Kwanini Wana CHADEMA ni wabishi sana? Huu ukweli huupinga!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Karibia wanaCHADEMA wote unaweza kusema ni watoto wa mama mmoja na kuna kitu kinawaunganisha, nacho ni ubishi.

Kuna hili jambo la Uchaguzi, wanaCHADEMA wote husema kwamba wao hushinda uchaguzi na kwamba huibiwa kura, na mfano mzuri ni Uchaguzi uliopita, lkn kwa nini mahesabu hayaendani na madai yao ya kuibiwa kura?

Kwa mfano CHADEMA walipata Wabunge 30 tu wakati CCM walipata Wabunge zaidi ya 150 na wana chadema wote huyakubali matokeo ya Ubunge lkn husema kwamba walishinda kura za Urais na kwamba waliibiwa, sasa hili mtu mwenye akili anaweza kulielezea vipi? Iweje Mtanzania asiwaamini CHADEMA kwenye kuongoza Bunge halafu akawaamini kwenye kuongoza Nchi?

Ni kwa nini CHADEMA wanakuwa wabishi namna hii na hawataki kuukubali ukweli kwamba bado hawajaweza kukubalika na Watanzania kuongoza hii nchi? Kuishi kwa uongo hakuwasaidii kwani mnawafanya wanachama wenu waamini jambo ambalo halipo, na hivyo kupunguza nafasi huko mbele ya kujiboresha.

Waambieni ukweli watu wenu kwamba, tumeshindwa uchaguzi kwa sababu kura zetu hazikutosha lakini kwa kuongeza juhudi na maarifa tuna uwezo mkubwa wa kuongeza kura zetu chaguzi zijazo, huu ndiyo ukweli na wala siyo udhaifu kama mnavyofikiri.
 
Tukutane 2020..ccm daima


Hata kama chadema watapata Wabunge 10 dhidi ya 200 wa CCM bado watasema wameibiwa kura za Uraisi, hapo ndipo ninaposhindwa kuwaelewa ni kwa nini ni wajinga namna hii?
 
Kwa kawaida ili tendo la kubishana lifanyike lazima kuwe na wa kubishana naye...

Hebu tuambie hao chadema wanabishana na nani?? Siamini kama watakuwa wanabishana wenyewe kwa wenyewe...

Kama kuna wanayebishana nao, na chadema wakaonekana ni wabishi zaidi, basi hao wanaobishana na watakuwa wazembe kama kenge.
 
Mshauri kwanza Mh. apeleke hela za wahanga wa tetemeko.

Sisi wakati tunatuma fedha zetu kwenye v-Mpesa vyetu tuliguswa na wale wahanga sio serikali.

Serikali inavyanzo vingi vya kupata pesa bila kutumia ulaghai na kula fedha za rambirambi.

Hii serikali Mungu anaiona lakini .!
 
Michezo ya ccm ya kugawa majimbo kisanii hili kuongeza wabunge ni uhafidhina,,mf.kulikua na haja ya kugawa nzega kua nzega mjini na vijijini,huo si uhuni,na kuna sehemu nyingine tuliangukia pua kama ubungo,,,
 
...

Hebu tuambie hao chadema wanabishana na nani?? Siamini kama watakuwa wanabishana wenyewe kwa wenyewe...

Unalosema ni sahihi ila mleta mada kakosea kwamba wana CHADEMA ni wabishi.

Viongozi wa CHADEMA na wafuasi/wanachama hawawaamini wengine na kwa sababu hiyo ni dhahiri kwamba hawajiamini. Matokeo yake huropoka hovyo (siyo ubishi) na kwa shari. Ukiwasikiliza kwenye majukwaa au bungeni, utaona jinsi wanavyoongea kwa kufoka utafikiri wanagombana na mtu.
 
60% ya wabunge wa ccm hawakushinda uchaguzi , wakiwamo mbunge wa kyela na mbunge wa songea mjini , kwa uwezo wako mdogo wa gharama ya elfu 7 huwezi kuyajua haya , huko aliko lubuva anakucheka sana .
 
Karibia wanachadema wote unaweza kusema ni watoto wa Mama mmoja na kuna kitu kinawaunganisha, nacho ni ubishi!

Kuna hili jambo la Uchaguzi, wanachadema wote husema kwamba wao hushinda uchaguzi na kwamba huibiwa kura, na mfano mzuri ni Uchaguzi uliopita, lkn kwa nini mahesabu hayaendani na madai yao ya kuibiwa kura?

Kwa mfano chadema walipata Wabunge 30 tu wakati CCM walipata Wabunge zaidi ya 150 na wana chadema wote huyakubali matokeo ya Ubunge lkn husema kwamba walishinda kura za Uraisi na kwamba waliibiwa, sasa hili mtu mwenye akili anaweza kulielezea vipi? Iweje Mtanzania asiwaamini chadema kwenye kuongoza Bunge halafu akawaamini kwenye kuongoza Nchi?

Ni kwa nini chadema wanakuwa wabishi namna hii na hawataki kuukubali ukweli kwamba bado hawajaweza kukubalika na Watanzania kuongoza hii nchi? Kuishi kwa uongo hakuwasaidii kwani mnawafanya wanachama wenu waamini jambo ambalo halipo, na hivyo kupunguza nafasi huko mbele ya kujiboresha!

Waambieni ukweli watu wenu kwamba, tumeshindwa uchaguzi kwa sababu kura zetu hazikutosha lkn kwa kuongeza juhudi na maarifa tuna uwezo mkubwa wa kuongeza kura zetu chaguzi zijazo, huu ndiyo ukweli na wala siyo udhaifu kama mnavyofikiri!
sio ubishi tu na matusi...wengi wamefubzwa akili ili viongozi wao wafikie malengo.
 
Mwizi kila siku anapiga hesabu za kuiba tu, wezi wakubwa nyie" mnaiba hadi mnajiibia wenyewe mnaiba ushindi, mnaiba matokeo, mnaiba michango ya wahanga, sasa unakuja na hoja za kwa nini chadema wanalalamika, we nani alikuambia ccm walishinda majimbo yote hayo kama si kuiba na kupoka na kupora na kunyang'anya na kuvamia ushindi wa upinzani, nenda kwanza kamwambie baba yako aache unyang'anyi kwa wanakagera.
 
Du hivi kumbe Ccm tunawabunge zaidi ya 150 so nilikuwa napiga vimahesabi hapa kama wabunge =150 zidisha kwa mgao wa m10 sijui jibu ni b 1.5 au laki na nusu embu wasomi nisaidieni hapo coz hizo sifuri sijui ni ngapi

Hiyo ni siku moja
 
Chadema Kuna makundi matatu,
1:werevu au great thinkers ambao huwa hawakurupuki ovyo na wanauelewa wa mambo huku wakipinga vitu kisomi.
2:Werevu kwa njaa zao wameamua kuweka akili Kando kuwa mapupet wa viongozi hata kama viongozi hawakosahihi. Uelewe wao unakodishwa kuwanufaisha maboss na sio taifa.
3:wafuata mkumbo wasiojua hata nini wanapinga au wanabisha ila tu msingi wa kubisha huko ni kuleta utofauti na CCM au serikali au kumap mawazo na kauli za kisiasa za wakuu wao. Hawa ni wengi kama mchanga wa bahari huku pia wamejaa. Kipimo mfano hadi sasa angalia unazungumzia nini na wao wanajibu nini.

Naomba kuwasilisha
 
Why is Congress still majority Republican when a Democrat has been president for 8 years?
If the American majority have favored Democrat for 8 years, shouldn't congress be majority Democrat by now?

WWW. quora .com

Hebu jibu hii logic kwanza
 
Back
Top Bottom