Yawezekana kuna upotoshaji wa makusudi kabisa juu ya uwepowa viti maalum bungeni kuwa ni nafasi wanazopewa vyama vya Siasa kuchagua Wanawake wa vyama hivyo kuingia Bungeni kama Wawakilishi wa vyama husika. Nadhani swala hili linahitaji kujadiliwa Upya na Elimu itolewe kwa Wananchi na wahusika.
Sheria zinazotoa Mwongozo kuhusu viti maalum ni pamoja na:-- Katiba; Sheria ya Taifa Ya Uchaguzi; na
Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2010 hivyo ni muhimu sana Wananchi wote kuzingatia kwa nini uwepo wa viti maalum Bungeni.
Imeelezwa bayana kuwa: - Viti maalum ni viti vilivyotengwa kwa mujibu wa sheria kuhakikisha kwamba watu au makundi ya watu wenye mahitaji maalum na ambao si rahisi kugombea Uchaguzi na kushinda kwa sababu ya hali yao (kama ulemavu na Uchache wao) wanapata nafasi ya kuwakilisha maoni na vipaumbele vyao katika ngazi tofauti za Uongozi (Bungeni, Wilayani, Halmashauri).
Kwa mujibu wa Sheria hizi, haya makundi yaloainishwa mpaka sasa katika bunge letu ni WANAWAKE na WALEMAVU. Na kwa upande wa Wanawake, Vyama vya Siasa vimepewa nafasi ya KUPENDEKEZA majina ya Wagombea wa Viti Maalum na sii KUTEUA majina hayo lengo likiwa hawa ni Wawakilisha wa shauri na maoni ya WANAWAKE WOTE nchini katika mahitaji yao dhidi ya Mfumo Dume ambao awali maamuzi yote ya Kijamii yalifanywa na Wanaume bila kushauriwa na Wanawake. Na Hapa ndipo Upotoshaji wa viongozi wa kisasa unapotokana..
Hivyo basi, Wabunge wa viti maalum iwe WALEMAVU au WANAWAKE ni Wawakilishi wa makundi yao na sii Vyama vyao bali Chama kinapendeleza tu majina ya Wawakilishi na vema zaidi ifahamike pia viti Maalum vimewekwa kama sehemu ya kuvutia Wanawake kushiriki katika Siasa za nchi yetu (Affirmative action) na ndio maana hupitishwa Wanawake wa viti Maalum 1/3 ya Bunge letu.
Sasa inapotokea mvutano baina ya Vyama na Wawakilishi wa Wanawake aidha wamependekezwa na Chama cha Siasa au Laa, nadhani ipo haja kubwa sana ya kufanya marekebisho ya Katiba na Sheria hizi ili kuwapa WANAWAKE mamlaka zaidi ya kufanya Maamuzi wao badala ya kutegemea Vyama vya Siasa. Aidha vyama vya Wanawake vifanye uchaguzi wao au wateuane wao wenyewe kupitia Mabaraza yao na sii vinginevyo.
Tumesikia mengi bunge la 11 kuhusu unyanyasaji wa Wanawake ndani ya vyama vya Siasa. Viti maalum vikitumika kama rushwa na biashara ya Ngono na kadhalika, udhalilishaji wa Wanawake umefikia hatua ya viongozi kusahau hata malengo yake kwa jina la Vyama vya Siasa. Bila shaka tumefika wakati Wanawake nchini kuwa kitu kimoja kwa maslahi yao maana safari yao wote ni moja.
Walisema TUKIWEZESHWA TUNAWEZA sasa iweje leo nafasi za Viti Maalum ziwe kigezo kikubwa cha malumbano ya Kisiasa? Nashauri Kuundwa Chombo kimoja cha UMOJA wa WANAWAKE kupitisha majina ya Wawakilishi wao badala ya Uongozi wa Vyama ambao bado mfumo Dume umetamalaki.
Sheria zinazotoa Mwongozo kuhusu viti maalum ni pamoja na:-- Katiba; Sheria ya Taifa Ya Uchaguzi; na
Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2010 hivyo ni muhimu sana Wananchi wote kuzingatia kwa nini uwepo wa viti maalum Bungeni.
Imeelezwa bayana kuwa: - Viti maalum ni viti vilivyotengwa kwa mujibu wa sheria kuhakikisha kwamba watu au makundi ya watu wenye mahitaji maalum na ambao si rahisi kugombea Uchaguzi na kushinda kwa sababu ya hali yao (kama ulemavu na Uchache wao) wanapata nafasi ya kuwakilisha maoni na vipaumbele vyao katika ngazi tofauti za Uongozi (Bungeni, Wilayani, Halmashauri).
Kwa mujibu wa Sheria hizi, haya makundi yaloainishwa mpaka sasa katika bunge letu ni WANAWAKE na WALEMAVU. Na kwa upande wa Wanawake, Vyama vya Siasa vimepewa nafasi ya KUPENDEKEZA majina ya Wagombea wa Viti Maalum na sii KUTEUA majina hayo lengo likiwa hawa ni Wawakilisha wa shauri na maoni ya WANAWAKE WOTE nchini katika mahitaji yao dhidi ya Mfumo Dume ambao awali maamuzi yote ya Kijamii yalifanywa na Wanaume bila kushauriwa na Wanawake. Na Hapa ndipo Upotoshaji wa viongozi wa kisasa unapotokana..
Hivyo basi, Wabunge wa viti maalum iwe WALEMAVU au WANAWAKE ni Wawakilishi wa makundi yao na sii Vyama vyao bali Chama kinapendeleza tu majina ya Wawakilishi na vema zaidi ifahamike pia viti Maalum vimewekwa kama sehemu ya kuvutia Wanawake kushiriki katika Siasa za nchi yetu (Affirmative action) na ndio maana hupitishwa Wanawake wa viti Maalum 1/3 ya Bunge letu.
Sasa inapotokea mvutano baina ya Vyama na Wawakilishi wa Wanawake aidha wamependekezwa na Chama cha Siasa au Laa, nadhani ipo haja kubwa sana ya kufanya marekebisho ya Katiba na Sheria hizi ili kuwapa WANAWAKE mamlaka zaidi ya kufanya Maamuzi wao badala ya kutegemea Vyama vya Siasa. Aidha vyama vya Wanawake vifanye uchaguzi wao au wateuane wao wenyewe kupitia Mabaraza yao na sii vinginevyo.
Tumesikia mengi bunge la 11 kuhusu unyanyasaji wa Wanawake ndani ya vyama vya Siasa. Viti maalum vikitumika kama rushwa na biashara ya Ngono na kadhalika, udhalilishaji wa Wanawake umefikia hatua ya viongozi kusahau hata malengo yake kwa jina la Vyama vya Siasa. Bila shaka tumefika wakati Wanawake nchini kuwa kitu kimoja kwa maslahi yao maana safari yao wote ni moja.
Walisema TUKIWEZESHWA TUNAWEZA sasa iweje leo nafasi za Viti Maalum ziwe kigezo kikubwa cha malumbano ya Kisiasa? Nashauri Kuundwa Chombo kimoja cha UMOJA wa WANAWAKE kupitisha majina ya Wawakilishi wao badala ya Uongozi wa Vyama ambao bado mfumo Dume umetamalaki.