Kwanini utawala wa Nyerere ulikumbwa na misukosuko mingi ukilinganisha na utawala wa Mwinyi, Mkapa na wengine?

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,291
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salamu, ningependa nijielekeze kwenye mada husika. Ndugu zangu watanzania, baba yetu wa Taifa mwl Julius K Nyerere aliiongoza nchi yetu kwa muda wa miaka 25. Kwa muda wote huo wa uongozi wake, nchi yetu ilikumbwa na misuko suko mingi ambayo haikuja kutokea katika tawala zingine. Mfano wakati wa utawala wa Nyerere tuliona majaribio mawili ya mapinduzi yalioshindwa, hali iliyopelekea mzee wetu aamue kung'atuka mwenyewe kabla haja ng'atuliwa, maana kwa hali ya nchi ilivyokuwa kipindi kile bila shaka mwenyewe aliona kwamba asingeweza kumaliza miaka mingine mitano akiwa madarakani.

Lakini pia ukiachana na hayo ya mapinduzi pia kulikuwa na misuko suko mingine, mfano yale mauaji yaliosababisha waziri wa mambo ya ndani wa wakati ule mzee wetu mh Ally H Mwinyi kujiuzulu uwaziri. Pia kulikuwa na misuko suko mingine iliyopelekea kina mzee Kawawa, bibi Tito Mohammed na wengineo kufungwa jela. Lakini kama hiyo haitoshi, wapo waliamua kukimbia hata nchi na kwenda kuishi ughaibuni, mfano mzee wetu hayati Oscar Kambona na wengineo.

Hapo sijagusia ukosefu wa vitu muhimu nchini kama vile chakula, mafuta ya kupikia na ya taa, ukosefu wa madawa hospitalini, usafiri kuwa washida mpaka yakaletwa yale magari yalioitwa chai maharage, mzunguko wa pesa mtaani ukawa wa mdondo. Nguo, viatu, soksi, mafuta ya kupaka, sabuni navyo vikawa havipatikani.

Cha kushangaza alipoondoka mwl Nyerere na kuingia Mwinyi, hali ilibadilika kwa kiasi kikubwa. Hakuna aliethubutu kuwaza tena mapinduzi, bidhaa zote muhimu zilipatikana kwa urahisi mitaani. Mzunguko wa pesa ukawa mkubwa, mitumba ya nguo, viatu, soksi kila kona, madawa yakawa mengi hospitalini mpaka watu wakaamua kufungua na zahanati zao. Pia hakuna aliewaza tena kukimbia nchi, isipokuwa tuliishuhudia wale waliokimbia utawala wa kwanza wanaaza kurejea katika utawala huu wa pili nk.

Hali hii aliyoanza nayo Mwinyi, naona imeendelea hadi leo. Je, ni kwanini misuko suko ilikuwa zaidi wakati wa awamu ya kwanza na sio awamu zingine? Je mwl Nyerere alihujumiwa au sera zake mwenyewe ndio zili muhujumu? Inamaana mzee Mwinyi kwa kutumia uwezo wake na cheo chake aliweza kulisuka vizuri jeshi letu na kurejesha utiifu wao kwa serikali yao na raisi wao? Je inamanaa Mwinyi hakuwa na maadui wa kuitingisha serikali yake, hadi kupelekea wengine kukimbia kama walivyokimbia awamu ya kwanza? Mwenye kujua zaidi sababu zilizopelekea mwl Nyerere kushindwa kuituliza hali, hadi kuamua kung'atuka anakaribishwa kutujuza. Asanteni sana kwa kunisoma?
 
Hapa kuna jambo zuri umeandika, inaonekana sera za ujamaa za Nyerere ndio zilisababisha hasira za baadhi ya wananchi.

Matokeo yake uhaba wa kupatikana mahitaji muhimu ya binadamu ndio ilikuwa chanzo kikuu, mfano sabuni nk.

Lakini sasa nashindwa kuelewa, kama watanzania wa wakati ule walikuwa wameamka kwanini hiki kizazi cha sasa kimelala?

Tunaona baadhi ya wanajeshi walitaka kumpindua, hii maana yake jeshi lilikuwa na macho ya kuona hali halisi ilivyokuwa kwenye jamii ya watanzania.

Vipi kizazi hiki jeshi halioni tatizo lolote? au kuna heshima ya kinafiki ya uoga kati ya jeshi letu na viongozi wa serikali?

Naandika hivi kwasababu naamini hata sasa kuna mengi yanayotakiwa kufanyika ili nchi yetu irudi kwenye mstari wake, mojawapo la msingi zaidi ni utii wa sheria zetu toka kwa viongozi wa serikali Rais akiwa mkuu wao.
 
Misukosuko Mingi ya awamu ya kwanza ilitokana na kufeli kwa siasa na uchumi wa kijamaa hapa Tanzania na Duniani.

Misukosuko mingine ni kawaida tu labda useme uchokozi wa Iddi Amini uliopelekea vita ,ila tofauti na hapo mambo almost ni yale yale
Shukrani mkuu kwa kutuwekea kile unachokijua kuhusu uongozi ule wa awamu ya kwanza. Bila shaka washauri wake pia hawakuwa wazuri, maana walishindwa kumshauri mwl asome alama za nyakati kuhusiana na siasa za kijamaa.
 
Hapa kuna jambo zuri umeandika, inaonekana sera za ujamaa za Nyerere ndio zilisababisha hasira za baadhi ya wananchi.

Matokeo yake uhaba wa kupatikana mahitaji muhimu ya binadamu ndio ilikuwa chanzo kikuu, mfano sabuni nk.

Lakini sasa nashindwa kuelewa, kama watanzania wa wakati ule walikuwa wameamka kwanini hiki kizazi cha sasa kimelala?

Tunaona baadhi ya wanajeshi walitaka kumpindua, hii maana yake jeshi lilikuwa na macho ya kuona hali halisi ilivyokuwa kwenye jamii ya watanzania.

Vipi kizazi hiki jeshi halioni tatizo lolote? au kuna heshima ya kinafiki ya uoga kati ya jeshi letu na viongozi wa serikali?

Naandika hivi kwasababu naamini hata sasa kuna mengi yanayotakiwa kufanyika ili nchi yetu irudi kwenye mstari wake, mojawapo la msingi zaidi ni utii wa sheria zetu toka kwa viongozi wa serikali Rais akiwa mkuu wao.
Mmmmh.. waswahili wanasema ukionacho chongo, wenzio hukiona kengeza. Haya unayoyaona ww kuwa ni mabaya. Kuna wengine wanayaona mazuri, au hawaoni ubaya wala uzuri wake.
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salamu, ningependa nijielekeze kwenye mada husika. Ndugu zangu watanzania, baba yetu wa Taifa mwl Julius K Nyerere aliiongoza nchi yetu kwa muda wa miaka 25. Kwa muda wote huo wa uongozi wake, nchi yetu ilikumbwa na misuko suko mingi ambayo haikuja kutokea katika tawala zingine. Mfano wakati wa utawala wa Nyerere tuliona majaribio mawili ya mapinduzi yalioshindwa, hali iliyopelekea mzee wetu aamue kung'atuka mwenyewe kabla haja ng'atuliwa, maana kwa hali ya nchi ilivyokuwa kipindi kile bila shaka mwenyewe aliona kwamba asingeweza kumaliza miaka mingine mitano akiwa madarakani.

Lakini pia ukiachana na hayo ya mapinduzi pia kulikuwa na misuko suko mingine, mfano yale mauaji yaliosababisha waziri wa mambo ya ndani wa wakati ule mzee wetu mh Ally H Mwinyi kujiuzulu uwaziri. Pia kulikuwa na misuko suko mingine iliyopelekea kina mzee Kawawa, bibi Tito Mohammed na wengineo kufungwa jela. Lakini kama hiyo haitoshi, wapo waliamua kukimbia hata nchi na kwenda kuishi ughaibuni, mfano mzee wetu hayati Oscar Kambona na wengineo.

Hapo sijagusia ukosefu wa vitu muhimu nchini kama vile chakula, mafuta ya kupikia na ya taa, ukosefu wa madawa hospitalini, usafiri kuwa washida mpaka yakaletwa yale magari yalioitwa chai maharage, mzunguko wa pesa mtaani ukawa wa mdondo. Nguo, viatu, soksi, mafuta ya kupaka, sabuni navyo vikawa havipatikani.

Cha kushangaza alipoondoka mwl Nyerere na kuingia Mwinyi, hali ilibadilika kwa kiasi kikubwa. Hakuna aliethubutu kuwaza tena mapinduzi, bidhaa zote muhimu zilipatikana kwa urahisi mitaani. Mzunguko wa pesa ukawa mkubwa, mitumba ya nguo, viatu, soksi kila kona, madawa yakawa mengi hospitalini mpaka watu wakaamua kufungua na zahanati zao. Pia hakuna aliewaza tena kukimbia nchi, isipokuwa tuliishuhudia wale waliokimbia utawala wa kwanza wanaaza kurejea katika utawala huu wa pili nk.

Hali hii aliyoanza nayo Mwinyi, naona imeendelea hadi leo. Je, ni kwanini misuko suko ilikuwa zaidi wakati wa awamu ya kwanza na sio awamu zingine? Je mwl Nyerere alihujumiwa au sera zake mwenyewe ndio zili muhujumu? Inamaana mzee Mwinyi kwa kutumia uwezo wake na cheo chake aliweza kulisuka vizuri jeshi letu na kurejesha utiifu wao kwa serikali yao na raisi wao? Je inamanaa Mwinyi hakuwa na maadui wa kuitingisha serikali yake, hadi kupelekea wengine kukimbia kama walivyokimbia awamu ya kwanza? Mwenye kujua zaidi sababu zilizopelekea mwl Nyerere kushindwa kuituliza hali, hadi kuamua kung'atuka anakaribishwa kutujuza. Asanteni sana kwa kunisoma?
Hakuna wa kumlinganisha na Nyerere katika awamu zote. Amekuta pori akaanza kufyeka, kung'oa visiki halafu unauliza kwa nini wakati wake alikutana na nyoka wengi? Labda tukuulize kwa nini Nigeria hakuna mapinduzi Kama ilivyokuwa 60/70/80 na 80s? Nao walikuwa wajamaa?
 
Hahaha.. kivipi mkuu, hebu fafanua kidogo.
Yule si alikuwa anaongea maneno mengi sana huku utekelezaji hakuna,misemo na nahau zisizoisha..

Alikuwa hapendi ukosoaji na hataki changamoto za wasomi ndio maana hakutaka kusambaza elimu kwa watu wengi,aliwafanga watu wengi kuwa wajinga Ili awatawale kirahisi.

Miaka 25 ya utawala alichofanikiwa kikubwa ni kujenga utaifa na yeye binafsi kuwa muadilifu ila hakuna succession aliyofanya na aliondoka madarakani kutokana na Hali mbaya ya uchumi na sera zake mbovu za Uchumi..
 
Mkuu mimi nimeleta mada yenye maswali kadhaa ili nijibiwe, sasa na wewe unanirudishia maswali yangu 😀😀😂😂
Pole mkuu. Nchi nyingi za kiafrika zilipata uhuru bila ya kuwa na human resources za uhakika za kusaidia uendeshaji wa serikali.
Muda mfupi baada ya nchi hizi kupata uhuru, zilijikuta zikiendelea kutegemea resources za kikoloni kama jeshi, mahakama na hata katiba.
Mwaka 1964 jeshi lilipoasi moja ya sababu kubwa lilipinga kuongozwa na wazungu. Kumbuka mpaka tunapata uhuru, jeshi lilikuwa chini CDF mzungu Brigedia Douglas, na wakati huo jeshi lilikuwa likiitwa KAR-Kings African Rifles. Na ndilo lililoasi mwaka 1964 kwa madai ya kupinga kuongozwa na wazungu na kutaka nyongeza ya mshahara. Mwalimu alitafuta msaada akianzia Kenya na baadaye Uganda na alikuta kote hali ni tete ni Kama wanajeshi waliambiana.
Ilimlazimu kuomba msaada uingereza ambako alipata msaada wa makomandoo 60 na ndio walifanikiwa kuzima uasi 1964. Na baadaye Mwalimu alivunja jeshi lote na kuanza kuunda upya chini ya Cdf wa kwanza wakati Kanali Hagai Mirisho Sarakikya na inasemekana kulikuwa na wanajeshi watatu tu wenye elimu za kijeshi kutoka vyuo vilovyoheshika Kama Sandhurst Uingereza. Mwalimu aliunda jeshi tulilonalo sasa JWTZ. Sasa history ni ndefu Sina hakika naweza kueleza yote, hata hivyo uasi ulitokea tukiwa hatuna itikadi ya ujamaa na utaona nchi nyingi za kiafrika zilizopata Uhuru miaka hiyo bila kujali itikadi zao zilipitia pagumu Sana hususani Africa ya magharibi.
Wakati kina Mwinyi wanaongia mambo yalikuwa yamebadilika Sana, angalau human resources ilikuwa imeongezeka, jeshi limestabilize na hata mahakama.
Lakini viongozi pia kutokana na waliyopitia bila shaka walijawa na woga, na siku zote mtu akiwa muoga hata maamuzi mengi yatakuwa na sura ya kujihami. Nadhani wengine wataongezea au kusahihisha.
 
Yule si alikuwa anaongea maneno mengi sana huku utekelezaji hakuna,misemo na nahau zisizoisha..

Alikuwa hapendi ukosoaji na hataki changamoto za wasomi ndio maana hakutaka kusambaza elimu kwa watu wengi,aliwafanga watu wengi kuwa wajinga Ili awatawale kirahisi.

Miaka 25 ya utawala alichofanikiwa kikubwa ni kujenga utaifa na yeye binafsi kuwa muadilifu ila hakuna succession aliyofanya na aliondoka madarakani kutokana na Hali mbaya ya uchumi na sera zake mbovu za Uchumi..
Oh hapo nimekupata mkuu, sijui kwa upande wa wengine.
 
Pole mkuu. Nchi nyingi za kiafrika zilipata uhuru bila ya kuwa na human resources za uhakika za kusaidia uendeshaji wa serikali.
Muda mfupi baada ya nchi hizi kupata uhuru, zilijikuta zikiendelea kutegemea resources za kikoloni kama jeshi, mahakama na hata katiba.
Mwaka 1964 jeshi lilipoasi moja ya sababu kubwa lilipinga kuongozwa na wazungu. Kumbuka mpaka tunapata uhuru, jeshi lilikuwa chini CDF mzungu Brigedia Douglas, na wakati huo jeshi lilikuwa likiitwa KAR-Kings African Rifles. Na ndilo lililoasi mwaka 1964 kwa madai ya kupinga kuongozwa na wazungu na kutaka nyongeza ya mshahara. Mwalimu alitafuta msaada akianzia Kenya na baadaye Uganda na alikuta kote hali ni tete ni Kama wanajeshi waliambiana.
Ilimlazimu kuomba msaada uingereza ambako alipata msaada wa makomandoo 60 na ndio walifanikiwa kuzima uasi 1964. Na baadaye Mwalimu alivunja jeshi lote na kuanza kuunda upya chini ya Cdf wa kwanza wakati Kanali Hagai Mirisho Sarakikya na inasemekana kulikuwa na wanajeshi watatu tu wenye elimu za kijeshi kutoka vyuo vilovyoheshika Kama Sandhurst Uingereza. Mwalimu aliunda jeshi tulilonalo sasa JWTZ. Sasa history ni ndefu Sina hakika naweza kueleza yote, hata hivyo uasi ulitokea tukiwa hatuna itikadi ya ujamaa na utaona nchi nyingi za kiafrika zilizopata Uhuru miaka hiyo bila kujali itikadi zao zilipitia pagumu Sana hususani Africa ya magharibi.
Wakati kina Mwinyi wanaongia mambo yalikuwa yamebadilika Sana, angalau human resources ilikuwa imeongezeka, jeshi limestabilize na hata mahakama.
Lakini viongozi pia kutokana na waliyopitia bila shaka walijawa na woga, na siku zote mtu akiwa muoga hata maamuzi mengi yatakuwa na sura ya kujihami. Nadhani wengine wataongezea au kusahihisha.
Shukrani kwa ufafanuzi mzuri mkuu. Kwa mujibu wa maelezo yako, bila shaka Nyerere ameongoza nchi katika kipindi kigumu sana hasa kwa nchi zetu za kiafrika ndo maana yalitokea yale yaliotokea.
 
Hali hii aliyoanza nayo Mwinyi, naona imeendelea hadi leo. Je, ni kwanini misuko suko ilikuwa zaidi wakati wa awamu ya kwanza na sio awamu zingine?
Swali lako lipo wazi sana.

Anzia na serikali ngapi zilikuwa zinapinduliwa na jeshi miaka hiyo; halafu utapata mwendelezo wa vurugu nyingi ambazo hayo matatizo unayoyafikiria kwa Tanzania nchi nyingine yalikuwa ni majanga tupu.

Hata hiyo hali ya utulivu unayoisema baada ya Nyerere, wewe unadhani ilianzia wapi? Unadhani ilidondoka tu toka mbinguni?
 
Yule si alikuwa anaongea maneno mengi sana huku utekelezaji hakuna,misemo na nahau zisizoisha..

Alikuwa hapendi ukosoaji na hataki changamoto za wasomi ndio maana hakutaka kusambaza elimu kwa watu wengi,aliwafanga watu wengi kuwa wajinga Ili awatawale kirahisi.

Miaka 25 ya utawala alichofanikiwa kikubwa ni kujenga utaifa na yeye binafsi kuwa muadilifu ila hakuna succession aliyofanya na aliondoka madarakani kutokana na Hali mbaya ya uchumi na sera zake mbovu za Uchumi..
Kawaulize makaburu na wareno popote walipo habari za "Nyerere kusema maneno tu" kama watakubaliana na wewe.
Nyinyi watu wengine vichwa ni kama mmejaza takataka tu!

"Alikuwa hapendi ukosoaji", wa kipumbavu? Hukusikia/kuona mijadala ya mambo mbalimbali yaliyokuwa yakifanyika ndani ya chama katika ngazi zote toka juu hadi shinani?
Weka ushahidi wa ukosoaji unaousema hakuupenda tuone kama ulikuwa ni wa kijinga.

"Kujenga utaifa", hata kama lingekuwa hilo tu, wewe huoni kwamba ni jambo muhimu, pengine kushinda mengine yote? Lakini si hivyo tu, leo unakuja hapa unasahau baba yako alipata elimu na mengi mengine ambayo asingeyapata chini ya ukoloni; halafu leo unakuja hapa na kujifanya wewe mjuaji.
Hata kama ungekuwa mjuaji, bado ungekuwa mjuaji wa kipumbavu kama hujui chimbuko la ujuaji wako huo lilitokana na nini.

Lakini najua napoteza muda wangu tu hapa na "skunk", asiyejua lolote maishani mwake.
 
Kawaulize makaburu na wareno popote walipo habari za "Nyerere kusema maneno tu" kama watakubaliana na wewe.
Nyinyi watu wengine vichwa ni kama mmejaza takataka tu!

"Alikuwa hapendi ukosoaji", wa kipumbavu? Hukusikia/kuona mijadala ya mambo mbalimbali yaliyokuwa yakifanyika ndani ya chama katika ngazi zote toka juu hadi shinani?
Weka ushahidi wa ukosoaji unaousema hakuupenda tuone kama ulikuwa ni wa kijinga.

"Kujenga utaifa", hata kama lingekuwa hilo tu, wewe huoni kwamba ni jambo muhimu, pengine kushinda mengine yote? Lakini si hivyo tu, leo unakuja hapa unasahau baba yako alipata elimu na mengi mengine ambayo asingeyapata chini ya ukoloni; halafu leo unakuja hapa na kujifanya wewe mjuaji.
Hata kama ungekuwa mjuaji, bado ungekuwa mjuaji wa kipumbavu kama hujui chimbuko la ujuaji wako huo lilitokana na nini.

Lakini najua napoteza muda wangu tu hapa na "skunk", asiyejua lolote maishani mwake.
Na wewe uliwahi kuvaa viraka na kuimba zidumu fikra sahihi za Mwenyekiti? 😂😂

Naona Babu umetokwa povu sio la Nchi hii.
 
Sera za ujamaa hazikuwa mbaya ila Kambarage alipoteza mapato ya nchi kusaidia wengine wapate uhuru wewe fikiria kule Kongwa walikuwa wanalishwa tu bure bure na hizo nchi kwa Sasa hazina hata shukrani kwa Watanzania ,unakijua kisa Cha Kambarage kuuza Meli ya serikali kimyakimya na Sokoine akataka kumtumbua bosi wake.
 
Back
Top Bottom