Kwanini ulikuwa unampa GF wako hela - ni tabia mbaya?

Kitu kidogo kilikuwa na mpaka sasa kinachukuliwa kama kiimarisha urafiki. Lakini kwa gf wa siku hizi, kwa kiasi kikubwa mambo yako tofauti sana
 
Husninyo;1825597]kweli ila kumpa hela gf wako kila baada ya kusex sio kitendo kizuri kabisa.Tena inaleta picha mbaya zaidi kama mwanaume huwa humsaidii/humpi hela gf wako siku zingine, siku umepewa utamu ndio unamwaga hela. Lol!

Siyo haki kusema mwanaume ndo anapewa utamu kwakweli, Husninyo unathibitisha hili kuwa raha anaisikia mwanaume peke yake wakati nyie ndo mnapiga na makelele kwa kunogewa?
 
[I said:
Wakumwitu;1825704]Kuna ma girl friend wengine wanakela jamani. Yeye kila ukikutana naye anachowaza ni kupewa hela. Hata kama umempa jana leo akija atalia hana hela. Mpaka wakati mwingine unajiuliza huyu anamatatizo gani? Yaani haoni aibu uso mkavu kama wa mbuzi. Na gear yake sasa yaani ile hela umenipa jana nimefanya hivi na vile leo yaani sina hela ya matumizi kabisa. Hapo anatarajia sympathy yako umpatie tena. Usipompa anauna na simu hupigiwi, au hata message hatumi. Ukimpigia umuulize kulikoni. Utasikia si nilikuambia toka jana sina hela. Kweli wanaume wakati mwingine tunageuzwa ATM, hata ya NMB ina afadhali. Kazi kwelikweli[/I]

Wa hivyo GF mbona anaonekana yupo kibiashara zaidi? Mie nisingewezana naye kwa kweli maana tabiya hiyo ningeikemea mapema zaidi. Na zaidi huyo atakuwa hakubendi bali kukutumia. Inamaana kama hauna basi msijuane, wa nini sasa unless na wewe unaye kibiasha zaidi.
 
Mbona mie nampa haka kajamaa hivi kumbe yeye ndo anatakiwa atoe :help::help::help:
 
Mzee mwanakijiji kwa thread hii inaonekana GF wako alikufaidi sana yaani ulikuwa unampa kila akija kwako pesa? za nini kila siku au alikuwa anakwambia shida fulani? mimi nakumbuka nilikuwa nikiwa nina shida fulani naitoa labda kabla ya wiki au mbili then ndio nipewe pesa nadhani inategemea na msichana uliyekuwa nae kwa kipindi hicho
 
mwanakijiji kumsaidia gf ni part ya majukumu ya mwanaume anaekwepa kufanya hivyo labda ni kwa sababu hana kabisa au ubahili au uchoyo.

Una point ndugu Wit lakini pale tu wahusika wana uhusiano uliorasmishwa mfano baba kwa binti/watoto na mke au mume kwa mke.Pale wote wanafanya kazi au wana kipato nadhani ni haki kabisa wahudumiane.Unaweza kukuta mwanamke ana kipato zaidi ya mwanaume, lakini BF atajiumiza sana ili atimize hili jukumu batili!

Hata kisheria, pale mwanamke ana uwezo basi anawajibika kumtunza mumewe.Akina kaka/baba mjue mna haki kutunzwa na wake zenu! Hivyo acheni kutumia pesa kama chambo, kinga na rungu.
 
ukiona wa hivyo na wewe stuka! Mtu gani amekalia kuomba kila siku,sikatai kuwa matatizo hayabishi hodi but not to that extent!na kwa nini anune!enzi anazozisemea mwanakijiji wasichana walikuwa hawana demand ya hivyo lkn due to moral changes things now is upside down,zamani mtoto wa kike alikuwa na haya kidogo hata akisaidiwa anaona soni lkn sasa hivi we press order like huh!! Ila inapendeza pia kuona kuwa mwanaume ana play part in supporting
Hili neno WiseLady!

Mi najiuliza, kwanini siku hizi ni HAPENDWI MTU BALI POCHI???
Je siyo wanaume wenyewe wanaendekeza hili?
 
Hili neno WiseLady!

Mi najiuliza, kwanini siku hizi ni HAPENDWI MTU BALI POCHI???
Je siyo wanaume wenyewe wanaendekeza hili?
Kama wenyewe wanakubaliwa kwa kuhonga unadhani mbeleni ndo hawatotakiwa kuendeleza?Wajifunze kua wakweli ili wakubalike kwa walivyo na sio pochi zao...otherwise wataendelea kutumika mpaka wachakae!
 
Hili neno WiseLady!

Mi najiuliza, kwanini siku hizi ni HAPENDWI MTU BALI POCHI???
Je siyo wanaume wenyewe wanaendekeza hili?

WOS tatizo linakuja pale mwanaume anapoingia kwa gia ya pesa na galz wanakubali kwa kigezo hicho,kwa maana ya kwamba inawezekana kabisa kukawa hakuna upendo wa kweli hapo ila ni influence ya pesa ikasababisha mapenzi,,,mahusiano ya aina hiyo ndo unakuta kila siku ni kuombana pesa mwisho inakuwa kero kwa mwanaume na kusahau kuwa chanzo ni yeye alitanguliza pesa iongee kwa niaba yake.

Msome lizzy hapa;
Kama wenyewe wanakubaliwa kwa kuhonga unadhani mbeleni ndo hawatotakiwa kuendeleza?Wajifunze kua wakweli ili wakubalike kwa walivyo na sio pochi zao...otherwise wataendelea kutumika mpaka wachakae!

Lizzy umenena vema,siongezi neno.
 
Una point ndugu Wit lakini pale tu wahusika wana uhusiano uliorasmishwa mfano baba kwa binti/watoto na mke au mume kwa mke.Pale wote wanafanya kazi au wana kipato nadhani ni haki kabisa wahudumiane.Unaweza kukuta mwanamke ana kipato zaidi ya mwanaume, lakini BF atajiumiza sana ili atimize hili jukumu batili!

Hata kisheria, pale mwanamke ana uwezo basi anawajibika kumtunza mumewe.Akina kaka/baba mjue mna haki kutunzwa na wake zenu! Hivyo acheni kutumia pesa kama chambo, kinga na rungu.

Nakubaliana na wewe kabisa maisha ni kusaidiana kila mmoja kuona kuwa ana jukumu kwa mwenzake,hili la wanaume kutumia chambo cha pesa ili kunasa mabinti nalo halina ubishi! Point yangu ni kuwa mwanaume kama kichwa cha nyumba asisahau majukumu yake,asifanye kama anahonga bali iwe ni sehemu ya kuonyesha kujali,inatufurahisha sana pia pale tunapoona mwanamke anamjali mwanaume hata kwa kidogo alicho nacho! Ukweli ina mvuto wa pekee sana
 
Unfortunately for me I dated only agemates so I didn't expect anything in return ...the man I married is also my agemate... We both were doing same job...equal salary..so I didn't expect any pampering except on birthdays and valentines....

nice msg Nsiande, personally naona culture ya kutoa kutoa kwa gf everytime ni old culture, pale ambapo mfumo dume ulikuwa in practice, kwa sasa hivi wamewezeshwa so kama hilo lipo na wote tuna hali moja issue inakuwa kusaidiana or kugawana majukumu....Gf wangu na mimi tunasaidiana, hatupeani pesa ila tunasaidiana services, kwenye daladala kila mtu anataka awahi kulipa nauli za wote..everything ni pamoja, tuna malengo ya kuanza maisha kwa apartment na kujenga nyumba pamoja!! this is 21st century!!!!!!!! yale kama mzee wa kijiji anavyoongelea ni mambo ya long time!!! mwanamke mchunaji anayetafuta buzi badala ya mpenzi ni ambao Beijing aijawasaidia...bado hawajaendelea na kutambua hali ya sasa ya kimaisha!!! Wapenzi ni a team!!! siku hizi ni kusaidiana na si kuchunana!!!!!
 
Wengine hatujabahatika kupewa pesa na boyfriend lol...au tuna mikosi?

Mnaopewa pesa na maboifrend hebu mnihabarishe manafanyaje au mnatumia mbinu gani?

Mkaka unayetoa pesa unasukumwa na nini?
 
Nilikuwa na mjadala na rafiki yangu mmoja siku chache zilizopita kuhusiana na tabia ambayo miaka hiyo ya 47 tulikuwa hatuchukulii kwa namna yoyote mbaya na ambayo bado inaendelea kwa namna moja au nyingine. Kulikuwa na tabia kwamba ukiwa na GF wakati ule wa shule basi alikuwa anakutegemea kwa matumizi madogomadogo.

Hivyo, akija kwako alikuwa anatarajia kuwa ataondoka na "chochote" na kwa kweli "mkikutana" bila "kupeana" chochote ilikuwa ni kama jambo lisilo la kawaida. Hii tabia iliendelea lakini ilikuwa ni tofauti kwa wale ambao walikuwa kama kwenye boarding schools ambapo hela zilikuwa zinakuja kwa mgao toka kwa familia kama mgao wa Tanesco. Huko boarding school mtu na gf wake walikuwa wanategemeana mmoja akipata chochote basi mwingine naye alikuwa ananeemeka..


Heshima Muzee ya Kijiji!!

Kwenye msisitizo mwekundu kwani wakati huo ulikuwa na umri gani? Ulikuwa unafanya kazi na yeye mwanafunzi au??

Kwenye bluu, "kupeana chochote" inamaanisha nini, yeye alikuwa anakupa nini ndipo nawe ulazimike kumpa pesa?
 
Back
Top Bottom