GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,464
- 108,619
Siyo Siri tena na nadhani sasa kuna ' Fukuto ' kubwa kabisa linalozidisha ' bifu ' kali kati ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group Bwana Ruge Mutahaba na Watu walio karibu na wawili hawa wanasema kwamba Kitendo kile cha Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli kuwakutanisha pale Mkoani Tanga kama sijakosea ndiyo Kwanza kimezidisha ' bifu ' lao.
Leo nilitaka tujikite kabisa kwamba ni kwanini pamoja na juhudi zote zile za Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli kuwakutanisha huku akiwataka wamalize tofauti zao lakini walionyesha tu ukaribu wao pale pale na ndani ya siku tatu hadi wiki moja na baadae ' bifu ' lao likaendelea hadi hivi leo?
Je wawili hawa kwa Kitendo chao cha kuliendeleza ' bifu ' lao kunatuma ujumbe gani / upi hasa kwa Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli ambaye alijitahidi kuwapatanisha huku akidhani ameshamaliza tatizo lao lakini leo hii lipo pale pale tena sasa likiwa limechua sura mpya?
Je kulikuwa na umuhimu wowote labda kwa Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli awaite na kuwapatanisha wote mubashara ( live ) pale pale katika ule Mkutano wake Mkoani Tanga au ilimbidi awaite tu kimya kimya Ikulu Kwake ili aweze kusikiliza malalamiko yao mmoja mmoja kisha Yeye kama Baba na Kiongozi awasuluhishe tu huko huko bila Wananchi ( Sisi ) kujua?
Nimalizie tu kwa kuwaambia akina Makonda na Mutahaba kwamba wakae wakijua huu muendelezo wao wa ' mabifu ' wakati walishasuluhishwa tena na Kiongozi Mkuu kabisa wa nchi unamdhalilisha sana Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli na si jambo la Kiungwana hata kidogo na nijuavyo hasa katika Mila zetu za Kiafrika Mtu mzima akiwapatanisha Vijana basi mnatakiwa siku hiyo hiyo mumalize tofauti zenu na amani, upendo na utulivu vitamalaki.
Paul Makonda na Ruge Mutahaba mmemuangusha sana Mheshimiwa Rais wa JMT Dr. Magufuli. Badilikeni!
Nawasilisha.
Leo nilitaka tujikite kabisa kwamba ni kwanini pamoja na juhudi zote zile za Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli kuwakutanisha huku akiwataka wamalize tofauti zao lakini walionyesha tu ukaribu wao pale pale na ndani ya siku tatu hadi wiki moja na baadae ' bifu ' lao likaendelea hadi hivi leo?
Je wawili hawa kwa Kitendo chao cha kuliendeleza ' bifu ' lao kunatuma ujumbe gani / upi hasa kwa Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli ambaye alijitahidi kuwapatanisha huku akidhani ameshamaliza tatizo lao lakini leo hii lipo pale pale tena sasa likiwa limechua sura mpya?
Je kulikuwa na umuhimu wowote labda kwa Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli awaite na kuwapatanisha wote mubashara ( live ) pale pale katika ule Mkutano wake Mkoani Tanga au ilimbidi awaite tu kimya kimya Ikulu Kwake ili aweze kusikiliza malalamiko yao mmoja mmoja kisha Yeye kama Baba na Kiongozi awasuluhishe tu huko huko bila Wananchi ( Sisi ) kujua?
Nimalizie tu kwa kuwaambia akina Makonda na Mutahaba kwamba wakae wakijua huu muendelezo wao wa ' mabifu ' wakati walishasuluhishwa tena na Kiongozi Mkuu kabisa wa nchi unamdhalilisha sana Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli na si jambo la Kiungwana hata kidogo na nijuavyo hasa katika Mila zetu za Kiafrika Mtu mzima akiwapatanisha Vijana basi mnatakiwa siku hiyo hiyo mumalize tofauti zenu na amani, upendo na utulivu vitamalaki.
Paul Makonda na Ruge Mutahaba mmemuangusha sana Mheshimiwa Rais wa JMT Dr. Magufuli. Badilikeni!
Nawasilisha.