariiii! Kwa lugha yetu asali tunaita ' UCHI' hahaha! Happy new year UCHI
 
Nainkwa, Nakaniwa, Nasembiwa, Nasemba, Nashumbwe, Natujwa, Nafwiwa, Nakadori, Na.....!lol..majina mengine....
Hata mnipige mawe baby wangu nitamwita Paris...
Mbona leo hatuabudu mawe, jua, miti mikubwa...?
 
Sisi waafrika hasa watanzania tunapenda sana kuiga vitu vya wazungu hata kama hatujui maana yake nini. Na kwa bahati mbaya sana tunaiga na kupitiliza kuliko hata hao tunaocopy kutoka kwao. Mimi sidhani kwamba ukoloni peke yake ndio ulioleta hii kasumba ya kupenda majina ya kizungu hata kama hatujui maan ya hayo majina bali pia kutothmini ila nadesturi zetu na kufagilia za nje. Si tk majina tu bali karibia kila kitu tunashobokea hata uchafu unaofanywa na wazungu. Hatjiamini na asili yetu na bahati mbaya sana hata serkali zetu hazikutilia mkazo kwenye suala la majina ya saili ndiyo maana tumefika hapa tulipo leo!

Kama kweli ni ukoloni ndio uliotufanya tuache majina yetu ya asili mbon nch kama za bara a asia kama CHINA, JAPANI, NCHI ZOTE ZA KIARABU watu wake wamedunmisha majina ya asili pamoja kwamba nao walitawaliwa na wakoloni? Hata baadhi ya nchi a Africa kama vile Africa ya Kusini na nchi za Afrika magharibi kam GHANA,NIGERIA na nchi nyingine za ukanda huo kwa kiasi ulani wanatumia majina yao ya asili? Hata nchi jirani kama Kenya na Uganda wanatuimia majina yao ya asili kwaasilimia kubwa ukilinganisha na Tanzania. Hivyo tatizo letu waafrika ni ulimbukeni wa kuiga na kuthamini vitu vya kizungu kiliko asili yetu tena tunaurahia kweli kweli!
 
msaada huanzia nyumbani!
Wewe hata usingetumia kiluga, ungejiita 'mlima' ingekua poa sana!
nilianza na neno mlima nikaambiwa kuna user anatumia ilo neno...nikatafufuta neno mlima kwa lugha yangu ya mama ikawa haina neno mbadala,,,nkaona haina kelele wacha niende kwenye lungha za kigeni.......
 
Back
Top Bottom