Kwanini Tundu Lissu na CHADEMA wanachukia maendeleo Kanda ya Ziwa?

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

Ukiwasikiliza na kusoma makala za Tundu Lissu na CHADEMA ni dhahiri wanatoa ujumbe kuwa eneo la Kanda ya Ziwa lisingestahili kuwa na chochote, naam wanaichikia Kanda ya Ziwa na kupinga maendeleo yake kitu ambacho ni hatari na wanapaswa kuadhidhibiwa kwenye sanduku la kura. Kwa ufupi:

Tumeshuhudia meli mpya na ukarabati wa meli za zamani kwa Ziwa Tanganyika, Nyasa na Victoria lakini Tundu na Chadema wananuna na Mv Victoria.

Tumeshihudia ujenzi wa viwanja vya ndege zaidi ya 11 vipya na kuweka rada Kilimnjaro, Mbeya na Mwanza. Lakini Tundu na Chadema wanachukia uwanja wa Chato na rada ya uwanja wa Mwanza.

Kumejengwa madaraja kadhaa juu ya mito na bahari ikiwemo Salender na Kigamboni lakini Tundu Lissu na Chadema wanachukia daraja la busisi.

Kumejengwa bandari kadhaa kwenye Ziwa Tanganyika, Nyasa na Victoria lakini Tundu Lissu na Chadema wamekasirishwa na ujenzi wa gati ya Musoma iliyopo Mwigobero.

Chuki hii ya Tundu na Chadema inayopandikizwa dhidi ya kanda ya Ziwa itawacharaza.
 
Mleta mada muongo ziwatanganyika kwasasa hakuna meli iliyokarabatiwa na inayokarabatiwa wala hakuna meli mpya inayoundwa kwanza kwahapo tu wewe nimuongo pia tumesema muda mwingi maendeleo yanapendwa ndiolengoletu lakini kunautaratibu tuliojiwekea haukufwata inatowa mwanya kuonesha kunamatumizi mabaya ya ofice unatakiwa ulijue hilo chadema iliukombozi upatikane inawapenda kanda yaziwa inawaihitaji haiwachukii tafuta namnanyingine uwachonganishe.
 
Mtoa mada, unapoandika bandiko lako humu jukwaani, kwanza jitathmini ndio uandike ndugu yangu, unapozungumzia suala la uwanja wa ndege ujue unazungumzia moja ya vitu vikubwa sana ambavyo vina gharimu ma bilion ya pesa, sasa ujue kuna vitu viwili inatakiwa uvifahamu.

1: Kuwekeza pesa
2: Kuzika pesa

Sasa unapozungumzia suala la uwanja wa ndege wa chato , kimsingi ni lazima tukubali kwamba ule sio uwekezaji bali ni uzikaji wa pesa , tafsir halis ya kuwekeza ni kwamba unawekeza sehemu ambapo kuna shughuli fln za kiuchuni zinafanyika, sasa kama utatumia mabilion ya pesa kwenda kuweka kitu ambacho ni kwa manufaa yako ww binafs maana yake huo sio uwekezaji bali ni uharibifu wa pesa za uma.

Binafs sina chama na wala sijishughulishagi na mambo ya siasa ila pale penye ukweli sina budu kufanya ivyo kama mtanzania mwenye mapenzi na nchi yangu, pesa kama ile angeamua kuipeleka kwenye miradi ya maendeleo ingemjengea sifa kubwa sana sababu ni miongon mwa vitu ambavyo angeweza kuviongea kwenye ilan ya chama chake, lakin kwa kile alichokifanya hawezi akasimama mbele ya watu akaongea kwamba moja ya maendeleo aliyoyafanya ni pamoja na kujenga kiwanja uko kwao.

Kwaiyo kujenga viwanja 11 ni jambo jema sana na la kimaendeleo lakin je! viwanja ivyo umevijenga wapi? sehemu ulipojenga kuna shughuli za kiuchumi zinaendelea uko? kwaiyo ndugu yangu tusiongee kishabiki bali tuongee kwa mapenzi ya tanzania na inapendeza ukiwa mkwel zaid ili hata kama mh atakuwa anasoma makala zetu atayafanyia kazi aya tunayoyazungumza hapa, msipende kusifia kitu ambacho kina muharibia mtu uwajibikaji , inatakiwa tuwe wawazi ili ajue na apate kuyafanyia kazi aya tunayoyazungumza. Mungu ibariki Africa , Mungu ibariki Tanzania & Mungu mbariki rais wetu mpendwa Dr John
 
Kwa sasa ziwa Tanganyika halina meli hatamoja inayotoa huduma ya abiria watu wanakufa sana tu kwakukosa huduma hiyo alafu unachukua melikibao unapeleka upande1 hilisio sawakabisa.
 
Watu hawali Madaraja ,hivi CCM mmeshindwa kabisa namna ya kufikiria nje ya Madaraja na Mabarabara !?
Walidanganywa kuwa madaraja ndiyo itakuwa kete yao ya ushindi, kumbe wameingizwa chaka.
 
Unapomwacha mwanao avae suruali iliyotoboka huku unanunua iPhone ya M.2 huo ni upumbavu.
Tundu Lissu anapinga ule ujenzi wa Chato Airstrip uliogharimu mabilioni bila sababu maalumu
Umemsahau kukemea pia na plan yao ya kujenga uwanja mkubwa wa mpira pale chatou eti utakuza utaliii.

Yaani watalii waje kuushangaa uwanaja wa mpira ambao ramani yake tunaitoa huko huko kwa watalii.
 
Nani kasema Tundu Lissu anachukia maendeleo ya Kanda ya Ziwa? CCM mmeishiwa hoja sasa mmeamia kwenye kutunga propaganda ili kuwagawa Watanzania.

Sasa kwa taarifa yenu hiyo divide and rule yenu haitofanikiwa kamwe. Mwambieni huyo muhutu wenu kuwa kanda ya ziwa tunajielewa na hatutapiga kura kikabila wala kikanda mwaka huu!

Tunaenda na Tundu Antiphas Lissu tu!
 
Nadhani Chadema Wana sera kabisa ya kuponda Kanda ya ziwa

Aliyewaambia mlichaguwa upinzani ndio maana sikuleta maendeleo shinyanga

Aliyesema mkichaguwa nje ya ccm mtaniona akiwa shinyanga

Aliyechukuwa fedha za msaada kagera kwa maafa ya tetemeko

Au kagera na shinyanga sio kanda ya ziwa?
 
Watu wa Kaskazn ni wabinafsi Sana. Wanataka kuona maendeleo kwao tu, ndio raha yao. Lami ziliingia had vijijin miaka ya 80 pamoja na umeme. Yaani Kilimanjaro bwana wabinafs san
 
Mmeanza kutumia ukanda, magu hana mpango na kanda ya ziwa, yeye mpango wake ni chato.watu wa kanda ya ziwa wanasema jpm alianza ubaguzi tangu akiwa waziri wa ujenzi.
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom