Kwanini Waafrika hatuendelei katika maisha

kwisha

JF-Expert Member
Sep 9, 2021
1,662
4,330
Kuna kitu nimejifunza katika maisha yetu sisi wa Afrika na nimepata jibu kwanini sisi ni maskini

First one sisi wa Afrika atupatiane support

Second one sisi wa Afrika tuna wivu sana

Unaweza mkuta mtu anaogapa kumfanyia jirani yake kitu fulani eti akimpa atafanikiwa ni bora akampe mtu mwingine support ambaye awezi msaidia kuliko kumpa jirani yake ambaye akifanikiwa

Mfano akijenga kiwanda ili naye siku moja akapate kazi apo yeye anaona wivu kwa style hii atuwezi endelea tutabaki kuwa nyuma siku zote

Mwaka jana nilitembelea TZ Dar es Salaam nilichokiona kiliniuzunisha saana

Kulikuwa na mdada fulani ambaye alikuwa anauza biashara vyake pale kuna wateja wengi walikuwa wanakuja wengi walikuwa wana sema ana BEI Saana mpaka alikuwa na lazimika kuuza kwa bei ya asara ili mradi tu asikose kidogo ya cha kula usiku

Siku moja nikamuuliza ivi unapataga faida katika ivi biashara vyako? Akaniambia ikitokea Bahati nzuri anapataga ila Mara nyingi wao wanafanya biashara ili wapete tu pesa za kuwalisha watoto wao Wala si kwa mahendeleo yao hicho kitu kili ni uzunisha unaweza je kumlinganisha mfanya biashara mdogo na mkubwa?

Eti waweke bei sawasawa hiyo ni tatizo

Sisi wa teja wa kawaida tusapoti wa Fanya biashara wa dogo ili nao kesho wa sapoti wa fanya biashara wa kubwa wewe ukimnunulia kitu chake leo kesho naye atamnunulia mfanya biashara mkubwa

Lakini unaweza kuta mtu ana ogopa kununua hata pipi kwa mfanya biashara mdogo eti ana bei anaenda moja kwa moja kwa mfanyabiashara ukubwa akanunue pipi ya BEI chini bro's mnategemea hawa wafanyabiashara wadogo nani atawafanya kuwa wa kubwa kama sisi

Na sasa hivi kumesha kuwa na upumbavu wa wafanya biashara kila mfanya biashara amesha kuwa Na wateja wake kitu ambacho kina waumiza wanaoanza biashara

Utakuta mtu anatoka Dar anaenda Dodoma kununua tu mchele wa kula eti Dar kuna bei sana unategemea hwa wa dar wakanunuliwe na nani kama sio wewe?

Mfano mimi nikiwa Rais naweza funga upambavu huo ili kila mkoa wafanyabiashara vyao iwe bei kali isiwe bei kali ivyo vitakuangalia ni wewe tu kutoa sapoti ili wenzako wa endelee ukitaka kufanya biashara vya Dili kubwa apo ndipo una weza ruhusiwa kufanya biashara katika mikoa mwingine

Katika inch yangu ya asili DRC kwenye mkoa wangu sasa ivi wananishukuru vijana wanaendelea wengine wanafanya biashara kwa mawazo yangu na support yangu ndogo tu

I trust Afrika we can -- when we give support to each other.
 
Mkuu bora ujali maisha yako na familia yako. Hata hao unawatetea wapewe support ndo wana roho mbaya. Yani bora hata usimsaidie. Sisi waafrika hata tukisaidiwaje hatusaidiki
 
Sababu zako ni nyepesi Sana,kikubwa ni Afrika inazalisha isivyotumia na inatumia isivyozalisha haiwezi kuendelea.

Kuhusu hicho kisa cha mtu kutoka hapa na kwenda sehemu nyingine kupata huduma,hii sio kwa waafrika peke yao.
Hata wazungu.

Kule Zenj mahotel Mengi ya kitalii yanamirikiwa na wazungu,wazungu Hawa wakitaka huduma kama za matengenezo madogo ya ujenzi, umeme, thamani, hawazitafuti kutoka kwa waafrika wa Zenj, watatafuta mzungu mwenzao awape hiyo huduma ata kama yupo nje ya nchi.

Kingine mtoto wa Kiafrika anazaliwa kwenye mazingira yasio na fulsa,Wanaijeria wanaenda South Afrika,wakifika wanaanzisha biashara na wanafanikiwa sana.

Sababu za kutokufanikiwa Afrika ni nyingi na zinarofautiana kila sehemu.

Rushwa, Siasa mbovu, Nigeria inazalisha mafuta lakini ndani ya nchi mafuta ni gharama kubwa!!!mafuta ya Rwanda yanapita Bandari ya Dar, lakini bei ya mafuta Rwanda ni ndogo ukilinganisha na Kule Dar.
 
Kuendelea bongo ni ngumu sana, mchawi wa kwanza ni serikali halafu na wengine ndio wanafuata sasa
 
Kwa sababu tukijenga kamjengo kana Fensi tiles na aluminium vio vya kuslode plus gari ya kutembelea na tuviwanja viwili ya akiba plus fremu za kupangisha basi tunajkua tumemaliza maendeleo.

Nimesahau moja na.la watoto kuwalipia ada st.english academia

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Sababu za umaskini wetu ulizozielezea sizo kabisa. Hakuna mtu mwenye akili timamu atanunua vitu vya bei ya juu wakati vya bei ya chini vyenye ubora huo huo anaweza kuvipata
 
Sababu za umaskini wetu ulizozielezea sizo kabisa. Hakuna mtu mwenye akili timamu atanunua vitu vya bei ya juu wakati vya bei ya chini vyenye ubora huo huo anaweza kuvipata
Kwa wazungu tuna nunua tu kwani utafanya aje usipo nunua unategemea Nani ATA nunua
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom