Kwanini vijana wengi wa CCM wanatetea siasa chafu za Sabaya?

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,272
47,268
Vijana wengi hasa wasio na ajira waliingia CCM sio kwa kukipenda chama bali kutafuta ridhiki na ajira za upendeleo ndani ya chama na serikali, huku role models wao wakubwa wakiwa akina Makonda, Polepole, Hapi, Mwigulu, Gambo, Sabaya, Murro, Shaka, Musiba, Habibu na wengine wengi.

Mienendo na tabia ya uongozi wa vijana niliowataja ilijulikana wazi ambayo ilikuwa ubabe, jeuri, fitina, dhulma, utekaji, mauaji nk, walitumia mbinu hizi hasa kuwadhalilisha wapinzani, wakosoaji na wafanyabiashara, wakajiona wao ndio Tanzania na Tanzania ni wao, wakasahau kuwa aliyewapa madaraka na jeuri hizo hana garantii na Mungu.

Kipindi cha utawala wa Mwendazake ili uteuliwe sifa kuu mojawapo ilikuwa ubabe, roho mbaya, matusi, jeuri, ilifikia wakati mwana CCM au polisi akimvunja mguu mpinzani anapongezwa pengine kupandishwa cheo.

Vijana wengi wa CCM wakaanza kuiga matendo na vituko vya akina Sabaya & Co, siasa chafu ambazo uchafu wake hata waonyeshwe kwenye video wanajifanya hawauoni, wakaiga vituko hivi ili waonekane wawafurahishe wakubwa zao wateuliwe, leo wameanza kukata tamaa baada ya kuona Mama hana siasa hizo chafu.

Baada ya kugundua hilo wanachofanya sasa ni kuwatetea role models wao wanaotenguliwa ambao walikuwa wateule wa mwendazake (Bashiru, Polepole, Biswalo, Sabaya), wameanza kumlaumu Mama wakitumia ilani ya chama kama ngao yao kuwa mama anaonyesha kushindwa kuitekeleza, huku lengo kuu ni kutaka kumshinikiza mama aendeleze ubabe wa mtangulizi wake siasa ambazo walitegemea kuja kunufaika nazo.

CCM Mwacheni Mama afanye kazi msimshinikize zamu ya Mwendazake imekwisha. Kazi iendelee.
 
Hao ni wachumia tumbo wasio na maadili. hawana hata chembe ya adabu...walikuwa wanaona raha kuwadhalilisha wazee hadharani. Wakae kwa kutulia chama kinarudi katika misingi yake ya utu na kuheshimiana.
Ally Hapi aliwatuka wazee ambao ni baba zake , babu zake bila aibu wa haya mdomoni wala rohoni.... Nashangaa mama hajamtema. Huyu kijana alikuwa nadhani na bado Jeuri. Apigwe chini..
 
Siasa chafu kwao ziliweza kuwapa chakula, wanachanganyikiwa kwa sasa Mama sio muumini wa siasa hizo. Ukizoea vya kunyoga vya kuchinja hutaviweza. Mbaya zaidi kichwani ni hamnazo wengi wao wanauwezo mdogo kichwani. Zama zimebadilika hawajui ima wamejitoa ufahamu. Siasa za maono, itikadi, falsafa za chama nk kwao ni giza totoro.
 
Zile siasa za awamu ya 5 ulikuwa ni uwendawazimu wa hali ya juu. Uongozi ule ulikuwa ni uchafu na laana kwa Taifa.

Tumeliharibu Taifa kwa miaka 5. Lakini ninaamini Mungu alikuwa na makusudi yake kuruhusu utawala dhalimu wa kiasi kile uje na udumu kwa miaka 5. Ametukumbusha kuwa bila katiba nzuri, nini kinaweza kuwapata wananchi na Taifa.

Walaaniwe viongozi dhalimu wote, na Mungu aendelee kudhihirisha ukuu wake dhidi yao.

Enyi waovu tubuni, fanyeni toba iliyo kuu ili mpokee msamaha wa Mungu, au la ninyi na wana wenu ishini katika laana maisha yenu yote.
 
Vijana wengi hasa wasio na ajira waliingia CCM sio kwa kukipenda chama bali kutafuta ridhiki na ajira za upendeleo ndani ya chama na serikali, huku role models wao wakubwa wakiwa akina Makonda, Polepole, Hapi, Mwigulu, Gambo, Sabaya, Murro, Shaka, Musiba, Habibu na wengine wengi.

Mienendo na tabia ya uongozi wa vijana niliowataja ilijulikana wazi ambayo ilikuwa ubabe, jeuri, fitina, dhulma, utekaji, mauaji nk, walitumia mbinu hizi hasa kuwadhalilisha wapinzani, wakosoaji na wafanyabiashara, wakajiona wao ndio Tanzania na Tanzania ni wao, wakasahau kuwa aliyewapa madaraka na jeuri hizo hana garantii na Mungu.

Kipindi cha utawala wa Mwendazake ili uteuliwe sifa kuu mojawapo ilikuwa ubabe, roho mbaya, matusi, jeuri, ilifikia wakati mwana CCM au polisi akimvunja mguu mpinzani anapongezwa pengine kupandishwa cheo.

Vijana wengi wa CCM wakaanza kuiga matendo na vituko vya akina Sabaya & Co, siasa chafu ambazo uchafu wake hata waonyeshwe kwenye video wanajifanya hawauoni, wakaiga vituko hivi ili waonekane wawafurahishe wakubwa zao wateuliwe, leo wameanza kukata tamaa baada ya kuona Mama hana siasa hizo chafu.

Baada ya kugundua hilo wanachofanya sasa ni kuwatetea role models wao wanaotenguliwa ambao walikuwa wateule wa mwendazake (Bashiru, Polepole, Biswalo, Sabaya), wameanza kumlaumu Mama wakitumia ilani ya chama kama ngao yao kuwa mama anaonyesha kushindwa kuitekeleza, huku lengo kuu ni kutaka kumshinikiza mama aendeleze ubabe wa mtangulizi wake siasa ambazo walitegemea kuja kunufaika nazo.

CCM Mwacheni Mama afanye kazi msimshinikize zamu ya Mwendazake imekwisha. Kazi iendelee.
Vijana wengi wa siku hizi hawajui tofauti ya mema na mabaya, wengi wapo tayari kutembea uchi bila kuona shida yoyote.
 
Vijana wengi hasa wasio na ajira waliingia CCM sio kwa kukipenda chama bali kutafuta ridhiki na ajira za upendeleo ndani ya chama na serikali, huku role models wao wakubwa wakiwa akina Makonda, Polepole, Hapi, Mwigulu, Gambo, Sabaya, Murro, Shaka, Musiba, Habibu na wengine wengi.

Mienendo na tabia ya uongozi wa vijana niliowataja ilijulikana wazi ambayo ilikuwa ubabe, jeuri, fitina, dhulma, utekaji, mauaji nk, walitumia mbinu hizi hasa kuwadhalilisha wapinzani, wakosoaji na wafanyabiashara, wakajiona wao ndio Tanzania na Tanzania ni wao, wakasahau kuwa aliyewapa madaraka na jeuri hizo hana garantii na Mungu.

Kipindi cha utawala wa Mwendazake ili uteuliwe sifa kuu mojawapo ilikuwa ubabe, roho mbaya, matusi, jeuri, ilifikia wakati mwana CCM au polisi akimvunja mguu mpinzani anapongezwa pengine kupandishwa cheo.

Vijana wengi wa CCM wakaanza kuiga matendo na vituko vya akina Sabaya & Co, siasa chafu ambazo uchafu wake hata waonyeshwe kwenye video wanajifanya hawauoni, wakaiga vituko hivi ili waonekane wawafurahishe wakubwa zao wateuliwe, leo wameanza kukata tamaa baada ya kuona Mama hana siasa hizo chafu.

Baada ya kugundua hilo wanachofanya sasa ni kuwatetea role models wao wanaotenguliwa ambao walikuwa wateule wa mwendazake (Bashiru, Polepole, Biswalo, Sabaya), wameanza kumlaumu Mama wakitumia ilani ya chama kama ngao yao kuwa mama anaonyesha kushindwa kuitekeleza, huku lengo kuu ni kutaka kumshinikiza mama aendeleze ubabe wa mtangulizi wake siasa ambazo walitegemea kuja kunufaika nazo.

CCM Mwacheni Mama afanye kazi msimshinikize zamu ya Mwendazake imekwisha. Kazi iendelee.
Hawawezi siasa za ushindani wanaweza ubabe kama muasisi wao jiwe
 
Ally Hapi aliwatuka wazee ambao ni baba zake , babu zake bila aibu wa haya mdomoni wala rohoni.... Nashangaa mama hajamtema. Huyu kijana alikuwa nadhani na bado Jeuri. Apigwe chini..
Tulia mkuu, zamani zetu kulikuwa na usemi "slow but sure" umesharudi naona.
Nani alijua Sabaya yatamfika haya? Maana kipigo sio kutenguliwa tuu bali kuchunguzwa.
Na Ole wao wachunguzi wajifanye kuficha mambo, wajue aliye agiza uchunguzi sio Retired au Chakaza watamvunga, huyo ni Rais kawatuma na anaweza kutuma wengine kuwachunguza na wao.
Hapi na wengine wangejiandaa tu kisaikolojia
 
Zile siasa za awamu ya 5 ulikuwa ni uwendawazimu wa hali ya juu. Uongozi ule ulikuwa ni uchafu na laana kwa Taifa.

Tumeliharibu Taifa kwa miaka 5. Lakini ninaamini Mungu alikuwa na makusudi yake kuruhusu utawala dhalimu wa kiasi kile uje na udumu kwa miaka 5. Ametukumbusha kuwa bila katiba nzuri, nini kinaweza kuwapata wananchi na Taifa.

Walaaniwe viongozi dhalimu wote, na Mungu aendelee kudhihirisha ukuu wake dhidi yao.

Enyi waovu tubuni, fanyeni toba iliyo kuu ili mpokee msamaha wa Mungu, au la ninyi na wana wenu ishini katika laana maisha yenu yote.
Huwa najiuliza bila Mungu kuingilia kati sijui tungefikaje 2025.
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom