Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Imeandikwa kwenye Biblia takatifu, katika kitabu cha Mithali, sura ya 14:34 nanukuu kama ifuatavyo "Haki huliinua Taifa, Bali dhambi ni aibu ya watu wote" mwisho wa kunukuu.
Kwa maandiko hayo ya kwenye Biblia takatifu, maana yake ni kuwa huwezi kuitenganisha HAKI na AMANI na kwa maana nyingine vitu hivyo ni sawasawa na chanda na pete.
Hata hivyo tumekuwa tukiwasikia mara nyingi, viongozi wetu wa kidini wakituhimiza sana sisi waumini wetu tuidumishe amani ya nchi hii, tena wamekuwa wakienda mbali zaidi na kutuonya kuwa amani ya nchi hii ikitoweka, kuirejesha itakuwa ngumu sana!
Ndipo hapo ninapowauliza hao viongozi wa Dini, ambao naamini wao wanavisoma sana hivyo vitabu vya dini na wana uelewa mkubwa zaidi yetu sisi waumini wa madhehebu hayo, kuwa ni kwanini wanatusisitizia sana sisi waumini wao tudumishe amani ya nchi hii, lakini wanashikwa na "kigugumizi* kuwasisitizia sana viongozi wetu wa kisiasa, nao watimize wajibu wao muhimu sana wa kutenda haki, pale wanapolitumikia Taifa hili?
Hivi ni nani asiyejua kuwa viongozi wetu wa kisiasa, wanaziminya waziwazi HAKI za wananchi, wanapotekeleza majukumu yao?
Tunafahamu pia nchi yetu imepata msamiati mpya, katika utawala huu wa serikali ya awamu ya 5 ya " watu wasioujulikana" ambao haukuwepo katika awamu za serikali zilizopita!
Tunaambiwa na Jeshi letu la Polisi, kuwa waliomwua aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo, miaka zaidi ya 4 iliyopita, ni WATU WASIOJULIKANA. Kwa kuwa hadi Leo hawajapatikana na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Tunaelezwa pia na Jeshi letu la Polisi kuwa watu waliomteka, msaidizi wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeaman Mbowe, BenSaanane, zaidi ya miaka 4 iliyopita, ni WATU WASIOJULIKANA!
Tumejuliishwa pia na Jeshi letu la Polisi nchini, watu waliomteka, mwandishi wa habari maarufu nchini, Azory Gwanda, zaidi ya miaka 3 iliyopita, ni WATU WASIOJULIKANA!
Tunaelezwa pia na Jeshi letu la Polisi nchini kuwa watu waliomminia risasi mfululizo zaidi ya 15 mwilini mwake, mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu, eti na wao, ni WATU WASIOJULIKANA!
Tunaambiwa na Jeshi letu la Polisi nchini kuwa watu waliomteka, mfanyibiashara maarufu nchini, Mohamed Dewji, eti na hao ni WATU WASIOJULIKANA!
Matukio ya kuuawa watu, kutekwa na kupotea, ni mengi sana, katika utawala huu wa serikali ya awamu ya 5 na umevunja rekodi ya serikali zote za awamu zilizopita, tokea tupate Uhuru wetu!
Tumeshuhudia pia Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally, akitamba kuwa chama chake, kitaendelea kutumia vyombo vya dola vilivyopo nchini, ili kuendelea kubaki madarakani!
Hivi hayo maneno aliyoyatamka Dkt Bashiru Ally ni ya kuyatamka hadharani au ni ulevi tu wa madaraka?
Ni dhahiri kuwa maneno hayo aliyoyatamka Dkt Bashiru Ally hadharani, ndiyo yanayochochea kwa kiasi kikubwa, uvunjifu wa amani hapa nchini na kutaka kuikimbiza amani tuliyo kuwa nayo hapa nchini tokea tupate Uhuru wetu toka kwa mkoloni
Kwa maandiko hayo ya kwenye Biblia takatifu, maana yake ni kuwa huwezi kuitenganisha HAKI na AMANI na kwa maana nyingine vitu hivyo ni sawasawa na chanda na pete.
Hata hivyo tumekuwa tukiwasikia mara nyingi, viongozi wetu wa kidini wakituhimiza sana sisi waumini wetu tuidumishe amani ya nchi hii, tena wamekuwa wakienda mbali zaidi na kutuonya kuwa amani ya nchi hii ikitoweka, kuirejesha itakuwa ngumu sana!
Ndipo hapo ninapowauliza hao viongozi wa Dini, ambao naamini wao wanavisoma sana hivyo vitabu vya dini na wana uelewa mkubwa zaidi yetu sisi waumini wa madhehebu hayo, kuwa ni kwanini wanatusisitizia sana sisi waumini wao tudumishe amani ya nchi hii, lakini wanashikwa na "kigugumizi* kuwasisitizia sana viongozi wetu wa kisiasa, nao watimize wajibu wao muhimu sana wa kutenda haki, pale wanapolitumikia Taifa hili?
Hivi ni nani asiyejua kuwa viongozi wetu wa kisiasa, wanaziminya waziwazi HAKI za wananchi, wanapotekeleza majukumu yao?
Tunafahamu pia nchi yetu imepata msamiati mpya, katika utawala huu wa serikali ya awamu ya 5 ya " watu wasioujulikana" ambao haukuwepo katika awamu za serikali zilizopita!
Tunaambiwa na Jeshi letu la Polisi, kuwa waliomwua aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo, miaka zaidi ya 4 iliyopita, ni WATU WASIOJULIKANA. Kwa kuwa hadi Leo hawajapatikana na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Tunaelezwa pia na Jeshi letu la Polisi kuwa watu waliomteka, msaidizi wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeaman Mbowe, BenSaanane, zaidi ya miaka 4 iliyopita, ni WATU WASIOJULIKANA!
Tumejuliishwa pia na Jeshi letu la Polisi nchini, watu waliomteka, mwandishi wa habari maarufu nchini, Azory Gwanda, zaidi ya miaka 3 iliyopita, ni WATU WASIOJULIKANA!
Tunaelezwa pia na Jeshi letu la Polisi nchini kuwa watu waliomminia risasi mfululizo zaidi ya 15 mwilini mwake, mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu, eti na wao, ni WATU WASIOJULIKANA!
Tunaambiwa na Jeshi letu la Polisi nchini kuwa watu waliomteka, mfanyibiashara maarufu nchini, Mohamed Dewji, eti na hao ni WATU WASIOJULIKANA!
Matukio ya kuuawa watu, kutekwa na kupotea, ni mengi sana, katika utawala huu wa serikali ya awamu ya 5 na umevunja rekodi ya serikali zote za awamu zilizopita, tokea tupate Uhuru wetu!
Tumeshuhudia pia Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally, akitamba kuwa chama chake, kitaendelea kutumia vyombo vya dola vilivyopo nchini, ili kuendelea kubaki madarakani!
Hivi hayo maneno aliyoyatamka Dkt Bashiru Ally ni ya kuyatamka hadharani au ni ulevi tu wa madaraka?
Ni dhahiri kuwa maneno hayo aliyoyatamka Dkt Bashiru Ally hadharani, ndiyo yanayochochea kwa kiasi kikubwa, uvunjifu wa amani hapa nchini na kutaka kuikimbiza amani tuliyo kuwa nayo hapa nchini tokea tupate Uhuru wetu toka kwa mkoloni