YEHODAYA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2015
- 36,909
- 51,904
Wanaume wengi wawe viongozi wa dini au wa kijamii au wa mitaani ndio huwa wanakomalia kufundisha mwanamke anavyotakiwa kuishi na mwanaume.
Ukienda Misikitini unakuta Maimamu na Mashehe ndio walimu wa kumsomesha mwanamke aishije na mwanaume. Ukienda kwa Wasabato unakuta wanaume ndiyo walimu wakuu. Kwa Wakristo unakuta Mchungaji au Padri ndiye kinara wa kutundisha mwanamke aishije na mwanaume. Ukienda mitaani na Vijijini wanaume ndio hujifanya waalimu wa kufunza wanawake jinsi ya kuishi na mwanaume.
Hivi kwani wanawake huwa hawapewi nafasi ili wafunze wanawake wenzao jinsi ya kukaa na mwanaume? Wanaume wanaogopa nini kuwapa maiki wanawake wafunze wanawake wenzao?
Ukienda Misikitini unakuta Maimamu na Mashehe ndio walimu wa kumsomesha mwanamke aishije na mwanaume. Ukienda kwa Wasabato unakuta wanaume ndiyo walimu wakuu. Kwa Wakristo unakuta Mchungaji au Padri ndiye kinara wa kutundisha mwanamke aishije na mwanaume. Ukienda mitaani na Vijijini wanaume ndio hujifanya waalimu wa kufunza wanawake jinsi ya kuishi na mwanaume.
Hivi kwani wanawake huwa hawapewi nafasi ili wafunze wanawake wenzao jinsi ya kukaa na mwanaume? Wanaume wanaogopa nini kuwapa maiki wanawake wafunze wanawake wenzao?