Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Hivi karibu taasisi tatu zinazojihusisha na utetezi wa sheria na haki za binadamu, zitafungua jumla ya kesi 10 ndani ya miezi mitatu katika Mahakama Kuu ya Tanzania, kupinga sheria kandamizi zinazominya demokrasia na uhuru wa kujieleza.
Taasisi hizo ni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC).
Taasaisi hizi wakishirikiana na watetezi wa demokrasia nchini wanafungua kesi katika nyakati ambazo.
Kwanza, wakurugenzi wa halmashauri ambao ni wasimamizi wa uchaguzi, wengi wao wameteuliwa wakiwa ni makada kindakindaki wa CCM.
Pili, wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wateule wa mwenyekiti wa CCM taifa kwa cheo cha urais, wanamaelekezo ya kutowatangaza wapinzani kuwa wameshinda kwa sababu aliyewateua, anayewalipa mshahara na magari anatokana na CCM.
Tatu, kuna matukio mengi yanayofanywa na wakurugenzi wa halmashauri (wasimamizi wa uchaguzi) yenye kuminya haki kwa vyama vya upinzani na kupendelea chama tawala CCM. Mathalani kunyimwa barua za utambulisho kwa mawakala wa chadema katika jimbo la kinondoni.
Nne, kukithiri kwa vitendo vya kiharifu kama mauaji, kukamatwa, kutekwa na kuumizwa kwa viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani. Matharani mgombea udiwani wa kata ya Mhandu Mwanza na meneja kampeni wake walikamatwa na kupelekwa gereza kuu la Butimba Mwanza wiki mbili kabla ya uchaguzi ili kutoa mwanya kwa CCM kufanya kampeni. Huku washindani wa CHADEMA wakiwa gerezani.
Kati ya sheria ambazo wameanza kupambana nazo kwa kufungua kesi ili zifanyiwe marekebisho, ni Sheria ya Vyama vya Siasa, Sheria ya Jeshi la Polisi na Sheria ya Uchaguzi.
Wanaharakati hawa wanachukua hatua nyakati ambazo tubashuhudia unyama wa kutisha ukifanywa kwa viongozi wa upinzani, utekaji, ubambikiwazi kesi, mashambulizi ya risasi za moto, mauaji yamegeuka na kuwa sehemu ya utamaduni mpya wa siasa zetu.
Wakati haya yakiendelea viongozi wetu wakina mzee Kikwete, Mkapa, Mwinyi, Warioba nk. Wamekaa kimya kabisa huku mambo yakiendelea kwenda mlama
Tayari wanaharakati wanaendelea na mapambano haya katika mamlaka za kisheria ( Mahakama), hata hivyo Fatuma Karume anasisitiza akisema, "Hatutakata tamaa kwenye hili," "Tumeshuhudia vitendo vingi ndani ya nchi vinavyowanyima wananchi demokrasia na uhuru wa kujieleza.Hii ni kinyume na katiba na ndiyo maana tumeunganika kupinga sheria hizo kwa mustakabali wa taifa"
Karume anasisitiza kuwa hawatakata tamaa, anasisitiza kuwa hatakata tamaa kwa sababu anajua fika kwamba sio rahisi watawala kufurahishwa na mapambano hayo. Hivyo wanaweza kuweka vizingiti na vikwazo vya kila namna.
Fatuma na wenzake wanafanya haya kwa maslahi mapana ya nchi yetu. Ni muda muafaka wa kuwaunga mkono kwa kila namna ili kulinasua taifa letu na kila hila na uonevu.
Taasisi hizo ni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC).
Taasaisi hizi wakishirikiana na watetezi wa demokrasia nchini wanafungua kesi katika nyakati ambazo.
Kwanza, wakurugenzi wa halmashauri ambao ni wasimamizi wa uchaguzi, wengi wao wameteuliwa wakiwa ni makada kindakindaki wa CCM.
Pili, wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wateule wa mwenyekiti wa CCM taifa kwa cheo cha urais, wanamaelekezo ya kutowatangaza wapinzani kuwa wameshinda kwa sababu aliyewateua, anayewalipa mshahara na magari anatokana na CCM.
Tatu, kuna matukio mengi yanayofanywa na wakurugenzi wa halmashauri (wasimamizi wa uchaguzi) yenye kuminya haki kwa vyama vya upinzani na kupendelea chama tawala CCM. Mathalani kunyimwa barua za utambulisho kwa mawakala wa chadema katika jimbo la kinondoni.
Nne, kukithiri kwa vitendo vya kiharifu kama mauaji, kukamatwa, kutekwa na kuumizwa kwa viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani. Matharani mgombea udiwani wa kata ya Mhandu Mwanza na meneja kampeni wake walikamatwa na kupelekwa gereza kuu la Butimba Mwanza wiki mbili kabla ya uchaguzi ili kutoa mwanya kwa CCM kufanya kampeni. Huku washindani wa CHADEMA wakiwa gerezani.
Kati ya sheria ambazo wameanza kupambana nazo kwa kufungua kesi ili zifanyiwe marekebisho, ni Sheria ya Vyama vya Siasa, Sheria ya Jeshi la Polisi na Sheria ya Uchaguzi.
Wanaharakati hawa wanachukua hatua nyakati ambazo tubashuhudia unyama wa kutisha ukifanywa kwa viongozi wa upinzani, utekaji, ubambikiwazi kesi, mashambulizi ya risasi za moto, mauaji yamegeuka na kuwa sehemu ya utamaduni mpya wa siasa zetu.
Wakati haya yakiendelea viongozi wetu wakina mzee Kikwete, Mkapa, Mwinyi, Warioba nk. Wamekaa kimya kabisa huku mambo yakiendelea kwenda mlama
Tayari wanaharakati wanaendelea na mapambano haya katika mamlaka za kisheria ( Mahakama), hata hivyo Fatuma Karume anasisitiza akisema, "Hatutakata tamaa kwenye hili," "Tumeshuhudia vitendo vingi ndani ya nchi vinavyowanyima wananchi demokrasia na uhuru wa kujieleza.Hii ni kinyume na katiba na ndiyo maana tumeunganika kupinga sheria hizo kwa mustakabali wa taifa"
Karume anasisitiza kuwa hawatakata tamaa, anasisitiza kuwa hatakata tamaa kwa sababu anajua fika kwamba sio rahisi watawala kufurahishwa na mapambano hayo. Hivyo wanaweza kuweka vizingiti na vikwazo vya kila namna.
Fatuma na wenzake wanafanya haya kwa maslahi mapana ya nchi yetu. Ni muda muafaka wa kuwaunga mkono kwa kila namna ili kulinasua taifa letu na kila hila na uonevu.