Kwanini vizazi vya kati ya mwaka 1980 na 2000 wanajulikana kama Kizazi cha Msongo wa Mawazo?

jastertz

JF-Expert Member
Jul 4, 2020
391
740

Ni mambo gani ambayo yamechangia hilo?

Kwanza kabisa, hebu tuanze kwa kufafanua zaidi tatizo kubwa katika msongo wa mawazo.

Hii inajidhihirisha kama dalili fulani, ambazo tunaweza kuangazia kama unapokuwa na msongo wa mawazo sehemu kubwa ya siku, kupungua kwa shauku katika shughuli ambazo hapo awali zilisababisha raha, kuongeza au kupungua kwa uzito, kukosa usingizi, kuhisi huna maana, kupoteza nishati, hisia za kutokuwa na thamani au hatia nyingi, kupungua kwa uwezo wa kufikiri au kutuliza akili katika kufanya jambo lako, na mawazo ya mara kwa mara ya kutaka kujiua.

Miezi michache iliyopita mgonjwa aliniambia: "Mimi ni wa kizazi cha msongo wa mawazo."

Ilikuwa kikao chake cha kwanza na alikuja kwa matibabu kwa sababu alijikuta bila hamu ya kitu chochote, bila motisha na hisia za kwamba maisha hayana maana.

Alikuwa sahihi, yeye ni wa kile kizazi kinachoitwa "kizazi cha msongo wa mawazo", kizazi ambacho kinajumuisha wawili kati yao: waliozaliwa kati ya mwaka 1981 na 1995 yaani (milenia) na wale waliokuja ulimwenguni kati ya 1995 na 2010 yaani (kizazi Z)

Kuna sababu kadhaa kwa nini kwanini viazi vya Milenia na Z wanajulikana kwa pamoja kama 'Kizazi chenya Msongo wa mawazo'.

Wacha tuchambue sababu tofauti ambazo zinaweza kuchochea hali hiyo, kwa upande wangu naweza sema ni:
1. Mitandao ya kijamii
2. Wasiwasi wa kidunia
3. Msongo wa ukosefu wa ajira
4. Wasiwasi wa kila mara kuhusu jamii

Kiufupi; kuanzia kufadhaika kwa ukosefu wa kazi hadi kuwajibika kupita kiasi kwa shida za ulimwengu: kuna sababu nyingi zinazoathiri hali ya kihisia na kiakili ya vijana.

Wewe unahisi ni kwanini? Karibu uchangie.
 
Pesa ni jawabu la kila Jambo wape pesa za kutosha na hakuna msongo
Wapo wenye pesa but ndo wagonjwa kuliko wasio kuwa nazo.

Wenye hela hawna furaha hata kidogo, na kama wanayo ila wanahitaji zaidi,
pesa sio kila kitu,
 
wapo wenye pesa but ndo wagonjwa kuliko wasio kuwa nazo.

wenye hela hawna furaha hata kidogo, na kama wanayo ila wanahitaji zaidi,
pesa sio kila kitu,
Asikudanganye mtu pesa ndo inayoleta furaha na wengine Wana mali ils cash hawana..pesa unampata demu yoyote unakunywa chochote unaenda popote
 
Asikudanganye mtu pesa ndo inayoleta furaha na wengine Wana mali ils cash hawana..pesa unampata demu yoyote unakunywa chochote unaenda popote
kama vile una hoja ngoja tukusikilize.
but me nachojua furaha ya pesa inategemea upo wapi na unafanya nini na wewe ni nani.
 
Pesa ni jawabu la kila Jambo wape pesa za kutosha na hakuna msongo
Ni kweli majibu ni pesa! Lakini ajabu pesa wanapewa wale waliokua nazo tayari kuzazi cha wabinafsi <<<<-1979! Sasaiv kizazi hichi cha msongo wa mawazo hakijaliwi pamoja na changamoto za mabadiliko ya maendeleo ya mwanadamu kinayo yapitia tena kwa kasi sana! Hakuna muda wa kurelax na kujipanga ni mchakamchaka kila siku!!!
 
kama vile una hoja ngoja tukusikilize.
but me nachojua furaha ya pesa inategemea upo wapi na unafanya nini na wewe ni nani.
Una million zako Mia Saba unanunua simu yoyote,mashine yoyote,unakula chochote Ila zikikata ule wasiwasi na hofu na msongo wenyewe
 
~Wanapata kila kitu,so akili zao zinakosa challenge kubwa,ubongo unakuwa loose tu,.....akili inahitaji changamoto ili kuwa busy.

~Teknolojia,na mitandao ya kijamii pia inachangia sana

~Kutaka mafanikio ya haraka.

Maelezo zaidi yanapatikana kwenye uzi wangu huu


 
~Wanapata kila kitu,so akili zao zinakosa challenge kubwa,ubongo unakuwa loose tu,.....akili inahitaji changamoto ili kuwa busy.

~Teknolojia,na mitandao ya kijamii pia inachangia sana

~Kutaka mafanikio ya haraka.

Maelezo zaidi yanapatikana kwenye uzi wangu huu


Instant gratification .
 
Wapo wenye pesa but ndo wagonjwa kuliko wasio kuwa
Wazungu wana kika kitu ila wanakuja kuirafuta furaha Afrika kwa mwsmvuli wa utalii.
Huku vijijini watu wameyakuvsli maisga tso hivyo wanafuraha.
Wanatembeleana, wanazikana, wansoeaba chumvi. Nk
Mjini watu hawaaminiani, hawasalimianu,hawatembrleani, wansoneana wivu, wanafitiniana, wanaugua magonjwa yasiotibika kama kisukari.
wanamatananio makubwa,
Mwishowe wanapata msongo wa mawazo
 
Back
Top Bottom