Kwanini Wakenya wengi wanasema mlima Kilimanjaro uko nchini kwao?

Ngamanya Kitangalala

JF-Expert Member
Sep 24, 2012
501
1,214
Kwa miaka mingi kumekuwepo na baadhi ya Wakenya wamekuwa wakisema na kutangaza huko duniani kuwa Mlima Kilimanjaro unapatikana ndani ya nchi yao.

Ni jambo ambalo limekuwa likiendelea kwa muda mrefu sana,mpaka kufikia kwa baadhi ya wageni( watalii) kutoka nchi mbalimbali duniani, kuamini kuwa mlima huo mrefu kabisa barani Africa kweli unapatikana nchini Kenya.

Ukipata muda tafuta kitabu kinaitwa "Why Tanzania is where it is: Tanzania's Colonial Boundaries from the Berlin Conference, 1884-1885 until its independence" kitabu hiki kimeandikwa na mjerumani Profesa Heinz Schneppen.

Kwenye kitabu hicho, kinaeleza kuwa kabla ya mwaka 1890 mlima Kilimanjaro na bandari ya Mombasa, zote zilikuwa Kenya,
kwenye himaya ya Waingereza.

Lakini baadaye kukawa na mabishano makubwa sana, kati ya waingereza na wajerumani kwenye kugombea umiliki wa ziwa Victoria

Sababu kubwa ya mabishano hayo, ilikuwa ni kutafuta chanzo cha mto Nile, ndani ya ziwa Victoria, kwa sababu kwa wakati huo, ilikuwa ukipata chanzo cha mto Nile unakamata Sudan, Misri na bahari ya Mediterranean, ambayo ilikuwa ni muhimu sana kwa wakati kwa sababu ya usafirishaji kwa bara la Ulaya.

Baada ya Uingereza kupata chanzo cha mto Nile, kule Jinja nchini Uganda, ndipo wakakubaliana kuchora mipaka upya kupitia mkataba wa Ango- Germany treaty wa tarehe 01 July 1890, ambapo Ujerumani walipewa 51% ya ziwa Victoria

Ndipo mpaka wa himaya ya wajerumani (Tanganyika) ukahama kutoka kusini ya Musoma na kupanda juu mpaka kaskazini ya Musoma haya yameelezwa kwenye kitabu kinaitwa "International boundaries of East Afrika", kilichoandikwa na A.C McEwen mwaka 1971

Ambapo sasa mlima Kilimanjaro na Mombasa zote zikaangukia ndani ya himaya ya wajerumani ( Tanganyika)

Kwa hiyo sasa, bandari zote katika pwani ya Afrika mashariki, zikawa zimeingia ndani ya himaya ya wajerumani ( Tanganyika)

Ndipo Waingereza wakaomba kupewa Mombasa ili na wao wawe na bandari

Na ndio mstari ule wa mpaka ukapindishwa pale kwenye mlima Kilimanjaro na kunyosha mpaka chini, ili Mombasa iwe ndani ya himaya ya Waingereza


Nadhani ndio sababu mpaka leo Wakenya wengi wanaamini mlima Kilimanjaro ni mali yao, kitu ambacho sio sahihi, Mlima Kilimanjaro uko Tanzania, kutokana na mipaka iliyochorwa na wakoloni
 
Utasemaje mlima Kilimanjaro ulikuwa Kenya wakati kabla ya 1885 ( Berlin conférence) hakukuwa na nchi iitwayo Kenya. Tuwe makini na propaganda za wa Kenya wapo vizuri sana kwenye hilo swala...

kwa kutumia hoja hoja hiyo hiyo ya Wa Kenya, asilimia 5% ya ziwa Victoria ambayo ipo Kenya inatakiwa irudishwe Tanzania pamoja na pwani yote ya Kenya maana pwani ya Kenya ilikuwa sehemu ya zanzibar na asilimia 5 ya ziwa Victoria ambayo Kenya wanayo sasa ilikuwa sehemu ya German East Africa.
 
Ule mlima upo Tanzania unateremkia bonde la Rufiji na kusababisha maji yanayotoka mlimani kuwa maji tiririka katika mto Ruvuma hadi Ruvuma basin katika pwani ya Mtwara.

Angalau watu wa Msumbiji wanaweza kusema ule Mlima Kilimanjaro upo nchini mwao, kwa sababu ya msitu mkubwa wakenya wanazani ule mlima upo karibu na kwao halafu wakenya wengi hawakusoma kihivyo wao wamesoma kingereza tu ila kwenye hizi taaluma za kimazingira ni wachofu sana.
 
Matumizi mazuri ya fursa kuvutia watalii, Karibu Kenya Masai Mara utaona pia Mt.Kilimanjaro, pia makampuni yao yanaandaa safari wapanda milima,japo hakuna njia kupandia upande wa Kenya.
 
Africa yote ni nchi 1 sema majambazi ndo yalikuja kutuwekea mipaka ndo maana wa masai wa kenya na bongo wapo kitu kimoja unawatenganisha mpka tu.
 
Kwa Sasa brochures za utalii Kenya zinasema ukitaka kuuona mlima Kilimanjaro vizuri pitia Kenya .
 
Hivi huko Berlin wamasai wangapi walialikwa? Au wakurya.wajita ndo. Makabila ya maeneo haya!!!

Au walikaa tu kihuni?? Sasa km hawakualikwa kwa nini hilo li umoja la OA.lisipangue huo ujinga?

Yaaani wote ni sehemu ya ethiopia na Misri tu. Na Africa yote ibadili hili jina la kupewa.eti Africa"" ni hili bara liitwe "E E continental" Ethiopia &Egypt nchi mama hizi.badala ya neno Africa ni la udhalili mno.mkijua maana yake wengu humu mtalia.

ndo maana Weusi mnakuwa maskini ; mbumbu.sababu ya hili jina. Sawa na kumuita mtoto jina eti Matatizo.au sumu atakuwa sumu kweli. Muda ni huu haribuni jina hili unaambiwa wewe muafrika una kubali tu!

Wewe ni. " Brown EE" wala siyo black african.ni jina la kuwadumaza.ukitaka kumuua mbwa mpe jina baya
 
Mount Kilimanjaro is in Tanzania, located northeastern, near the Kenya border. It is the tallest mountain in Africa rising at 5,895 meters (19,340) feet above sea level and Its one of the seven summits. Kilimanjaro is approximately 200 miles from the Equator and about 140 miles (225 km) south of Nairobi, Kenya

Mount Kilimanjaro is famous tourist attraction bringing thousands of participants from all over the world. Kilimanjaro is award winning mountain climbing destination.

Tourists usually climb Mount Kilimanjaro from Tanzania, permits to enter Kilimanjaro National Park are provided in Tanzania by Government authority Conservation called KINAPA.

Mount Kilimanjaro is in Tanzania close to a small town called Moshi.

Kenyans, for years, have done a great job at advertising Mount Kilimanjaro as their own due to the fact that Tanzania is it’s neighbor and that it can be seen on their side but the fact is that the whole mountain is on the Tanzanian side and all the climbing permits are through Tanzania government.

Kilimanjaro location on a map


Don’t be fooled anymore if you thought that Mount Kilimanjaro is located in Kenya. You can also go on Google maps and search for ” Mount Kilimanjaro” and you will see the location.

Can you see Mount Kilimanjaro from Kenya?​

Mount Kilimanjaro can be seen from Amboseli national park in Kenya. One of the best places to view Kilimanjaro on a clear day and also the greater Amboseli ecosystem is Observation Hill.

Kilimanjaro view from Amboseli National Park Kenya


Even though you can see Mount Kilimanjaro from the Kenya, It can only be accessed/climbed from the Tanzanian side.



Mount Kilimanjaro Location on google maps​







Below I have a quick summary of the 7 Mount Kilimanjaro Routes.​

Marangu Route: Hut accommodation is only available on this Kilimanjaro route.

Machame Route: The most popular Kilimanjaro route.

Rongai Route: The easiest Kilimanjaro route. This route ascends Mount Kilimanjaro from the north-eastern side of the mountain, along the border between Tanzania and Kenya

Lemosho Route: The most beautiful Kilimanjaro route.

Northern Circuit Route: The newest and longest Kilimanjaro route.

Umbwe Route: The shortest, steepest and hardest Kilimanjaro route.

Shira Route: Approaches from the Western side of Kilimanjaro.

When planning to climb Mount Kilimanjaro, you are required to get yourself acclimatized for a few days. Visit Arusha or Moshi a town at the foot of the mountain to relax and get yourself acclimatized.
 
Ule mlima upo Tanzania unateremkia bonde la Rufiji na kusababisha maji yanayotoka mlimani kuwa maji tiririka katika mto Ruvuma hadi Ruvuma basin katika pwani ya Mtwara.
Angalau watu wa Msumbiji wanaweza kusema ule Mlima Kilimanjaro upo nchini mwao, kwa sababu ya msitu mkubwa wakenya wanazani ule mlima upo karibu na kwao halafu wakenya wengi hawakusoma kihivyo wao wamesoma kingereza tu ila kwenye hizi taaluma za kimazingira ni wachofu sana.
Duh...mkuu upo serious! Mlima Kilimanjaro na Msumbiji wapi na wapi? hahahahaha!
 
Unakuta nchi zote hizo mali ya Mfalme wa Zanzibar Husein Bin Ali Bin Hassan El Mwinyi.
 
Mkuu kwa reference izo hakika umefanya jambo zuri na binafsi nimepata kitu. Lkn kama na wao wanasema Mt.kilimanjaro ni yao bac hata na sie ile mombasa ni yetu
 
Back
Top Bottom