Kwanini viongozi watokao CCM kwenda upinzani jamii inawaheshimu kuliko wapinzani kwenda CCM?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,795
71,214
Nimejaribu kufanya kautafiti nimegundua kiongozi au mwananchi wa kawaida anayetoka CCM na kujiunga kwenye siasa za upinzani anakuwa na heshima kubwa kwenye jamii kuliko wale watokao Upinzani na kujiunga CCM (wengi wanaita kuunga mkono juhudi).

Hebu tumwangalie kubwa lao Lowassa, alipojitoa CCM akapata heshima kubwa kwenye jamii hata hao CCM walikuwa wanambeza kumbe wanamtamani mno. Karudi huko hakuna anayemjali tena pamoja na kupokelewa kwa heshima zote za CCM.

Angalieni Waitara na Bulaya nani anaheshima katika jamii?

Kafulila sio Kafulila tena yule "tumbili" kiboko ya kutetea wanyonge. Ona Gekule kule Babati alivyokuwa mbunge wa Chadema na rafiki wa wanababati na alivyo sasa mbunge wa CCM na adui wa RAIA wa Babati?

Vipi Nyalandu baada ya kuutosa ubunge wa CCM? Mbona heshima imekuwa kubwa mno huwezi kumlinganisha na Dr Mkumbo au yule wa Siha?

Mifano ni mingi mno.
Swali linabaki kwa nini wanaokimbilia CCM wanaonekana ni NJAA TUU zinawaongoza?

Askofu Bagoza kasema ni vigumu kuwaongoza wenye njaa, nami nasema NI VIGUMU KUONGOZWA NA WENYE NJAA NA TAMAA.


 
Kuna sababu nyingi lkn baadhi yake ni hizi zifuatazo.

1:Wananchi au umma umeichoka sana ccm either kwa kukaa sana madarakani au kwa kushindwa kutimiza malengo na matarajio yao kama watawaliwa.

2:Kiongozi akiwa ndani ya ccm hujiona ni Mungu wa dunia hivyo akiamua kutoka huko kwenye ufalme na kujiunga huku upinzani ambako kila kukicha viongozi wake wanshinda mahakamani wananchi wanamuona huyo ni shujaa na kiongozi mkweli asiyehitaji kutukuzwa.

3:Ukiwa upinzani unakuwa umefunguliwa kutumia kipawa chako ulichopewa na Mungu na kukiongeza kupitia masomo.
Ukiwa ccm unakuwa umefungwa mdomoni kwa kufuri kubwa.

Kwangu hizi ni sababu
Nimejaribu kufanya kautafiti nimegundua kiongozi au mwananchi wa kawaida anayetoka CCM na kujiunga kwenye siasa za upinzani anakuwa na heshima kubwa kwenye jamii kuliko wale watokao Upinzani na kujiunga CCM (wengi wanaita kuunga mkono juhudi).
Hebu tumwangalie kubwa lao Lowassa, alipojitoa CCM akapata heshima kubwa kwenye jamii hata hao CCM walikuwa wanambeza kumbe wanamtamani mno. Karudi huko hakuna anayemjali tena pamoja na kupokelewa kwa heshima zote za CCM.
Angalieni Waitara na Bulaya nani anaheshima katika jamii?
Kafulila sio Kafulila tena yule "tumbili" kiboko ya kutetea wanyonge. Ona Gekule kule Babati alivyokuwa mbunge wa Chadema na rafiki wa wanababati na alivyo sasa mbunge wa CCM na adui wa RAIA wa Babati?
Vipi Nyalandu baada ya kuutosa ubunge wa CCM? Mbona heshima imekuwa kubwa mno huwezi kumlinganisha na Dr Mkumbo au yule wa Siha?
Mifano ni mingi mno.
Swali linabaki kwa nini wanaokimbilia CCM wanaonekana ni NJAA TUU zinawaongoza?
Askofu Bagoza kasema ni vigumu kuwaongoza wenye njaa, nami nasema NI VIGUMU KUONGOZWA NA WENYE NJAA NA TAMAA.

 
Jamii ya watanzania inataka siasa za kistaarabu zisizo na shaka wala kutia DOA usalama wetu na ni CCM pekee yenye kushiriki siasa za hivyo.

Jamii haiwezi kuukubali upinzani kwa sababu:
1. Miaka mingi siasa za upinzani zimekuwa zikiratibu migomo na maandamano yasiyo na tija na baada ya wananchi kupata uelewa wameukataa kabisa

2. kupinga na kubeza imekuwa ni nyenzo ya upinzani kusonga mbele awamu hii, wananchi wamechoshwa na kituko hiki.

3.Kila mtanzania mwenye akili timamu anashawishika na kuhamasika na yanayofanywa na CCM chini ya Rais Magufuli
 
Wanajua fika wapi yalipo makao makuu ya shetani,hata mbinguni ndivyo ilivyo pale mwana kondoo mmoja ukitubu na kuachana na dhambi Fraha na heshima hutamalaki mbele ya wenye haki,lakini mwanakondoo akitoka miongoni mwa watenda haki na kushikamana na waovu wingu jeusi na fadhaa huzikumba mbigu na sauti za ole husikika kila kona. Heshima itatoka wapi wakati ulieshikamana nae wanamjua!!!
Ni hayo tu ndugu zangu.
 
Wapo baadhi ya viongozi CCM ni wabaya kama ilivyo kwa baadhi ya viongozi walio kwenye vyama vya upinzani Siku akitokea mtu yeyote msafi na mwenye nia ya dhati ya kuwakomboa watanzania kwa kupitia chama chochote kile atapita kwa nguvu zote.Tatizo kila ukiwaangalia wanasiasa wengi unaona kabisa hawana dhamira ya kweli,wamejaa viburi kutengeneza chuki ubaguzi na upendeleo.
 
Jamii ya watanzania inataka siasa za kistaarabu zisizo na shaka wala kutia DOA usalama wetu na ni CCM pekee yenye kushiriki siasa za hivyo.

Jamii haiwezi kuukubali upinzani kwa sababu:
1. Miaka mingi siasa za upinzani zimekuwa zikiratibu migomo na maandamano yasiyo na tija na baada ya wananchi kupata uelewa wameukataa kabisa

2. kupinga na kubeza imekuwa ni nyenzo ya upinzani kusonga mbele awamu hii, wananchi wamechoshwa na kituko hiki.

3.Kila mtanzania mwenye akili timamu anashawishika na kuhamasika na yanayofanywa na CCM chini ya Rais Magufuli
Kwa hiyo mkuu una taka kupingana na post #7 hapo juu?
Mbona ufafanuzi wake uko very clear?
 
Ni kwa sababu...

Kutoka Upinzani na kuingia CCM ni sawa na kuchota maji bombani na kwenda kuyajazia baharini...



Cc: mahondaw
 
Jamii ya watanzania inataka siasa za kistaarabu zisizo na shaka wala kutia DOA usalama wetu na ni CCM pekee yenye kushiriki siasa za hivyo.

Jamii haiwezi kuukubali upinzani kwa sababu:
1. Miaka mingi siasa za upinzani zimekuwa zikiratibu migomo na maandamano yasiyo na tija na baada ya wananchi kupata uelewa wameukataa kabisa

2. kupinga na kubeza imekuwa ni nyenzo ya upinzani kusonga mbele awamu hii, wananchi wamechoshwa na kituko hiki.

3.Kila mtanzania mwenye akili timamu anashawishika na kuhamasika na yanayofanywa na CCM chini ya Rais Magufuli
Fala
 
Umemsahau silaaa.
Kweli, Dr Slaa ni mfano mkubwa. Yule wa Chadema alikuwa maarufu kwa watu na mfano wa kuigwa lakini huyu pamoja na kupewa Ubalozi ameshuka daraja toka Premier league Kwenda daraja LA nne.
Sasa hakuna anayejali awepo au asiwepo!
 
Nimejaribu kufanya kautafiti nimegundua kiongozi au mwananchi wa kawaida anayetoka CCM na kujiunga kwenye siasa za upinzani anakuwa na heshima kubwa kwenye jamii kuliko wale watokao Upinzani na kujiunga CCM (wengi wanaita kuunga mkono juhudi).

Hebu tumwangalie kubwa lao Lowassa, alipojitoa CCM akapata heshima kubwa kwenye jamii hata hao CCM walikuwa wanambeza kumbe wanamtamani mno. Karudi huko hakuna anayemjali tena pamoja na kupokelewa kwa heshima zote za CCM.

Angalieni Waitara na Bulaya nani anaheshima katika jamii?

Kafulila sio Kafulila tena yule "tumbili" kiboko ya kutetea wanyonge. Ona Gekule kule Babati alivyokuwa mbunge wa Chadema na rafiki wa wanababati na alivyo sasa mbunge wa CCM na adui wa RAIA wa Babati?

Vipi Nyalandu baada ya kuutosa ubunge wa CCM? Mbona heshima imekuwa kubwa mno huwezi kumlinganisha na Dr Mkumbo au yule wa Siha?

Mifano ni mingi mno.
Swali linabaki kwa nini wanaokimbilia CCM wanaonekana ni NJAA TUU zinawaongoza?

Askofu Bagoza kasema ni vigumu kuwaongoza wenye njaa, nami nasema NI VIGUMU KUONGOZWA NA WENYE NJAA NA TAMAA.



Ni kanuni ya Mungu kwamba malaika mmoja akijiunga na ma-Ibilisi analaniwa moja kwa moja na shetani akiamua kutubu anasamehewa na kibarikiwa.
 
Kweli, Dr Slaa ni mfano mkubwa. Yule wa Chadema alikuwa maarufu kwa watu na mfano wa kuigwa lakini huyu pamoja na kupewa Ubalozi ameshuka daraja toka Premier league Kwenda daraja LA nne.
Sasa hakuna anayejali awepo au asiwepo!
Amekuwa kama mechi za ndondo. Hahahaaa
 
Jamii ya watanzania inataka siasa za kistaarabu zisizo na shaka wala kutia DOA usalama wetu na ni CCM pekee yenye kushiriki siasa za hivyo.

Jamii haiwezi kuukubali upinzani kwa sababu:
1. Miaka mingi siasa za upinzani zimekuwa zikiratibu migomo na maandamano yasiyo na tija na baada ya wananchi kupata uelewa wameukataa kabisa

2. kupinga na kubeza imekuwa ni nyenzo ya upinzani kusonga mbele awamu hii, wananchi wamechoshwa na kituko hiki.

3.Kila mtanzania mwenye akili timamu anashawishika na kuhamasika na yanayofanywa na CCM chini ya Rais Magufuli
Bado hujajibu hoja za mleta mada, jaribu tena.
 
Nimejaribu kufanya kautafiti nimegundua kiongozi au mwananchi wa kawaida anayetoka CCM na kujiunga kwenye siasa za upinzani anakuwa na heshima kubwa kwenye jamii kuliko wale watokao Upinzani na kujiunga CCM (wengi wanaita kuunga mkono juhudi).

Hebu tumwangalie kubwa lao Lowassa, alipojitoa CCM akapata heshima kubwa kwenye jamii hata hao CCM walikuwa wanambeza kumbe wanamtamani mno. Karudi huko hakuna anayemjali tena pamoja na kupokelewa kwa heshima zote za CCM.

Angalieni Waitara na Bulaya nani anaheshima katika jamii?

Kafulila sio Kafulila tena yule "tumbili" kiboko ya kutetea wanyonge. Ona Gekule kule Babati alivyokuwa mbunge wa Chadema na rafiki wa wanababati na alivyo sasa mbunge wa CCM na adui wa RAIA wa Babati?

Vipi Nyalandu baada ya kuutosa ubunge wa CCM? Mbona heshima imekuwa kubwa mno huwezi kumlinganisha na Dr Mkumbo au yule wa Siha?

Mifano ni mingi mno.
Swali linabaki kwa nini wanaokimbilia CCM wanaonekana ni NJAA TUU zinawaongoza?

Askofu Bagoza kasema ni vigumu kuwaongoza wenye njaa, nami nasema NI VIGUMU KUONGOZWA NA WENYE NJAA NA TAMAA.





Kama wewe ni mwislaamu au mkristo halafu ukasikia mtu mmoja amekimbia kutoka kwa shetani mtekaji, muuji, mdhulumaji, mbabikiaji wa kesi za uongo, mla watu, mpiga watu risasi n.k. akaongoka na kuwa mwislaamu au mkristo na mwingine ukasikia kajisajili kwa ibilisi, wewe binafsi nani utampa heshima?
 
Back
Top Bottom