Kwanini viongozi wote wa serikali wasiwe mfano wa kupima kama wanatumia madawa ya kulevya?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Mimi nafikiri wakati umefika viongozi wa serikali wawe mfano wa utekelezeji wa operations zote zinazoanzishwa na serikali badala ya wao kubaki wahamasishaji tu bila ya wao wenyewe kushiriki kikamilifu na kwa vitendo kwa kuonyesha mfano.

Mfano zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma liliishia tu kwa watumishi wa kawaida ila sidhani kama viongozi wa juu wa serikali walihusika katika zoezi hili.

Sasa wameibuka na operation ya kuhisi watu fulani ama wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya au wanatumia madawa hayo na kuamua kuwapima na kutangaza hadharani matokeo.

Binafsi nafikiri wakati umefika kwa serikali kuonyesha mfano kwa vitendo na kwa kuanza viongozi wote wa juu waende wakapimwe kama wanatumia madawa haya na vipimo hivyo vifanywe na taasisi zisizo za kiserikali au zilizoko nje ya nchi na matokeo ya vipimo hivyo yatangazwe hadharani na kiongozi atakaebainika kutumia madawa hayo awajibike mara moja kwa kujiuzulu nafasi yake.

Na kama kweli tuko seriuos tutunge sheria inayomtaka kila mtu anaetaka kugombea naafasi mbali mbali za uongozi wa nchi hii shariti kwanza apimwe kama anatumia madawa hayo na akibainika kutumia basi sheria itamke wazi kuwa anakuwa amepoteza sifa ya kugombea nafasi yoyoye ile ya uongozi katika nchi hii.

Hili likitushinda basi tuache kufuatilia na kuwapima baadhi ya watu na badala yake tu-deal na wasambazi na wauzaji wa madawa haya.

Hivi nani kati yetu ana uhakika wote wanaokamata, wanaotoa maagizo watu wapimwe, wanaotoa taarifa za watumiaji na hata wanaopima kama wote hawa hakuna miongoni mwao anaetumia madawa haya?
 
Sio Madawa peke yake hadi vipimo vya akili vinakuja ukikutwa kichaa unaachia ngazi... na Tz kati ya wanne mmoja ni kichaa balaa Office zitakimbiwa
 
Mimi nafikiri wakati umefika viongozi wa serikali wawe mfano wa utekelezeji wa operations zote zinazoanzishwa na serikali badala ya wao kubaki wahamasishaji tu bila ya wao wenyewe kushiriki kikamilifu na kwa vitendo kwa kuonyesha mfano.

Mfano zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma liliishia tu kwa watumishi wa kawaida ila sidhani kama viongozi wa juu wa serikali walihusika katika zoezi hili.

Sasa wameibuka na operation ya kuhisi watu fulani ama wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya au wanatumia madawa hayo na kuamua kuwapima na kutangaza hadharani matokeo.

Binafsi nafikiri wakati umefika kwa serikali kuonyesha mfano kwa vitendo na kwa kuanza viongozi wote wa juu waende wakapimwe kama wanatumia madawa haya na vipimo hivyo vifanywe na taasisi zisizo za kiserikali au zilizoko nje ya nchi na matokeo ya vipimo hivyo yatangazwe hadharani na kiongozi atakaebainika kutumia madawa hayo awajibike mara moja kwa kujiuzulu nafasi yake.

Na kama kweli tuko seriuos tutunge sheria inayomtaka kila mtu anaetaka kugombea naafasi mbali mbali za uongozi wa nchi hii shariti kwanza apimwe kama anatumia madawa hayo na akibainika kutumia basi sheria itamke wazi kuwa anakuwa amepoteza sifa ya kugombea nafasi yoyoye ile ya uongozi katika nchi hii.

Hili likitushinda basi tuache kufuatilia na kuwapima baadhi ya watu na badala yake tu-deal na wasambazi na wauzaji wa madawa haya.

Hivi nani kati yetu ana uhakika wote wanaokamata, wanaotoa maagizo watu wapimwe, wanaotoa taarifa za watumiaji na hata wanaopima kama wote hawa hakuna miongoni mwao anaetumia madawa haya?
Ushauri wako una hitilafu:
1. Kwa kawaida mtu anapimwa kutaka kujua kama anatumia madawa ya kulevya kutafuta ushaidi kwa mfano kutaka kufahamu iwapo wanamichezo wanatumia madawa ya kusisimua misuli zenye athari ya ushindani, na
2. Watuhumiwa wa kutumia madawa:
(a) si busara na haki kuwatuhumu watu wholesomely.

(b) kwa kuwapima watumishi tu ni kuwanyanyapaa. Ikibidi watanzania wote wapimwe. Kipimo nadhani ni aghali, na
(c) Kupima kwa aina hiyo kutalenga kupata mafanikio gani? Udhibiti wa matumizi ufanyike au watu waathirike kwanza?
 
Uzi wako ni mzuri na una nia njema sana..

Ila nilikuwa nashauri kwa viongozi ambao ni wagombea ambao umependekeza wapimwe kama ni watumiaji wa madawa ya kulevya, kabla ya yote wapimwe kwanza AKILI ( ufanyaji kazi na ufanisi wa ubongo) kabla ya chochote kile.


Kuna dalili nyingi sana.. na hii ni kutokana na sheria zetu kuwa dhaifu tunaweza kuja kuongozwa na KICHAA.
 
Ushauri wako una hitilafu:
1. Kwa kawaida mtu anapimwa kutaka kujua kama anatumia madawa ya kulevya kutafuta ushaidi kwa mfano kutaka kufahamu iwapo wanamichezo wanatumia madawa ya kusisimua misuli zenye athari ya ushindani, na
2. Watuhumiwa wa kutumia madawa:
(a) si busara na haki kuwatuhumu watu wholesomely.

(b) kwa kuwapima watumishi tu ni kuwanyanyapaa. Ikibidi watanzania wote wapimwe. Kipimo nadhani ni aghali, na
(c) Kupima kwa aina hiyo kutalenga kupata mafanikio gani? Udhibiti wa matumizi ufanyike au watu waathirike kwanza?
Sijaona point ya kunishawishi hapo maana ukweli ni kuwa wengi tu huenda wanatumia hivyo nao wapimwe.

Huko tuendako jambo hili litakuja tu kuibuka na kufanyiwa kazi.
 
Back
Top Bottom