Kwanini viongozi na wafuasi wa CHADEMA wanashindwa kukiri kuwa wamepoteza Kata ya Tanga Songea?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimefuatilia mijadala juu ya matokeo ya Udiwani katika kata 20 na Ubunge wa Dimani. Nilichojifunza katika mijadala hiyo ni kwamba, CHADEMA na UKAWA wanakufa na Tai Shingoni. Wanajifariji huku wanateketea. Wanaumia ila wanajifanya wana tabasamu. Wanapigwa ila wanajifanya wakakamavu.

Mtakumbuka kuwa kwenye uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, Kata ya Tanga iliyopo Manispaa ya Songea ilichukuliwa na Mussa Ndomba wa CHADEMA. Hata hivyo, baada ya kuona kuwa CHADEMA hakipo kwa maslahi ya Watanzania, Ndomba aliamua kujiunga na CCM na hivyo kupoteza Udiwani. Mtakumbuka kuwa Mussa Ndomba amekabidhiwa kadi ya CCM tarehe 7 Januari 2017 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipofanya ziara mkoani Ruvuma.

Kutokana na uwezo wa Mussa Ndomba, CCM walimpa nafasi ya kugombea Udiwani kwenye uchaguzi wa Marudio wa Januari 22 akiwa na muda wa siku 15 tu ndani ya CCM. Hata hivyo, Wana Tanga walimwamini na wakampa kura za kishindo kuliko zile alizopata akiwa CHADEMA Oktoba 2015.

Nawashangaa sana UKAWA. Pamoja na CCM kutwaa kata hiyo ya Tanga, tumewapora pia kata nyingine kule Mkoa wa Tanga ambayo ilikuwa inashikiliwa na chama mwanachama wa UKAWA, CUF. Kwa hali hiyo, CCM tumeweza kutetea viti vyetu 17 na kuwapora UKAWA kata 2 na hivyo kutufanya kuibuka kidedea kwa kata 19.

Hivi CHADEMA wanajua kweli hesabu? Au wanafanya makusudi ili kuficha aibu? Kwa nini hawataki kukiri kuwa CCM ni baba lao? Kwa nini huyu UKAWA anakosa adabu kwa mzazi wake?

Endeleeni kujifariji. Tukutane 2020.
image.jpg
 
HBARI ndeeeeeeeefu.. matokeo yalishatoka na kila mtu anajua, ccm furahia na wengine waache wajipange..
 
Kata ya Tanga Songea CCM hawaitaki hata kuskia na safari hii wametumia umafia wa kila aina ili kata hii irudi kwao.
Na huyo Mussa usaliti wake dhidi ya wananchi wa Tanga atakuja juta tuu siku.
 
Kata ya Tanga Songea CCM hawaitaki hata kuskia na safari hii wametumia umafia wa kila aina ili kata hii irudi kwao.
Na huyo Mussa usaliti wake dhidi ya wananchi wa Tanga atakuja juta tuu siku.
Mkuu, kwa nini sasa mnaficha kusema bayana kuwa CHADEMA mmepoteza Kata hiyo? Mbona hili lipo bayana!
 
Kumbe Tundu Lissu ni Muongo sana!

Akihojiwa na DW ya Ujerumani Alisema Chadema imefanikiwa kukomboa kata yake moja Kumbe walikuwa na kata Mbili moja wameirudisha CCM
 
Mkuu, kwa nini sasa mnaficha kusema bayana kuwa CHADEMA mmepoteza Kata hiyo? Mbona hili lipo bayana!
Unaelewa nachoeleza kweli hiyo kata CCM hawaitaki sio vijana wala wazee wake kwa waume.
Wanachuki kubwa sana dhidi ya CCM ni hila ovu tu zinazowabeba mnazotumia ili kujipa ushindi .
 
Ni kwa sababu jamaa ni waongo na wazandiki sana. Sasa naamua kuwavua nguo mchana kweupe

Unajivua nguo mwenyewe.Tuletee Tume huru halafu usitumie wale jamaa wanaoitwa polisi wala wakurugenzi makada wa CCM.

Pili tuletee analysis wangapi waliipigia kura CCM 2015 na wangapi waliipigia CCM 2017.Msiwe mnapiga kelele wakati hata ngoma hamjui kuicheza.
 
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu amesema matokeo ya uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani hayawakatishi tamaa 2020
 
Hata ile kata ya Arusha si ilikuwa ya Diwani wa CDM aliyefariki, acha waendelee kujifariji, 2020 ndio watapigwa vizuri na kutambua Lowasa ni asset au liability.
 
Back
Top Bottom