Kwanini ukimsifia Rais Magufuli CHADEMA wananuna na kutoa dhihaka - Wanahitaji Elimu?

Kabende Msakila

JF-Expert Member
Oct 7, 2020
1,382
1,246
WanaJF, Salaam!

Nimefuatilia kwa takriban miaka sita (6) hivi humu kwenye jamvi huru la siasa. Ukijitokeza kusifia, kuunga mkono jitihada za Serikali inapofanya jambo zuri i.e Ujenzi wa vivuko Busisi - Sengerema, ujenzi wa barabara za lami, ujenzi wa vituo vya afya, uteuzi wa wapinzani, maridhiano ya kitaifa Zanzibar nk nk.

Kwa hayo na mengine mengi ukitokea hadharani na kuyasifia ukweli ni kwamba hawa jamaa wa CDM wanaudhika kweli - wanajaa gesi na hapo unashushiwa dhihaka kibao kama:

(i). Lumumba buku saba - sasa Je, wao wanaposifia Tundu Lissu au Mbowe huwa mmepewa Ufipa kiloba?

(ii). Weka namba ya simu chini ili uteuliwe (as if Serikali ina nafasi ya kuteua kila mtanzania mwenye hisia na mawazo chanya) - Je, ninyi mnaposifia CHADEMA huwa mnafanya hivyo ili chama cha Mbowe kiwateue?

(iii). Wauaji, watekaji na wakandamizaji wa haki za binadamu - hivi huwa mnasahau kwamba ukandamizaji mmeuasisi huko CHADEMA - CCM tumebadili wenyeviti wa taifa mara kadhaa, CHADEMA mmebadili mara ngapi? Mmeshajiuliza kwa nini Silinde, Waitara, Katambi, Dkt Kaburou, Zitto, Dkt. Slaa, Dkt Mashinji, Lijualikali na wengine wengi waliamua kuwaacha?

Nihitimishe kwa kusema kwamba si kwamba Paskali Mayyala, Msakila Kabende nk kuunga mkono jitihada za Serikali ni kutaka teuzi "NO". Things are always clear kwamba Serikali ya JPM iko makini sehemu zote na imeweza kujibu maswali mengi ya upinzani kama dhana ya ufisadi, uwajibikaji, matumizi ya fedha za umma nk

Asubuhi njema wanachadema, ACT-Wazalendo, CUF, NLD, UDP, NCCR nk.

Msakila M Kabende
Kigoma
Tanzania
 

Kabende Msakila

Ndugu yangu, hivi Umekwisha jiuliza chanzo chake kwa miaka yote hiyo sita au uliamua tu kupotezea? Chanzo chake ni Wizi wa kura miaka nenda rudi.​

Wenye nchi- wananchi wanajua kwamba adhabu ya vibaka na wezi ni kuwamwagiliwa madumu ya petrol na kuchomwa, wezi wa kukwapua heleni za akina mama wanapigwa kipigo cha mbwa mwizi , wanaobomoa nyumba kwa fatuma wanajua adhabu yao wakikamatwa.

Sasa , achilia mbali Chadema, watu wamechoshwa na wizi wa aina yeyote ile... na huu wizi wa kura hawajajua tu namna bora ya kuukomesha, siku wakijua, watakiwasha nchi nzima... inasadika na wengi kwamba ccm na system wanashirikiana kuiba au kufanya magumashi kwenye uchaguzi (ni dhana iliyo tapakaa kila sehemu) halafu wanataka watu wake kimya tu... watu wana hasira sana mioyoni mwao isipokuwa tu hawajapata njia ya kukomesha huu umagumashi wa wizi wa kura na kuchakachua matokeo... hivyo chochote kinachotoka na wizi huo hakipendwi achilia mbali hizi habari za kusifia mtu anayetokana na wizi...hata yeye sio kosa lake... ni basi tu labda hajui...

Ipo siku wenye nchi wakijua namna bora ya kukomesha wizi wa kura, mziki wake watausikia tu hata wakiwa makaburini....
 
Unfortunately kuna kikundi cha watu haswa upinzani hua wanajiona wamepatia maisha na kuita wengine wajinga! wao wanadhan sku CCM itatoka CCM basi yaisha yao yataboreka, wapuuzi wa mwisho kabisa hawa!

Mtu anasema chanzo cha umaskini tanzania ni ccm kuwepo madarkani apo apo hajiamini kama anaweza kwenda kufanya kazi nje ya nchi yeye serikali ndo mwisho wa kilio chake, WTF!
 
Mimi nakushangaa wewe ambaye unahangaika na mawazo ya watu ambao unawajua uwezo wao kifikra.

Nakushauri usihangaike na comment za watu wajinga jinga kama wewe sio mjinga!

Kukwazwa na comment za watu wajinga hata wewe utaonekana ni mjinga!

Wewe weka mada yako, acha wachangiaji wachangie wanavyotaka/kupenda. Kwa kufanya hivyo utakuwa umetimiza waiibu wako!
 
unfortunately kuna kikundi cha watu haswa upinzani hua wanajiona wamepatia maisha na kuita wengine wajinga! wao wanadhan sku ccm itatoka ccm basi yaisha yao yataboreka, wapuuzi wa mwisho kabisa hawa! mtu anasema chanzo cha umaskini tanzania ni ccm kuwepo madarkani apo apo hajiamini kama anaweza kwenda kufanya kazi nje ya nchi yeye serikali ndo mwisho wa kilio chake, WTF!
Watu wamekatishwa tamaa na mambo mengi.. kwa wale wanaojua mziki au msururu wa documents za kuombea passport ya Tanzania wanjua habari yake.. sasa hiyoi tu passport halafu ukisha ipata bado tena msururu wa visa ya kazi kwenye ubalozi husika.. watu wanataka urahisi wa maisha na watamchukia yeyote anayekwamisha mambo yao.. haijalishi ni CHADEMA, CCM au nguchiro... wao wanataka mambo yao yaende bila mkwaruzo na ndio maana frustration zao zinaishia huko kwa wana siasa na vyama vyao
 
Watu wamekatishwa tamaa na mambo mengi.. kwa wale wanaojua mziki au msururu wa documents za kuombea passport ya Tanzania wanjua habari yake.. sasa hiyoi tu passport halafu ukisha ipata bado tena msururu wa visa ya kazi kwenye ubalozi husika.. watu wanataka urahisi wa maisha na watamchukia yeyote anayekwamisha mambo yao.. haijalishi ni CDM, ccm au nguchiro... wao wanataka mambo yao yaende bila mkwaruzo na ndio maana frustration zao zinaishia huko kwa wana siasa na vyama vyao
This is a very normal process, unless ni nchi yenye visa onn arrival process ni ile ile
 
Mimi nafikiri wanachadema wanaomsifia Tundu Lisu kwa nyimbo, mapambio na mashairi, na kupinga mikakati ya raisi JPM ya kuua tabia ya kutegemea misaada toka nje, wanahitaji kusoma historia ya wazungu jinsi walivyokuja Africa miaka iliyopita walivyowatenda babu zetu nk.

Wanachadema wakasome historia ya maisha ya watu weusi waliyokua wakiishi kabla na baada ya wazungu kuingia Africa, wakimaliza kusoma wafanye tathmini kwa kina, huenda itawasaidia kuelewa kuwa wazungu ni watu wa aina gani, na ni kwann wanatawala karibia dunia nzima.
 
Kabende Msakila
Ndugu yangu, hivi Umekwisha jiuliza chanzo chake kwa miaka yote hiyo sita au uliamua tu kupotezea? Chanzo chake ni Wizi wa kura miaka nenda rudi...

Siyo wizi wa kura "miaka nenda rudi" kwa sababu magufuli alisimama mwaka 2015 tu, na CHADEAM wakaanza kununa tangu hapo; haya matokeo ya 2020 ni muendelezo ule wa kununa.

Sababu kubwa ni kuwa Magufuli aliwafutia sera zao zote. Sera kuu za Chadema zilikuwa ni kulaumu kuwa serikali haifanyi mambo ya muhimu ikiwa ni pamoja na kuendeleza huduma za afya na elimu vijijini, kupigana na ufisadai, kufufua ATCL, kufufua reli na kuondoa ukiritimba serikalini, kueneza umeme vijinini, barabara vijijini. Jamaa akafanya yote hayo na kuwaacha CHADEMA hawana la kusema, ndiyo maana wakamchukuia na kuanza kuzipinga sera hizo hizo walizokuwa wakijidai kusimamia.
 
1607382350643.png
 
Kabende Msakila
Ndugu yangu, hivi Umekwisha jiuliza chanzo chake kwa miaka yote hiyo sita au uliamua tu kupotezea? Chanzo chake ni Wizi wa kura miaka nenda rudi...
Hakuna uchaguzi usio na wizi duniani. Nyie pia ni wezi wa kura. Sema mnaiba 5 hadi 10 tu. Wenzenu wanapiga ndefu. Poleni kwa kulia na be jua bila kukimbilia kivulini. Akili ndogo Kama ya kenge.
 
Wako sahihi kutokana na nafasi yao katika serikali na taifa kwa ujumla {wapinzani} japo kuwa mpinzani haimaniishi upinge kila kitu🤔🤔

#jr
 
Hakuna uchaguzi usio na wizi duniani. Nyie pia ni wezi wa kura. Sema mnaiba 5 hadi 10 tu. Wenzenu wanapiga ndefu. Poleni kwa kulia na be jua bila kukimbilia kivulini. Akili ndogo Kama ya kenge.
“Akili ndogo kama ya kenge”- ulimpimia wapi hizo akili na Kwa kutumia kip IMO gani au ni maoni yako...
Unaposema, “ nyie pia ni wezi wa kura”- maana yake kuiba ni sawa au una maana gani mkuu?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom