Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa Jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.
Eti ndugu zangu watanzania;
Kwanini ENGINEERS wazuri sana duniani (Magari, Mitambo) wanapatikana nchini Ujerumani? Siri yao ni nini hasa?
Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba;
Moja (1) Siku ya Ijumaa ilee ya wiki iliyopita nilimsindikiza mjomba wangu mmoja kule kariakoo kwenda kununua kipuri (spare) moja ya mshine ya kusagia unga kwa ajili ya kupeleka kijijini kwao kwa maana hii ndio biashara yake miaka nenda rudi.
Sasa baada ya kufika katika duka la baba mmoja mtanzani mwenye asili ya bara la asia (al maaruf kama mhindi) tukakuta ni kweli anayo spare ile ila zipo za aina tatu. Moja ni kitoka nchini Singapore, nyingine nchini China na ya tatu ni kutoka nchini Ujerumani. Sasa yeye akawa anamsisitiza mjomba wangu kwa lafudhi ya Kiswahili cha kihindi "chukua hii baba ipo genuine kabisa fresh from german" basi uncle akanunua, akalipa kisha sisi haoooo tukarudi zetu home.
Mbili (2) Vile vile inasemekana kwamba, mtu akianza kuendesha gari za Kijerumani kama vile Mercedes Benz, BMW, Audi au VolksWagen kwa namna zinavyokuwa nzito na kutulia sana barabarani, mtu huyo kamwe hatotamani tena maishani mwake kuendesha gari za Kijapan kama vile Toyota na Nissan.
Tatu (3) Bila kuishia hapo, huku mitaani pia mara nyingi kumekuwepo na msemo maarufu kwa mfano utamsikia mtu akijigamba kwa rafiki yake kwamba "daaah mwanangu hii pasi tangia niinunue huu ni mwaka wa 8 sasa na sijawahi kuipeleka kwa fundi, chuma cha mjerumani hiki mzee baba"
Nne (4) Msafari wa Rais wa Russia ndugu Vladmir Putin umejaa gari za kijerumani tupu. Kuanzia BMW motorcycles; and Mercedes G-Class, Mercedes E-Class, S-Class mpaka BMW 5 Series. Tazama picha ya msafara wa Putin hapo chini.
Sasa kwa kuzingatia scenario hizo zote nne (4) ndio nikajawa na maswali mengi sana akilini mwangu kwamba WHY ARE GERMANS SO GOOD AT ENGINEERING?
Kuna baadhi ya watu hapa watakuja kusema ninaisifia sana Ujerumani kwa maana ninauza vitabu vyao hahahahaaaaaa
OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
PUMZIKA KWA AMANI MZEE MKAPA. VITA UMEIPIGANA NA MWENDO UMEUMALIZA BABA YETU. MUNGU AKUPE PEPO ILIYO NJEMA MZALENDO MWENZANGU.
Eti ndugu zangu watanzania;
Kwanini ENGINEERS wazuri sana duniani (Magari, Mitambo) wanapatikana nchini Ujerumani? Siri yao ni nini hasa?
Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba;
Moja (1) Siku ya Ijumaa ilee ya wiki iliyopita nilimsindikiza mjomba wangu mmoja kule kariakoo kwenda kununua kipuri (spare) moja ya mshine ya kusagia unga kwa ajili ya kupeleka kijijini kwao kwa maana hii ndio biashara yake miaka nenda rudi.
Sasa baada ya kufika katika duka la baba mmoja mtanzani mwenye asili ya bara la asia (al maaruf kama mhindi) tukakuta ni kweli anayo spare ile ila zipo za aina tatu. Moja ni kitoka nchini Singapore, nyingine nchini China na ya tatu ni kutoka nchini Ujerumani. Sasa yeye akawa anamsisitiza mjomba wangu kwa lafudhi ya Kiswahili cha kihindi "chukua hii baba ipo genuine kabisa fresh from german" basi uncle akanunua, akalipa kisha sisi haoooo tukarudi zetu home.
Mbili (2) Vile vile inasemekana kwamba, mtu akianza kuendesha gari za Kijerumani kama vile Mercedes Benz, BMW, Audi au VolksWagen kwa namna zinavyokuwa nzito na kutulia sana barabarani, mtu huyo kamwe hatotamani tena maishani mwake kuendesha gari za Kijapan kama vile Toyota na Nissan.
Tatu (3) Bila kuishia hapo, huku mitaani pia mara nyingi kumekuwepo na msemo maarufu kwa mfano utamsikia mtu akijigamba kwa rafiki yake kwamba "daaah mwanangu hii pasi tangia niinunue huu ni mwaka wa 8 sasa na sijawahi kuipeleka kwa fundi, chuma cha mjerumani hiki mzee baba"
Nne (4) Msafari wa Rais wa Russia ndugu Vladmir Putin umejaa gari za kijerumani tupu. Kuanzia BMW motorcycles; and Mercedes G-Class, Mercedes E-Class, S-Class mpaka BMW 5 Series. Tazama picha ya msafara wa Putin hapo chini.
Sasa kwa kuzingatia scenario hizo zote nne (4) ndio nikajawa na maswali mengi sana akilini mwangu kwamba WHY ARE GERMANS SO GOOD AT ENGINEERING?
Kuna baadhi ya watu hapa watakuja kusema ninaisifia sana Ujerumani kwa maana ninauza vitabu vyao hahahahaaaaaa
OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
PUMZIKA KWA AMANI MZEE MKAPA. VITA UMEIPIGANA NA MWENDO UMEUMALIZA BABA YETU. MUNGU AKUPE PEPO ILIYO NJEMA MZALENDO MWENZANGU.