G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Viongozi wanaojitapa kuishinda Corona ni wale wale ambao kwenye kila tukio hujitokeza na kupiga makelele kweli huku wakitunisha vifua ila baadaye wanakuja kufeli vibaya sana wakati uhalisia unapojidhihirisha.
Wakati kwenye hili jambo la Corona tayari tumeacha siasa zitawale uhalisia, wameibuka wale wale wakiongozwa na Rais Magufuli wakisema kuwa wameishinda Corona. Ni wale wale kina Paul Christian Makonda, Palamagamba Kabudi na baadhi ya wapotoshaji wengine wa ukweli. Mbaya zaidi kwenye hili wanaonyesha dhahiri siasa zao za uongo mchana kweupeeee vila hata ya aibu.
Unatangaza vipi umeishinda vita wakati mwanzoni tu mwa vita ulitundika silaha kwenye mabega ukatoka nduki? Unamdanganya nani kwenye dunia hii asiye na akili? Tofauti na huko nyuma uongo umekuwa tukielezwa sisi watanzania, leo uongo wanaelezwa dunia ya watu wenye kila aina ya vifaa kuthibitisha upotoshaji wetu.
Sasa huko kwa majirani tu tunaumbuliwa mchana kweupe huku ndani tukiendelea kupiga zumari. Haitachukua muda tutatumia muda wetu mwingi kupambana na uongo wetu. Tuombe uzima ila tusije tena kuambiana tuungane mkono, sijui hii ni vita ya nchi! Litakuwa la kwenu wenyewe!
Ni wajibu wa wizara husika ya afya kuachwa ifanye kazi kwa uweledi maana hii ni dunia ambayo Corona kwenye kiipambania wengi wamelipa kipaumbele cha kipekee. Hizi siasa hazina umbali mrefu ohooo.
Wakati kwenye hili jambo la Corona tayari tumeacha siasa zitawale uhalisia, wameibuka wale wale wakiongozwa na Rais Magufuli wakisema kuwa wameishinda Corona. Ni wale wale kina Paul Christian Makonda, Palamagamba Kabudi na baadhi ya wapotoshaji wengine wa ukweli. Mbaya zaidi kwenye hili wanaonyesha dhahiri siasa zao za uongo mchana kweupeeee vila hata ya aibu.
Unatangaza vipi umeishinda vita wakati mwanzoni tu mwa vita ulitundika silaha kwenye mabega ukatoka nduki? Unamdanganya nani kwenye dunia hii asiye na akili? Tofauti na huko nyuma uongo umekuwa tukielezwa sisi watanzania, leo uongo wanaelezwa dunia ya watu wenye kila aina ya vifaa kuthibitisha upotoshaji wetu.
Sasa huko kwa majirani tu tunaumbuliwa mchana kweupe huku ndani tukiendelea kupiga zumari. Haitachukua muda tutatumia muda wetu mwingi kupambana na uongo wetu. Tuombe uzima ila tusije tena kuambiana tuungane mkono, sijui hii ni vita ya nchi! Litakuwa la kwenu wenyewe!
Ni wajibu wa wizara husika ya afya kuachwa ifanye kazi kwa uweledi maana hii ni dunia ambayo Corona kwenye kiipambania wengi wamelipa kipaumbele cha kipekee. Hizi siasa hazina umbali mrefu ohooo.