Mung Chris
JF-Expert Member
- Sep 12, 2017
- 3,367
- 3,778
Nimejiuliza sana, kati ya waganga nilio wahi kuwafahamu au kuwatembelea na wale ambao marafiki zangu wachache wali wahi kuwaona hakuna ambaye nimewahi kutana naye ambaye hana magonjwa makubwa kama Presha, HIV, au kwa wanawake wana matumbo makubwa utadhani ni wajawazito, na ni maskini sana.
Ukienda kwao watakwambia wanatibu hayo magonjwa ila kwenye familia zao au wao wenyewe wanayo hawawezi kujitibu na kuwatibu wana familia wao.
Watakwambia tutakupa dawa ya biashara ili ufanye biashara upate pesa zaidi huku wao wenyewe hawamiliki biashara au ndugu zao hawamiliki biashara, familia zao zinakuwa ni maskini sana, je pesa alizowahi kukusanya kwenye uganga au uchawi haiwezi kuanzisha biashara ili na wao waitumie dawa ili wapate hela nyingi.
Watakwambia atakufanyia dawa ili uwe tajiri umiliki mapesa mengi sasa unajiuliza kwanini akufanyie wewe wakati yeye, ndugu zake na watoto wake wana maisha duni sana kwanini asiwafanyie nao wapate hayo mapesa.
HIVI SISI HUWA NI VIPOFU AU TUMELOGWA KUDANGANYWA
Ukienda kwao watakwambia wanatibu hayo magonjwa ila kwenye familia zao au wao wenyewe wanayo hawawezi kujitibu na kuwatibu wana familia wao.
Watakwambia tutakupa dawa ya biashara ili ufanye biashara upate pesa zaidi huku wao wenyewe hawamiliki biashara au ndugu zao hawamiliki biashara, familia zao zinakuwa ni maskini sana, je pesa alizowahi kukusanya kwenye uganga au uchawi haiwezi kuanzisha biashara ili na wao waitumie dawa ili wapate hela nyingi.
Watakwambia atakufanyia dawa ili uwe tajiri umiliki mapesa mengi sasa unajiuliza kwanini akufanyie wewe wakati yeye, ndugu zake na watoto wake wana maisha duni sana kwanini asiwafanyie nao wapate hayo mapesa.
HIVI SISI HUWA NI VIPOFU AU TUMELOGWA KUDANGANYWA