Kwanini wafanyakazi wa mashirika ya umma na serikalini hawapigi kelele sheria ya Hifadhi ya Jamii?

mr liverpool! madai yako mengi! mfano: dr uli na mukoba, hawa jamaa! si watumishi wauma! ila angalia wanachokifanya, watumishi wenyewe kuuza sura tu! au na wewe mr liverpool umo?
Sidhani kama ni lazima wewe unione barabarani na bango ndipo ujue kwamba naunga mkono madai, nafikiri uliona mgomo wa Walimu (watumishi wa Umma), Uliona jinsi Muhimbili ilivyokuwa mfano kwenye mgomo n.k Hoja hapa ni kwani wafanyazai wa Umma wapo kimya kwenye madai ya marekebesho ya sheria mpya ya mafao? Majibu yangu na ya watu wengine ni kwamba ni kwa sababu watumishi wa Umma wanaoongozwa na sheria ya Utumishi wa Umma na kanuni zake wanalazimika kustaafu/kupata pension miaka 55 kwa hiari na 60 kwa lazima. Hoja ya kupinga sheria mpya ina mantiki kwa sababu ukiajiriwa Private unakuwa chini ya masharti ya NSSF (10/10) na unaweza kufukuzwa muda wowote. Sasa kwanini usubiri mpaka miaka 55? Wakati Mtumishi wa Umma anapoajiriwa anaambiwa kabisa pension yak ni after 55 au 60 years kupitia LAPF, PPF, PSPF na GEPF (5/15). HOJA YA KUDAI MAREKEBISHO NI YA MSINGI SANA MKUU NA KILA MTU ANAIUNGA MKONO
 
Jamani nashangazwa hv ni kwa nn wafanyakazi wa mashirika ya umma/Serikalini..mfano walimu,madakitari,mapolisi,Tanesco,TRA hawajapigia kelele hiyi sheria mpya ya kupewa mafao baada ya miaka 55 na kuendelea?..inamaana wao hawako katika mifuko hiyo au inakuaje?.

Kwasababu wanapata ULAJI SEHEMU NYINGINE hawategemei MAFAO; ni WAGUSHAJI

WAKUBWA...
 
quote_icon.png
By Gerrard

Sababu ni moja tu. Barua zetu zimeandikwa "Appointment under Permanent and Pensionable Terms". Siku ya kwanza unapoajiriwa na kuingia mkataba unajua utastaafu kwa hiari miaka 55 na kwa lazima miaka 60. So unapiga kelele ili iweje?




Hapo penye red pameniuma sana mkuu hata hivyo usijali naheshimu mawazo yako
Ha ha ha pole sana Mkuu, potezea tu na mimi nafuta kauli yangu. Tuendelee na mada yetu Mkuu
 
Kwasababu wao wana uhakika wa kufanya kazi hadi wanastaafu!!!

Japokuwa wengi wao huwa wanapigika kupita kiasi pamoja na kupewa mafao yao ya miaka 60 wakati wanaotungiwa sheria ya hakuna fao la kujitoa ambao wapo sekta binafsi wao huwa vizuri kwa kuwa kisaikolojia walishajiandaa kwamba anytime wanapigwa chini
 
Utaratibu wa Pensheni kwa watumishi wa umma ni tofauti kabisa na hayo ya NSSF na PPF. Michango ya mtumishi wa umma kwenye Pensheni si mkubwa maana mishahara pia ni midogo.Lakini anapostaafu mtumishi wa umma anapata mafao mazuri maana Serikali inamwongezea katika akiba yake. Kuna formula inafanyika ambayo mtu hulipwa kulingana na muda aliotumika na ngazi ya mshahara wa mwisho hivyo kwao ni bora kusubiri hiyo miaka ya kustaafu kuliko kuacha kazi na kuchukuwa kiakiba chake ambacho hakitoshi chochote.
 
Gerald,sasa je,ungekuwa kwe2 malawi raisi wetu mbabe mwanamke banda anayelidai ziwa letu lote malawi liwe la malawi tu angekupa ujemedari wa batalion ya blantaya kwa kusema ukweli huo
 
Last edited by a moderator:
Nadhani ni kwa sababu zifuatazo:
Mosi-Serikalini kazi hazina presha, job security ni kubwa na nafasi za kutengeneza pesa kwa wizi ni nyingi sana. Matokeo ni kuwa kama kwanza hauna presha ya kazi, una uhakika kwamba iwe jua au mvua bado utakuwepo kwenye ajira na mwisho pamoja na kuwa kamshahara rasmi ni kadogo bado utatengeneza pesa kwa njia mbalimbali..una sababu gani ya kuacha kazi, na ikiwa huna sababu ya kuacha kazi..una sababu gani ya kufikiria kuhusu pensheni wakati una hakika kuwa wakati ukifika pensheni yako itakuwepo bali tayari utakuwa umeshatengeneza maisha kupitia njia kadhaa za magumashi.

Pili-Wafanyakazi wa serikalini na Ma-Sina Uchungu(SU) wana nidhamu ya woga...usitegemee wao kushiriki kuipinga serikali iliyowaajiri kwa kupitisha sheria hii dhalimu(hawaoni kuwa hata sisi katika private sector tunachangia uwepo wa ajira zao kupitia PAYE tunazolipa kila mwezi).

Tatu-Kazi katika sekta binafi zinachosha na kuzeesha haraka....kwa sababu hiyo, wengi tunafanya kazi tukiwa na malengo kuwa baada ya muda tutoke na kutafuta shughuli nyingine nyepesi kidogo...katika hili wengi tunafikiria self-employment, hilo la kujiajiri linahitaji mitaji na kwetu hayo mafao ya kujitoa ni sehemu ya hiyo mitaji. kwa hiyo mtu anapozuia tusipate mafao hayo mpaka tukifika miaka 55-60(binafsi nna 37 kwa hiyo ni miaka17-23 ijayo), tunamuona kama mwenye dhamira mbaya ya kuua jitihada zetu za kutaka kujitegemea baada ya kutumika katika sekta binafsi.

Nne-Kuna sababu za kisiasa pia, si lazima ziwe ni siasa za vyama bali ni ile tu kuwa watu hawako tayari tena kuona mijitu iliyoshiba mpaka kuvimbirwa, inakaa huko kisha ikapanga kuwa ili tuwe na maisha bora ya uzeeni basi wazuie tusichukue kilicho chetu wakati ulio muafaka kwetu bali iwe ni kwa vile wao wanavyoona itafaa. Wameshindwa kutuwekea mazingira ya sisi wenyewe kujitengenezea maisha bora leo tukiwa bado vijana, hawawezi kuwa na dhamira ya kweli ya kutuwekea maisha bora ya uzeeni. Tunaamini kuwa hizo ni hadaa na ghilba za wanasiasa uchwara na wachumia matumbo....tumenyonywa vya kutosha, tumedharauliwa vya kutosha na sasa wakati umefika wa kusema HAPANA!!!

Nawasilisha!
 
kuna job security ukifanya kazi serikalini au shirika la umma.

Job Security ni wewe mwenyewe. Mimi nafanya kazi private sector na sikirii kufukuzwa. Private sekta kuna opportunity nzuri ya ku-practice na baadaye kuanzisha kampuni yako. Serikalini wenyew mmesema ni wavivu. Si maneno yangu ni maneno yenu.
 
Back
Top Bottom