Kwanini wanaume hawafanyi hivi?

Wervemarcel

JF-Expert Member
Apr 10, 2015
2,390
3,293
Nawasalimu wakuu wote.

Leo mchana wakati nipo kwenye daladala, nikawa nawaza kimya kimya.

Kwanini utasikia Mwanamke ameenda kwa Mganga ili kumuwekea mume au mpenzi wake manjonjo asitoke kando?

Naomba nikiri, sijawahi kusikia tangu nimezaliwa, mwanaume ameenda kwa Mganga ili kumuwekea mke limbwata au mapenzi yakolee, Kuna nini hapa?

Inasemekana hata hawa vijana wa kiume wadangaji ( kina saydavto, noel gio etc) ni waumini wa waganga ili kulinda madanga yao, kwanini madanga hawaendi?

Nisiwachoshe tu ningependa kufahamu kuna connection gani hapa. Ni hilo tu kwa leo.
 
Siri yake ni pesa...sisi tunaenda kwa waganga sana tena ndio tunaongoza lakini hatuombi mapenzi tunaomba pesa kwani ukishapata pesa watakuja tena si mmoja tu unachagua uwatakae...pesa ni limbwata ya wanaume kwa wanawake
 
Siri yake ni pesa...sisi tunaenda kwa waganga sana tena ndio tunaongoza lakini hatuombi mapenzi tunaomba pesa kwani ukishapata pesa watakuja tena si mmoja tu unachagua uwatakae...pesa ni limbwata ya wanaume kwa wanawake
Umetolea ufafanuzi mzuri sana.

Vipi kuhusu wanawake wenye kila kitu lakini bado wanapanga foleni kwa mjomba, ni pesa au mapenzi?
 
Si kwa wanaume wa siku hizi.
Wanaume wengi wamekuwa wadangaji.
Wanadanga kutuzidi sisi dada zao.
Itakuwa wanaenda huko lakini hawasemi wanaenda kisirisiri.


Si utani, wanaume pia wanadanga hasa hawa wa jiji la makonda.

Ndio maana nimetolea mfano hapo kwenye bandiko langu.

Ila hawa wengi wao ni kina juma lokole ( chakula).
 
Si kwa wanaume wa siku hizi.
Wanaume wengi wamekuwa wadangaji.
Wanadanga kutuzidi sisi dada zao.
Itakuwa wanaenda huko lakini hawasemi wanaenda kisirisiri.
Wanaenda sana ila wanajifanya wanatafuta pesa kumbe madanga , mwenzao anadaiwa boxes huko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom