Kwanini waTanzania sio wazalendo!?

UrbanGentleman

JF-Expert Member
Jun 19, 2016
2,586
1,883
Hello salamu waungwana,

Kuna jambo flani limekua likintatiza sana nimekua nikijiuliza nini chanzo cha waTz wengi kuikana nchi yetu na kupiga teke utaifa hasa linapokuja swala la kuonesha wazi mapenzi na nchi yetu.

Unakuta si viongozi katika act zao za kutetea maslahi ya nchi tuu, Huu ni ugonjwa mpaka kwa vijana katika michezo hawajui wanawakilisha kitu gani as in identity ya kutambulisha origin ya muhusika.

Nimewahi kutembelea mataifa flani miaka ya nyuma nimeona jinsi watu wanavyoheshimu tamaduni za nchi nyingine na kutukuza utaifa wao kuanzia mavazi, vyakula mpaka imani zao.

Imefika mbali mpaka unakuta katika mitandao vijana wanaona ni vyema kusema wanaishi ughaibuni kuliko kusema wao ni wazawa wa chato au kolomije ni kwanini?

Kwanini uzalendo haupo, kwanini imekua ngumu kuweka utaifa kwanza kwanini imekua ngumu kujiuliza nitaifanyia nini Tanzania.?

Nitoe tu angalizo kuwe na somo la uzalendo katika mitahala yetu. Maana kunawakati lazima iwepo namna ya kuweka tofauti na selfishness zetu pembenu na uzalendo uchukue nafasi yake ili taifa letu lifaidike .

Nitaenda nchi zote duniani but I'm proud to be Tanzanian sababu its where I will rise my blood as Tanzanian sio mlomwizi,

Ukiangalia EPL kama wewe ni mpenzi wa premier league utaelewa kuwa wenzentu wanathamini sana utaifa wao first priority kwao ni Taifa analotoka sio hapo tu ukienda kwenye sector ya utarii wageni wanao kuja kilicho kikuu kwao ni Taifa lao watokalo lakini kwanini sisi ni tofauti!?

Utakuta viongozi wanaongea mambo ambayo unajiuliza hawa ni waTz kweli hawa wanafanya mambo ambayo unafika wakati unasema baada ya miaka kazaa watoto wetu watajivunia lipi!?

Guys tuwe na uzalendo ndani ya mioyo yetu. Hui kitu inaanzia ndani ya family zetu watoto wakiona unahubiri mapenzi juu ya Taifa letu wataiga uzalendo huo tu.




Gentleman
 
Hawana uzalendo kwa sababu ya ccm!

Walikuwa Wazalendo sana enzi za TANU na mwanzo wa CCM, lakini baadaye CCM imegeuka zimwi na kula uzalendo wao wote!.

Tulipigana vita vya uganda utkiwa wamoja kabisa kwa mapenzi ya dhati, lakini leo hii hatuwezi hata kuwachukulia hatua mafisadi walioko CCM!.

CCM imewaaminisha watu kwamba unafiki unalipa!.

CCM imeondoa mshikamano wa kitaifa imeleta mafarakano na matabaka.

CCM inawadharau wananchi na kuwafanya mali yake binafis na hivyo kuwaondolea upendo kwa nchi!.

CCM inafuga uharlifu kwa gharama ya wazalendo na kuwonyeshe Wazalendo kwamba uzalendo wao ni utumwa na mauti yao ni uhai wa Ccm!

CCM hainawajali Watanzania na inawatumia kwa kunufaisha watu wachache!

Ubaguzi, dharau, dhihaka, uonevu na uwongo wa ccm kwa Watanzania, ulaghai na matumizi ya nguvu badala ya hoja katika utawala, yamewafanya Watz waone hawna haki katika nchi il wao ni vibarua wa kuwazalishia na kuwalinda ccm.

CCM ndiyo sababu ya kuua uzalendo katika nchi kwa sababu viongozi wa CCM na mawakala wao hawana Uzalendo!
 
Mkuu hilo tatizo lilianzia pale tulipofuta somo la siasa shuleni.tukalibatiza sijui civics,tukabadilisha mitaala yetu,tukaua JKT.Na sisi tukakoma kuwa taifa.
Unafikiri hivi vinatosha? Ni kweli hapa ndipo tulipokosea?
 
Usishangae mkuu,mara ya mwisho kufurahia utanzania wangu ni kipindi nikiwa mtoto mchanga,tangu kipindi kile kodi ya kichwa inafanya kazi,nilijisikia vibaya sana kuona wazazi wangu wanakimbilia porini kukwepa kamata kamata,ilipofutwa,ufisadi na dhuluma vikashika hatamu.Njia pekee ya kurudisha uzalendo ni mpak fisiem iondoke.
 
Unafikiri hivi vinatosha? Ni kweli hapa ndipo tulipokosea?
Kwa fikra zangu za kkk,naona kama kila mtoto kitu chake cha thamani kukijua ni familia yake,cha pili ni taifa lake na hayo unajifunzia shuleni kwa elimu,nyimbo,michezo nk. Siku hizi hata muingiliano wa jamii umekufa,hatuna marafiki wala mashujaa,anyone can be a hero at any time.
 
Hawana uzalendo kwa sababu ya ccm!

Walikuwa Wazalendo sana enzi za TANU na mwanzo wa CCM, lakini baadaye CCM imegeuka zimwi na kula uzalendo wao wote!.

Tulipigana vita vya uganda utkiwa wamoja kabisa kwa mapenzi ya dhati, lakini leo hii hatuwezi hata kuwachukulia hatua mafisadi walioko CCM!.

CCM imewaaminisha watu kwamba unafiki unalipa!.

CCM imeondoa mshikamano wa kitaifa imeleta mafarakano na matabaka.

CCM inawadharau wananchi na kuwafanya mali yake binafis na hivyo kuwaondolea upendo kwa nchi!.

CCM inafuga uharlifu kwa gharama ya wazalendo na kuwonyeshe Wazalendo kwamba uzalendo wao ni utumwa na mauti yao ni uhai wa Ccm!

CCM hainawajali Watanzania na inawatumia kwa kunufaisha watu wachache!

Ubaguzi, dharau, dhihaka, uonevu na uwongo wa ccm kwa Watanzania, ulaghai na matumizi ya nguvu badala ya hoja katika utawala, yamewafanya Watz waone hawna haki katika nchi il wao ni vibarua wa kuwazalishia na kuwalinda ccm.

CCM ndiyo sababu ya kuua uzalendo katika nchi kwa sababu viongozi wa CCM na mawakala wao hawana Uzalendo!
Very hurting but unafikiri kipo chama kinachoweza kuokoa Taifa kutoka kwenye huu uzandiki !? Je nini kifanyike sote tufaidike hasa watoto wetu wafurahie matunda ya mbegu njema
 
Kula wale wachache, sheria na mikataba waingie wachache Kwa maslahi yao binafsi, likibuma ndio wajifanye kutuaminisha kutuungane kutetea rasilimali zetu. Katika hali kama hiyo uzalendo unatoka Wapi.

Wazee wetu walikua wazalendo enzi za kusaka Uhuru. Uzalendo wakulazimisha pasipo vitendo hauwezi kudumu
 
Usishangae mkuu,mara ya mwisho kufurahia utanzania wangu ni kipindi nikiwa mtoto mchanga,tangu kipindi kile kodi ya kichwa inafanya kazi,nilijisikia vibaya sana kuona wazazi wangu wanakimbilia porini kukwepa kamata kamata,ilipofutwa,ufisadi na dhuluma vikashika hatamu.Njia pekee ya kurudisha uzalendo ni mpak fisiem iondoke.
Sina imani na hao wengine kama ilivyo kwa hawa waliopo sasa sijui ni wapi tutaponea
 
Kwa fikra zangu za kkk,naona kama kila mtoto kitu chake cha thamani kukijua ni familia yake,cha pili ni taifa lake na hayo unajifunzia shuleni kwa elimu,nyimbo,michezo nk. Siku hizi hata muingiliano wa jamii umekufa,hatuna marafiki wala mashujaa,anyone can be a hero at any time.
Sure nakumbuka hii kitu lakini sikuhizi mmmnh
 
Kula wale wachache, sheria na mikataba waingie wachache Kwa maslahi yao binafsi, likibuma ndio wajifanye kutuaminisha kutuungane kutetea rasilimali zetu. Katika hali kama hiyo uzalendo unatoka Wapi.

Wazee wetu walikua wazalendo enzi za kusaka Uhuru. Uzalendo wakulazimisha pasipo vitendo hauwezi kudumu
Unafikiri nini kifanyike!?
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom