Kwanini Watanzania wengi hawajui/hawafanyi Biashara za Exportation kwenye mazao ya Kilimo?

Lasway.Jr

JF-Expert Member
Jul 25, 2015
230
402
Hebu kila mmoja atupe uzoefu wake kwenye biashara za exportation

Au useme ni sababu gani zinakufanya ushindwe kufanya exportation

Mimi nitaeleza kidogo:

Leo nimeona tujadili kidogo ni kwanini sisi watanzania tunalima na tuna Ardhi nzr sana lakini hatufanyi Biashara kubwa kwenye kilimo yaani exportation , badala yake wakenya ndio wanatupiga Mzinga na kumiliki Biashara hizi Je? Tulichelewa WAP? Au ni nini ambacho hatuji?

Nitaeleza kwa namna ambavyo nimefanya utafiti wangu na kugundua mambo kadhaaa:

Kwanza kabisa, watanzania wengi sio wakulima (we a not Farmers rather we are peasants) nikiwa na maanisha kuwa hakuna mtanzania au hata kama wapo ni wachache wanaoweza kulima kuanzia hekari 50+, 100+, 250+ kwa pamoja na kuzalisha bidhaa za kilimo , kwa hyo ni ngumu kufanya Biashara za exportation kwa sababu hatuna vigezo hivyo

Pili, tulio wengi tumekuwa nyuma sana kwenye matumizi ya teknolojia pamoja na matumizi ya utaalamu kwenye kilimo vitu vya msingi kama soil test, water test, farm planning, post harvesting handling, pack house, ware house management na vingine vingi watanzania wengi hatuvijui na hatuna elimu yake , nimeeleza baadhi ya hivi vitu kwa sababu ili uweze kufanya exportation kwa baadhi ya mazao lazima uwe na certificate za taasisi ya kimataifa ya GAP sasa hawa wana vigezo na masharti yao ambayo yanaendana na vitu nilivyotaja hapo juu

Nilipokuwa naendelea kufanya utafiti kuona nani ametuloga niligundua kuwa Tanzania hasa wakulima hatuna taarifa sahihi kwenye masoko ya bidhaa za kilimo na pia tumewekuwa watu wa njaa sana na kuuza mazao Yetu Mara tuu tunapovuna kwa kuona fursa ya sisi kuwa wavivu ndio maana wahindi na waarabu ndio nakumbana nao huko masokoni kwenye Biashara kubwa za exportation na wanapata faida kubwa sana sio sana tuu faida kubwa mno (mfano mzr ni kwenye korosho) miaka yote hawa jamaa walikuwa wanapata faida kubwa kiasi gani ? Kwa sababu wakulima wananunua korosho kwa shilingi 500-1500 kwa kilo na sasa korosho hyo hyo inauza 4000 kwa kilo na wananunua just imaging

Kwa ndugu zetu wakenya matajiri wengi ni wakulima lakini sio ajabu sana kwa Wakenya kutupiga vikumbo kwenye exportation kwa sababu settlers walioanza Kilimo Kenya miaka ya 1885+ mpaka Leo wapo so not bad because their trade back home ndio maana Kenyan wanaexport sana UK, lakini soko lao liko vizuri kwa sababu wana certificate za mashamba ambazo hutumika kufanya exportation iwe rahisi hasa kwenye mazao ya matunda na mboga mboga kwa hiyo wanachofanya wanakuja Tanzania wananunua mazao yetu then wanatumia certificate na label zao wanauza Ulaya

Nyingine ni kwamba Tanzania tuna viongozi wengi sana ambao sio wafanyabiasha na wengi ni maskini ndio maana wakienda ulaya wanarudi na laptop na camera na wanasahau kurudi na connection za Biashara, hata wasomi wengi wanaokwenda kusoma wanarudi bila connection yoyote kitu ambacho wakenya wakienda wanarudi na akili ya Biashara kubwa, nafurahia sasa vijana wetu walioenda kusoma China wa nafanya Biashara sasa na jambo jema

Ukitaka kuanza Biashara ya exportation kwa Tanzania anza na dry food na sio mboga mboga kwa sababu hizi zinahitaji regulations nyingi sana , but grain ziko vizuri sana, na pia ukitaka Biashara ya exportation ikae vizuri anza na zile nchi ndogo Scandinavian countries, Asian, etc Ulaya kuna milolongo mingi, mimi nimeanza kidogo na nitaleta mrejesho hapa mambo yakikaa vizuri.

Hebu kila mmoja atupe uzoefu wake kwenye Biashara za exportation

Au useme ni sababu gani zinakufanya ushindwe kufanya exportation

===

Baadhi ya michango...

Hallo i am a kenyan based in the European union, nitajitahidi kuandika na swahili ila munajua sisi wakenya swahili yetu ni ya kuomba maji na pia nafahamu nikiandika na english wemgi hapa hawataelewa, na sisemi hivyo kwa ubaya dada na kaka zangu wabongo na pia masemeji wangu maana nafikiri nitaoa huko kwenu, sasa tuingia kwa hii jambo la export, kweli vile huyu kaka amesema kuexport to european union kuna masariti magumu sana hata kenya iko muda walifunguwa kuexport hapa EU sababu ya kitu tunaita MLI, yaani ni chemicals ngapi ziko kwa hio tunda au mboga, na pia unahitaji hii kitu inaitwa GAP yaani hio inaoyesa vile mazao huaza toka mbegu mpaka inafika kuexport, kazi hio,

Kenya iko na ardhi dogo sana lakini inatengeneza billions of shillings kila mwaka na export of fresh produce, ila tz mko na ardhi tele rotuba nzuri lakini munatengeneza hela chache sana kutoka export of farm produce, WHY, kwanini, moja elimu ni changamoto huko bongo, 2 hamna viongozi ambao wanajali taifa lenu, 3 wakulima hawana hela na maarifa ya kisasa, kaa irragation, greenhouses , cold stroge facilities, sababu ni nyingi.tz ni taifa mungu aliibariki kabisa, lakini elimu na uongozi ndio changamoto. hebu fikiria tz ndio wenye mifugo mingi nambari 2 africa, lakini munaangiza nyama toka nje ya nchi, mko na over 2,000 coastline, mko na 3,000 rufiji delata acres amazo munaweza kuuza kufunga na kuuza schrimps and crabs, good mashamba ambapo munaweza kuza avocados and hortculture na mutengeneza billions every year, lakini hamna hilo.

Tanzania needs a seriuos investor in agriculture ambae atafundisha watu jinsi ya kufanya hii export of produce from tz. mwaka huu naja hapo tz na nitasirikiana na TAHA, and pia sugcot kuona ni vipi, kwahivyo jambo ninalosema kila muda ni kuwa ukasagundua tatizo, iliobaki ni kutafuta suluhiso,so kaa kuna yeyote ambae angehitaji either maarifa zaidi maana niko tayari na connection hapa EU na sio eu to hata asia and australia anaweza wasiliana nami toungee zaidi nikifika tuone vile tunaweza saidiana.

Mimi naamini kuwa mungu alituweka katika hii dunia tusaidiane, asanteni sana, sijui swahili yangu vipi, ukiwa intrested na hii bussiness get in touch pls, thank you

Habari za asubuhi naomba na mimi niongezee jambo hapo kwenye usafirishaji wa mazao. Miezi miwili nyumba alikuja rafiki yangu akanipa mchongo kuwa kwa sasa majirani zetu wa Rwanda wana njaa kupita kiasi.

Basi tukaenda boarer ya Rwanda tukaulizia nini wanahtaji hakutupata ushirikiano mzuri kabisaa
jamaa ikabidi azame ndani Kigali kabisaa huko akaja na fursa kede kede kweli njaa ipo Rwanda na wanahtaji sana msosi.

Basi tukajipanga kutafta vibali jamani asikwambie mtu vibali vya kusafirisha mazaoi nje (hata hapo Rwanda) ni vingi utazani daftari la tution.
Sasa tukaamua kuwa bora tu base na boarder ya Rwanda na wao wakatupa conditions zao baada ya hapo tukatafta gari maeneo ya kahama hapo tukachukuwa mzigo tukazama Kigali jamani mzigo uliisha ndani ya saa moja tu na hapo tuliuza kwa gharama ya juu sana.

Tukarudia mara nne hadi sasa tunategemea kurudia mara ya tano sasa.

Nilichojifunza katika biashara hii jamani. Ku export mazao kunahtaji uwe umejipanga kabisa na sio kukurupuka kama hapa wanasema sehemu fulani kuna soko la nyanya hapana soko lipo ila lina vigezo vyake balaa. Elewa vigezo vyote vya soko lako ndio uingie mfano sisi tulisikia Rwanda wanahitaji mihogo saana, na hata askari wa boda walisema mihogo inahtajika sana. Sasa tungekurupuka kupeleka mihogo Rwanda bila kuingia Kigali na kujua mihogo hiyo inahtajika katika hali gani mzee si tungelia jamani.

kingine nchi yetu siasa ni nyingi mnoo n uongo uongo ni mwingi sana, mfano hapa bongo wakulima wa mihogo wameaminishwa kuwa soko liko China ooh ni zuri nk wakat hapo Kigali mihogo ukiiprocess wanavyohtaji wao ni kama dhahabu. Hapo kigali viazi ni dili sana sana.
Tuweni serious na maisha jamani hakuna mafanikio ya bila kujitoa na kutoa jasho

Wachangiaji wengi kwenye hii mada nahisi wakati Tanganyika inapata uhuru walikuwa hawajazaliwa.
Tatizo kubwa la Tanganyika/Tanzania katika kukuza uchumi ni mabadiliko ya mara kwa mara ya Political economy yaliyokuwa yanafanywa.

....Kabla ya Uhuru uchumi wetu ulikuwa wa Kipebari/kabaila.
.... Baada ya Uhuru kulitokea mabadiliko makubwa ya uchumi kwa kufuata uchumi wa Kijamaa na kubinafsisha mali za watu binafsi na kuzifanya za umma.
....Baada ya ujamaa kushindwa tukarudi tena kwenye ubebari /ukabaila uchwara ambao bado hauko wazi katika kumiliki mashamba na viwanda kwa uhuru.
Mfano mzuri kwa Inchi zilizofanya makosa kama ya Tanganyika/Tanzania ni Zimbabwe.

Kenya hawakubadili mfumo wa uchumi wa Inchi toka wapate uhuru hadi leo.
Tunasema kila siku Inchi ambayo haina consistence katika Political economy kamwe haiwezi kuendelea kiuchumi.

Katika hili lazima tutofautishe swala la Education na Knowledge.
Education tunaipata darasani na knowledge (ujuzi) tunaupata kwa kufanya kazi.
Watanzania wengi wanafikiri wakisoma sana darasani basi wamekamilika. Ni heri ufanye kazi na mtu mwenye ujuzi (knowledge) lakini hana elimu kubwa kuliko kufanya kazi na mtu mwenye elimu kubwa lakini asiye na ujuzi.

Tanzania bado ni Inchi bora nadhani Duniani katika mazingira rafiki ya kujenga viwanda, kulima, kuchimba madini, bandari za kutosha, maziwa ya kutosha, mali asili kama wanyama na mbuga za wanyama, mito ya kutosha na kubwa kuliko yote AMANI YA INCHI.

Kenya katika haya yote wako nyuma mno na future yao baadaye wataitegemea Tanzania.
 
Uzi mzuri sana lakini sitoshangaa ukiwa na wachangiaji wachache.

Binafsi napenda sana Biashara za Exportation kiukweli zinafaida sana na hizi fursa wanafaidi watu wachache wanaojua ABC za kufanya exportation, Kuna mtandao mmoja jina lake limenitoka kidogo huwa nasikia ni wazuri sana kwa kuunganisha international buyer & seller.

Mkuu vipi wewe umeanza jaribu na zao gani??
 
Taarifa sahihi za Mbegu na masoko bado ni tatizo kubwa kwa wakulima wengi nchini, Gharama zinazochajiwa na wakaguzi wa kilimo na Mbegu mashambani nalo ni tatizo ndomana wakulima tunatumia local ways.

Ila kwa hii inshu ya exportation umenigusa sana, Napenda tu kujua kwa hapa nchini ni taasisi zp ambazo znachek ubora wa mazao na ku'issue vibali, na taasisi za nje ambazo unaweza ku-link nao ili kuwa na uhakika wa soko?
 
Asilimia kubwa ya wakulima ni wadogo kwa kiwango (peasants) na hivyo ni vigumu kwao kuwa na ufahamu wa mambo kama haya.. Wale wachache wanaoweza kujua mambo haya wamejikita zaidi kwenye upagazi (a.k.a. ajira) maofisini.

Kama ulivyosema, kwa Kenya viongozi wengi ni wafanyabiashara, kwa hiyo inakuwa rahisi kuwa na sera/sheria ambazo ni rafiki kwa biashara.

Nimewahi ku export kidogo seafood. Nilipeleka mara kadhaa kaa hai Singapore. Changamoto niliyokutana nayo ni vifo vya kaa, maana mzigo ukifika kule wanahesabu na kulipia walio hai tu. Hapa inawezekana mnunuzi asiwe mkweli juu ya kiwango cha vifo maana mzigo unatuma kwa ndege.. Lakini pia kwa hapa Tz usipokuwa makini unauziwa kaa ambao tayari wamechoka kutokana na kukaa siku nyingi tangu wavuliwe.

Kuhusu samaki frozen na fresh, changamoto ni kuwa, Fisheries (wizara ya uvuvi) wanataka uwe na kiwanda kilichoidhinishwa kwa ajili ya kuandaa mzigo. Kama huna kiwanda, uingie mkataba na kiwanda then ndo wizara watakuruhusu. Ukienda viwandani, vyote ni vya wahindi, na hawa wahindi hawakubali jambo hilo ili waendelee kufanya biashara wao tu
 
Naona tunaendelea na kasumba ya kulaumiana wabongo. Hakuna mkulima asiyependa kuuza nje ya nchi mazao yake maana huko ndio kuna faida kubwa kuliko soko la ndani ambalo halina uhakika wa bei. Leo korosho wanacheka lkn uhakika wa bei kuendelea kuwa nzuri bado haupo wakati huo mbaazi imeachwa shamba ng'ombe wanaila

Anyways point yangu ni kwamba, unaposema kuwa mkulima wa Tanzania anatakiwa abadilike aanze kuuza mazao nje tujiulize hilo soko la nje lipo wapi? Tatizo ni hizo connection za masoko ya nje. Wahindi wameshikilia hii biashara sababu wana connection ya wahindi wenzao huko india na Asia. Mimi mmatumbi napataje hiyo connection ya wateja wanao hitaji zao langu nje ya nchi?

Cha kufanya watu Kama mwenye thread hii ambao mmefanya research msiwe wachoyo, leteni taarifa za masoko ya nje muone kama watu hawaja changamkia fursa. Ukituambia unafanyia kazi utaleta mrejesho ndio hatukuoni Tena au hata tukija kukusikia huo mrejesho hautakuwa na taarifa za kina za hao wateja wa nje.

Kifupi selfishness/ubinafsi ndio vinatutia umasikini. Humu ndani kuna nyuzi nyingi tu za exportation na kwenye hizo nyuzi kuna watu ambao wana uzoefu na connection lakini hakuna hata mmoja aliyetoa contacts au maelezo yakinifu ya hizo connection wanaishia kujitapa tu. Hawa viongozi Wa serikali waacheni hata mkiwapa lawama wao hawana habari hivyo tusaidiane sisi wenyewe
 
Ila nafikiri wakulima wetu ifike mahali wabadilike kama unahitaji mafanikio fulani halafu ni mzito kujielimisha kuhusu njia sahihi za kuyafikia bási itakuwa shida.

Wakenya ni more agressive sana kwenye masuala kama haya miaka ya nyuma hapo kuna mkenya alikuwa anakuja kulangua vitunguu Singida na Asali Tabora; huyu jamaa alikuwa anafanya package na branding halafu ana export Asia sasa jifikirie ni faida gani alikuwa anatengeneza?
 
Taarifa sahihi za Mbegu na masoko bado ni tatizo kubwa kwa wakulima wengi nchini, Gharama zinazochajiwa na wakaguzi wa kilimo na Mbegu mashambani nalo ni tatizo ndomana wakulima tunatumia local ways.

Ila kwa hii inshu ya exportation umenigusa sana, Napenda tu kujua kwa hapa nchini ni taasisi zp ambazo znachek ubora wa mazao na ku'issue vibali, na taasisi za nje ambazo unaweza ku-link nao ili kuwa na uhakika wa soko?
Kuna mazao yenye vibali maalumu kama kahawa, korosho, pamba, etc , kuna mazao mengine hayana vibali maalumu rather utatakiwa uende wizarani pale watakupa maelekezo
 
Sijasikia habari ya vyama vya ushirika nahisi vina jukumu pande hizi!Je vimeshindwa au ni nini msingi wa vyama vya ushirika!.Kingine pia mitaji hao wakulima wakenya wanakopesheka vipi hawa wakwetu siamini kwamba ukosefu wa elimu wala connection ndo changamoto kubwa kwenye kilimo chetu la hasha!
 
Nimewahi ku export kidogo seafood. Nilipeleka mara kadhaa kaa hai Singapore. Changamoto niliyokutana nayo ni vifo vya kaa, maana mzigo ukifika kule wanahesabu na kulipia walio hai tu. Hapa inawezekana mnunuzi asiwe mkweli juu ya kiwango cha vifo maana mzigo unatuma kwa ndege.. Lakini pia kwa hapa Tz usipokuwa makini unauziwa kaa ambao tayari wamechoka kutokana na kukaa siku nyingi tangu wavuliwe.
sad experience
 
Back
Top Bottom