Mapenzi ni jambo linaloweza kuanza na kuisha hata kwa watu walio kwenye ndoa ila hapa Tanzania ni kama mwanamke akishaolewa hairuhusiwi mapenzi kwa mwanaume aliyemuoa yaishe.
Inashangaza watu wanaua watu, wanajeruhi na hadi kulawiti wanaume wenzao kwa sababu eti mke amechepuka!
Ile ahadi inayosemwa mtakuwa pamoja mpaka kifo kiwatenganishe huwa ni maneno tu kama katika kanga ila ukweli na uhalisia kwa binadamu haiko hivyo.
Wanaume wa Tanzania wametunga hadi msemo mke wa mtu ni sumu kwa hofu ya kuibiwa wake zao!