Kwanini tunawanyamazia wanaoanza kupandikiza mbegu ya kutaka kuharibu amani yetu ambayo tumejivunia kwa miaka mingi?

Landson Tz

JF-Expert Member
May 8, 2011
295
221
Ni muda sasa unaendelea kupita tangu baadhi ya watu wakiwemo viongozi hasa wabunge wakijitokeza hadharani na kutoa kauli za kuvunja katiba bila kuchukuliwa hatua zozote za kisheria.

Wabunge wa bunge lilipita wakiwemo na hata hili la sasa wanajitokeza kwenye vikao vya bunge na kutaka kumshawishi na wengine wanatamani kumlazimisha Rais wetu kuvunja katiba ili kutawala mihula zaidi ya miwili.

Ikumbukwe kuwa machafuko mengi yanayotokea Afrika yanatokana na watawala kung'angania (wengine wanaita kung'ang'anizwa) madaraka.

Kazi anayoifanya Rais wetu ni nzuri lakini akimaliza muda wake hatuta shangaa anapatikana Rais mwingine ambaye anaweza kufanya mazuri zaidi ambayo hata Rais mwenyewe atafurahi kuya shuhudia.

Kutokana na mfumo mzuri wa kutawala kwa mihula miwili, mmoja baada ya mmoja iliyo asisiwa na baba wa taifa ni mfumo mzuri ambao ni kiwango cha kimataifa tuulinde na kuu heshimu.

Watanzania tuwekeze katika kujenga mifumo imara na si kujenga watu imara, maana watu wa Mungu waliumbwa kwa udongo!!

Naomba nitowe rai kwa wanao kereketwa na kutoa kauli za kuvunja katiba, kuchunga sana mihemuko yao maana taifa likiangamia historia haita waacha salama.

Mwisho: Nashauri serikali, wana harakati na wanasheria wetu kuweka utaratibu wa kuwafungulia mashika watu wa namna hii na kufungulia mashitaka ya kuvunja katiba na hatimaye adhabu kali itolewe ili iwe fundisho kwa wengine!!

Naomba kuwasilisha.

Landson Tz
 
Ungeeleza mtu kasema nini basi ungeweza kueleweka. Vilevile kitatiba bunge ni huru simlitaka bunge la chama kimoja sasa matatizo ya nchi yapo hakuna wa kusingizia tena😂
 
Ungeeleza mtu kasema nini basi ungeweza kueleweka. Vilevile kitatiba bunge ni huru simlitaka bunge la chama kimoja sasa matatizo ya nchi yapo hakuna wa kusingizia tena😂
Nazungumzia wale wana taka kubadirisha katika ili kuruhusu Rais Magufuli kutawala mihula zaidi ya miwili ni kinyume cha katiba yetu na utamaduni wetu .
 
Ujue mpaka inafikia kiwango cha katiba kuchezewa na kufanyiwa hujuma jua kwamba uongozi wa juu umeisha jua wananchi wa nchi husika ni malofa sana , wajinga , wapumbafu, hawana misimamo na umoja na pia taasisi zote kuanzia mahakama, bunge, polisi, jeshi mpaka usalama wa taifa uko upande wao na wana maslahi mapana na huo ufedhuri
 
Kushawishi kutendeka kosa, ni kosa. Utafutwe utaratibu wa kuwashataki nguchiro wote wanaoshawishi katiba kuvunjwa.
 
Kushawishi kutendeka kosa, ni kosa. Utafutwe utaratibu wa kuwashataki nguchiro wote wanaoshawishi katiba kuvunjwa.
Hilo litafanikiwa tu endapo wakiwa na ujasiriwa kujiondea kinga walizojiwekea.
 
Wana chama wa CCM wengi ni wapuuzi, akianza kuongea utadhani vifaa vya ujenzi vimeshuka bei, mazao yamepata soko la uhakika, kumbe ni aibu kubwa sababu tu anaona yeye analipwa pesa nyingi ana assume kila mtu analipwa kama yeye
 
Ungeeleza mtu kasema nini basi ungeweza kueleweka. Vilevile kitatiba bunge ni huru simlitaka bunge la chama kimoja sasa matatizo ya nchi yapo hakuna wa kusingizia tena😂
Wana singizia TRA utadhani ipo chini ya CHADEMA kumbe ndiyo hao kila siku wanapongezwa kwa kuvunja record ya mapato hewa.
 
Ujue mpaka inafikia kiwango cha katiba kuchezewa na kufanyiwa hujuma jua kwamba uongozi wa juu umeisha jua wananchi wa nchi husika ni malofa sana , wajinga , wapumbafu, hawana misimamo na umoja na pia taasisi zote kuanzia mahakama, bunge, polisi, jeshi mpaka usalama wa taifa uko upande wao na wana maslahi mapana na huo ufedhuri
Tunaendeshwa kwa amri sasa hivi hakuna cha nini wala nini mkuu
 
The political constitution is not a spiritual doctrine it is regularly amended in compliance to the requirements of the present conflicting time........
 
Back
Top Bottom