Kwanini waandishi wa habari Tanzania hawaripoti taarifa zenye maslahi mapana kwa Taifa letu?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Nimekuwa nikifuatilia waandishi wa habari wa nchi hii, nikagundua kuwa zile habari muhimu sana, zenye maslahi mapana kwa Taifa hili hawaziandiki na badala yake, wao Kila siku ni kuandika "mapambio" ya kusifu na kuabudu viongozi walioko madarakani!

Waandishi wa habari wa nchi yetu, wamejijengea tabia ya kuwa hata kama ni "minor issue" ilimradi lmefanywa na watawala wetu wa CCM, basi watai-report kwa ukubwa Sana, wakati "big issues" kama hizo za kuuawa kwa raia zenye utata, wakizifukia!

waandishi wa habari Wana dhamana kubwa Sana ya kutuhahabarisha sisi wananchi kuhusu matukio mbalimbali yanayotokea hapa nchini.

Nikitoa mfano ni wa habari hii ilivyotokea majuzi ya Mauaji ya watuhumiwa watatu wa Mauaji wa ujambazi, yaliyotokea huko Serengeti, Mkoani Mara, ambapo uongozi wa Chadema, umetilia shaka Mauaji hayo, baada ya taarifa ya RPC wa Mara, kuwa watuhumiwa hao wa ujambazi, waliuawa, baada ya kurushiana risasi na askari.

Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema, kwa waandishi wa habari, ni kuwa taarifa hiyo inatia shaka Sana, kutokana na "circumstancial evidence" ya Mauaji hayo yalivyotokea.

Tufahamu pia wajibu namba moja wa Jeshi letu la Polisi, ni kutulinda sisi raia pamoja na mali zetu.

Kwa hiyo uongozi huo wa Chadema, umemuomba Rais Samia, aunde Tume ya Majaji, kuchunguza Mauaji hayo.

Uundwaji wa Tume hiyo ya Majaji, kwa tukio lenye utata, haitokuwa jambo geni, kwa kuwa kama mkumbukavyo, wakati wa utawala wa awamu ya nne, ya Jakaya Kikwete, aliunda Tume ya aina hiyo, baada ya Mauaji ya watu, ambao Polisi wetu walitoa taarifa kuwa waliwaua "majambazi" hao wakati wakijibizana risasi.

Hata hivyo baada ya Tume hiyo kutoa ripoti yake, ikaeleza kuwa hao waliotajwa na Jeshi letu la Polisi, kuwa walikuwa majambazi, hawakuwa majambazi, bali walikuwa wafanyibiashara halali wa madini, toka Ifakara!

Ili kuujua ukweli wa Mauaji yanayoendelea nchini kwetu, siku hadi siku, kwa madai ya Polisi, kuwa wameuawa baada ya kujibizana kwa risasi, inabidi Rais Samia, aunde Tume hiyo ya Majaji, Ili kuondoa utata huu, kwa kuwa kwa mfumo wetu wa utawala, mhimili pekee unaoweza kutoa hukumu ya kifo ni mhimili wa Mahakama baada ya kupokea ushahidi.

Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa sheria zetu, hakuna mtu mwingine yeyote aliyepewa mamlaka hiyo ya kuua raia bila kwanza kupata ushahidi usiokuwa na shaka.

Kuendelea kuruhusu mtindo huu wa Polisi kujichukulia sheria mkononi, Taifa hili tunaliingiza kwenye hatari kubwa, kwa kuwa leo yamewakuta hao raia wa Serengeti, nani anayejua who is next, may be it can be you or me🥺

Mungu ibariki Tanzania
 
Nimekuwa nikifuatilia waandishi wa habari wa nchi hii, nikagundua kuwa zile habari muhimu sana, zenye maslahi mapana kwa Taifa hili hawaziandiki na badala yake, wao Kila siku ni kuandika "mapambio" ya kusifu na kuabudu viongozi walioko madarakani!

Waandishi wa habari wa nchi yetu, wamejijengea tabia ya kuwa hata kama ni "minor issue" ilimradi lmefanywa na watawala wetu wa CCM, basi watai-report kwa ukubwa Sana, wakati "big issues" kama hizo za kuuawa kwa raia zenye utata, wakizifukia!

waandishi wa habari Wana dhamana kubwa Sana ya kutuhahabarisha sisi wananchi kuhusu matukio mbalimbali yanayotokea hapa nchini.

Nikitoa mfano ni wa habari hii ilivyotokea majuzi ya Mauaji ya watuhumiwa watatu wa Mauaji wa ujambazi, yaliyotokea huko Serengeti, Mkoani Mara, ambapo uongozi wa Chadema, umetilia shaka Mauaji hayo, baada ya taarifa ya RPC wa Mara, kuwa watuhumiwa hao wa ujambazi, waliuawa, baada ya kurushiana risasi na askari.

Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema, kwa waandishi wa habari, ni kuwa taarifa hiyo inatia shaka Sana, kutokana na "circumstancial evidence" ya Mauaji hayo yalivyotokea.

Tufahamu pia wajibu namba moja wa Jeshi letu la Polisi, ni kutulinda sisi raia pamoja na mali zetu.

Kwa hiyo uongozi huo wa Chadema, umemuomba Rais Samia, aunde Tume ya Majaji, kuchunguza Mauaji hayo.

Uundwaji wa Tume hiyo ya Majaji, kwa tukio lenye utata, haitokuwa jambo geni, kwa kuwa kama mkumbukavyo, wakati wa utawala wa awamu ya nne, ya Jakaya Kikwete, aliunda Tume ya aina hiyo, baada ya Mauaji ya watu, ambao Polisi wetu walitoa taarifa kuwa waliwaua "majambazi" hao wakati wakijibizana risasi.m

Hata hivyo baada ya Tume hiyo kutoa ripoti yake, ikaeleza kuwa hao waliotajwa na Jeshi letu la Polisi, kuwa walikuwa majambazi, hawakuwa majambazi, bali walikuwa wafanyibiashara halali wa madini, toka Ifakara!

Ili kuujua ukweli wa Mauaji yanayoendelea nchini kwetu, siku hadi siku, kwa madai ya Polisi, kuwa wameuawa baada ya kujibizana kwa risasi, inabidi Rais Samia, aunde Tume hiyo ya Majaji, Ili kuondoa utata huu, kwa kuwa kwa mfumo wetu wa utawala, mhimili pekee unaoweza kutoa hukumu ya kifo ni mhimili wa Mahakama baada ya kupokea ushahidi.

Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa sheria zetu, hakuna mtu mwingine yeyote aliyepewa mamlaka hiyo ya kuua raia bila kwanza kupata ushahidi usiokuwa na shaka.

Kuendelea kuruhusu mtindo huu wa Polisi kujichukulia sheria mkononi, Taifa hili tunaliingiza kwenye hatari kubwa, kwa kuwa leo yamewakuta hao raia wa Serengeti, nani anayejua who is next, may be it can be you or me.

Mungu ibariki Tanzania
Huenda wamemuachia mmoja wao yule anyeziiita makala zake kwa maslahi ya taifa 😂😂.kisa wamekubaliana kutafuta ulaji kwa wanachukua chako mapema kwa zamu 🤸🤸🤸
 
Waandishi wa Habari ndio watu tunaowategemea kuleta uelewa kwenye Jamii yetu ila wamepigwa Super glue midomoni. Freedom of speech was banned years ago now days Hadi waandishi wa Habari wa michezo nao wanajadili mpira kama siasa.
Tunategemea Hili kundi kwa 80% kuleta mabadiliko katika Jamii imekuwa kinyume chake wanazungumza wakiwa nyuma ya mlango.
Tanzania yangu daaah!
Am super proud to be here
 
Waandishi wa Habari ndio watu tunaowategemea kuleta uelewa kwenye Jamii yetu ila wamepigwa Super glue midomoni. Freedom of speech was banned years ago now days Hadi waandishi wa Habari wa michezo nao wanajadili mpira kama siasa.
Tunategemea Hili kundi kwa 80% kuleta mabadiliko katika Jamii imekuwa kinyume chake wanazungumza wakiwa nyuma ya mlango.
Tanzania yangu daaah!
Am super proud to be here
Naunga mkono hoja, kuwa waandishi wa habari wamewekewa super glue, midomoni mwaol🥺
 
Waandiahi walikuwa na njaa Sana hawa. Nadhani mnakumbuka kilio cha ndugu yetu Pascal Mayalla. Kilio chake kilikuwa ni cha waandishi wa habari wote.

Mama alipoingia madarakani amejua kucheza na njaa za waandishi wa habari ili kuwafunga midomo.

Anaambatana nao ktk safari za nje....hili lilikuwa ni ombi maalumu kwa mama lililotolewa na mwenyekiti wa TEF ndugu Balile.

Wanapewa matangazo ya serikali......ombi la pili la ndugu Balile kwa niaba ya waandishi wa habari.

Baada ya kupewa walichokitaka unategemea wataandika nn zaidi ya kumsifia mama?? Mama hata aboronge atapewa sifa kedekede
 
Tasnia ya habari Tanzania ni pasua kichwa mkuu hii inachangizwa na sababu mbalimbli ambazo kwa namna moja ama nyingine zinafanya waandishi kuogopa kufanya investigative journalism ( Habari za uchunguzi)

Mosi,waandishi wamepoteza dira kwa kuacha maadili ya kazi yao na kusaka nafasi za uteuzi hii imepelekea wengi kuwa makasuku mfano ni Mwandishi nguli Pasco mayalla.

Pili,Kupotea na vifo vya utata kwa waandishi wa habari ndani ya nchi hii nani asiye jua juu ya kupotea kwa Bwana Azori ngwanda wa Mwananchi communication limited? Bado tasnia ya habari haija sahau kifo Cha Daudi Mwangosi wa channel Ten mkoa wa Iringa vipi kuhusu kifo Cha utata Cha bwana Stani katabalo

Tatu,sheria kandamizi zipo bado tusijitoe ufahama kujisaulisha kwamba sheria zimebadilika zipo mfano ni The Media Service Act of 2016.licha kwamba sheria hii imetoa mwanga mzuri kwa kutambua Journalism Kama professional lakini Kuna vipengele ni hatari kwa ustawi wa tasnia ya habari nchini.

Nne,Kuto zingatia taaluma (unprofessionalism) Kuna watu mpaka Leo wanaamini kwamba uandishi ni kipaji(talent) na sio taaluma(professional) ndio maana kwenye media nyingi wamejaa vilaza mfano wakina Mwijaku,Baba levo nk

Tano, Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia yameleta kitu kinacho itwa "Citizen Journalism" hii kitu imekuwa challenge kwa waandishi wengi maana kila mtu ana share habari hivyo Mwandishi lazima afanye jambo la ziada kuonesha utofauti wake na watu ambao sio waandishi.

Kwa uchache naomb niishie hapa GT wataongeza madini muhumu
 
Waandiahi walikuwa na njaa Sana hawa. Nadhani mnakumbuka kilio cha ndugu yetu Pascal Mayalla. Kilio chake kilikuwa ni cha waandishi wa habari wote.

Mama alipoingia madarakani amejua kucheza na njaa za waandishi wa habari ili kuwafunga midomo.

Anaambatana nao ktk safari za nje....hili lilikuwa ni ombi maalumu kwa mama lililotolewa na mwenyekiti wa TEF ndugu Balile.

Wanapewa matangazo ya serikali......ombi la pili la ndugu Balile kwa niaba ya waandishi wa habari.

Baada ya kupewa walichokitaka unategemea wataandika nn zaidi ya kumsifia mama?? Mama hata aboronge atapewa sifa kedekede
Mkuu umenena vema kabisa chanzo Cha mapato kwa media house ni matangazo na mbaya zaidi serikali ndio inatoa matangazo mengi kwa hali hii chombo kipi kipo tayali kukosoa serikali wakati huo huo matangazo ndo chanzo kikuu Cha mapato kwenye media na serikali ndo mtangazaji mkuu

Kuna msemo mmoja kwenye tasnia ya habari unasema kwamba

"Huwezi mnyoshea kidole mtu ambaye anakuwekea sahani ya chakula mezani" mwisho wa kunukuu
 
Ungeuliza kwanini wananchi hawapendi kufatilia taarifa / habari zenye masilahi mapama ya nchi hii badala yake wanaendeshwa kwa trends za ajabu?
Wananchi wafuatilie taarifa zenye maslahi, wazifuatilie ziko wapi ????

TBC na ITV kuna taarifa mule ? Au unaongelea hawa vijana wa online TVs waliajiriwa na Millard Ayo na Nasibu Abdul? Na wale ma DJ wanaosoma vichwa vya magazeti asubuhi na kufanya fanya utani hapo studio siku imekwenda, hao ndio newsmen unaosema tuwafuatilie ?

We can only consume what we are fed. Usiwalaumu wananchi kwenye hili tafadhali.
 
Nimekuwa nikifuatilia waandishi wa habari wa nchi hii, nikagundua kuwa zile habari muhimu sana, zenye maslahi mapana kwa Taifa hili hawaziandiki na badala yake, wao Kila siku ni kuandika "mapambio" ya kusifu na kuabudu viongozi walioko madarakani!
Mkuu 'Mystery', kumbe jibu tayari unalo kwenye huo mstari wa mwisho! Ni "Maslahi."

Nchi inasubiri "Revolution" hii, kuondokana na hali hii mbovu iliyotapakaa kila mahali, hadi kwa wananchi wenyewe!

Utaanzia wapi kuhoji mwandishi wa habari, tena mwandishi anayemfanyia kazi mwenye kijarida chake ambaye naye ni mnufaika wa muundo uliopo?

Mi nadhani, wakati mwingine inafaa kuanzisha mada kama hii siyo kwa kuhoji, kana kwamba jibu halijulikani, bali itasaidia sana kuchambua hali hiyo inayowakabili unaowaita "waandishi wa habari."
Kiufupi, Tanzania sasa hatuna waandishi wa habari.
 
Naunga mkono hoja, kuwa waandishi wa habari wamewekewa super glue, midomoni meal🥺
Hivi mkuu 'Mystery', kwenye mada kama hii, hatuwezi kuwa hata tunatafuta mifano ya wengine wanafanya nini, na kwa nini sisi hapa hali ni tofauti kabisa?

Binafsi sitaki kwenda mbali sana kutafuta mfano tunaoweza kuutumia katika kuangalia hali yetu na hawa wengine.
Kuna mambo mengi sana huwa sikubaliani na mambo yanayofanyika Kenya kuwa mfano kwetu, lakini nikiangalia tasnia ya habari na waandishi wa huko, na kuilinganisha na hii yetu hapa, huwa naona aibu sana hata kujilinganisha nao; hata kwenye mambo wanayoandika ambayo sikubaliani nao.

Kiujumla, nadhani hali yetu ni zaidi ya kuwekewa "superglue midomoni" kwa waandishi wetu. Tatizo ni pana zaidi, na sehemu muhimu ya tatizo hilo ni elimu yetu.
Angalia hata katika uandishi wa mapambio unaofanywa na hawa wa kwetu. Ukisoma huwezi kutoka umeridhika na uandishi wenyewe uliotumika kwenye makala za namna hiyo. Makala za kusifu.
 
Back
Top Bottom